TCU na wizard ya elimu siwaelewi

TCU na wizard ya elimu siwaelewi

Waliosoma diploma ya maabara, au Pharmacy hawaruhusiwi kusoma MD, Kwa wakati huo huo aliyemaliza kidato cha sita anaruhusiwa hivi nini hoja yao kuhusu hili?
Nadhani umejikanganya hapo.
Vigezo vya kusoma degree zote hapa Tanzania viko vya namna mbili. Kuna kigezo cha moja kwa moja (direct entry) hiki kinamuhusu mwanafunzi aliyemaliza kidato cha Sita na kufikia ufaulu wa kuingia chuoni kwa kozi husika. Kwa kozi zote za afya kwa sasa ni lazima awe kidato cha Sita awe amesoma PCB (ukiondoa Environmental health science ambapo hata CBG inakuruhusu). Na kuna kigezo cha kuzunguka (indirect entry) kinamhusu mhitimu wa diploma wa kozi ile ile ya degree anayotaka kusomea.

Kwanini Diploma ya Maabara, Famasia au Uuguzi nk haziwezi kuruhusu kusomea MD? Jibu ni moja tu, Diploma hizo hazikumuandaa mhusika kuja kusomea au kufanya kazi za fani ya MD.

Hali ni hiyo hiyo pia ikiwa mtu kasomea diploma ya Medicine halafu akataka kuja kusomea degree ya Maabara, Famasia au Uuguzi, hataruhusiwa.
 
Acha ujinga wewe.
Aliyesoma diploma ya Pharmacy Kuna digrii yake na aliyesoma maabara kuna digrii yake, kwanini unataka uchanganye mambo. Yaani ni sawasawa eti mtu kasoma diploma ya Sheria eti akasome sociology.

Wale wa form 6 wanasoma Physics, Chemistry na Biology ambapo unawapa nafasi ya kusoma kada ya afya anayoitaka kutokana na ufaulu aliopata.
Kwani wenye diploma hawajasoma form six boss?
 
Hawajasomaa ndio na kama walisoma basii walifelii na kama walifelii ni sawa na haakusomaa
Kuna waliofaulu wakachaguliwa vyuo vikuu kozi ambazo hazina soko,mtu anaona bora akasome kozi ya afya ngazi ya diploma sababu ya ajira. Nina jamaa yangu alisoma degree ya ualimu mpaka kamaliza,akaamua kwenda kusoma diploma ya Afya.
 
Acha uongo wewe huwezii kwendaa kusoma diploma ya pharmacy bila kuwa na angalau D ya physics
Kwa diploma physics haiangaliwi, tafuta guidebook usome, sio unaropoka tu
 

Attachments

  • IMG_20230711_145807.jpg
    IMG_20230711_145807.jpg
    19.6 KB · Views: 13
Back
Top Bottom