GE2010 TCRA na makampuni ya simu wanavyokata michango kwa ajili ya CCM

GE2010 TCRA na makampuni ya simu wanavyokata michango kwa ajili ya CCM

Wana jf msidangayike na watu wanaotumia mtandao huu kutisha watanzania.
Ndani ya tanzania sheria zinafuatwa kikamilifu na tcra pamoja na mitandao yote na watoa huduma mbalimbali za "vas" wanafuata taratibu zilizowekwa na tcra kikamilifu.

Kumekuwa na ujumbe unaosambazwa unaosema:
"tuma neno hapana kwenda 15016 uone maajabu" huku wengine wakisema mitandao na ccm zinachukua fedha za wateja kwa wizi - yaani ujanja ujanja.

1. Hii namba ni ya bure hai chaji hata sent moja - jaribu ukikatwa nenda kadai utarudishiwa hela yako
2. Hii ni namba ya mawasiliano.
3. Ukituma neno ccm au chochote - utaambiwa asante kwa kujiunga.
4. Ukituma neno ndio - utaambiwa "asante kwa kujiunga na huduma hii ya changia ccm na ushinde zawadi kati ya pikipiki 64, baiskeli 200 na millioni 45 kutoka ccm. Kujitoa tuma neno hapana kwenda 15016"
5.ukituma neno hapana - utaambiwa asante kwa ujumbe wako, utaondolewa kwenye huduma hii ya changia ushinde na ccm.

Tcra na mitandao vinajua hii namba inafuata sheria zote ndio maana haitahangaika na wazushi wasio fikiria bali kuropoka ropoka tu. Hawa inabidi tcra na polisi iwashughulikie kwani ni kosa la jinai kuanzisha false panic alerts kwa jamii.

Lakini pia kumbuka kila unapotuma neno lolote kwenye namba hiyo tayari unakua kwenye database ya ccm. Wakikutumia ujumbe wowote rpomosheni au mawasiliano usije lalamika maana umeingia anga zao.

Kumbuka haya majibu yote yamewekwa kwenye computer na inakujibu kufuatana na ulicho andika.

Guys hakuna wizi hapa - acheni kudanganya watu bure.

Vinginevyo baada ya kutuma neno lolote kwenye hiyo namba, nenda tcra na majibu uliyopata ukashtaki, kama watakuuliza ulifuata nini kwenye hiyo namba na unataka wakusaidie je.
unapata percent ngapi, maana CCM ni wazee wa percent
 
.........Ndani ya tanzania sheria zinafuatwa kikamilifu ..............


Guys hakuna wizi hapa - acheni kudanganya watu bure.

Una umri gain wewe!
Sheria zinafuatwa. Sheria zipi na nani anafuata? Najua vibaka wa Manzese wanaogopa sheria lakini Kinana anafuata?, Lowasa anafuata? Makamba anafuata?

Usiseme hakuna wizi. Nani aamini. CCM wako desperate na uchaguzi. Ulizia Wizara zote uone kama wamepewa pesa za shughuli za serikali. Imefikia wizara hazina hata pesa za kununua karatasi. Kisa ni uchaguzi.

Lakini tunafahamu uchaguzi umefadhiliwa na una bajeti yake. Hawa CCM wenzako wanakomba kila wanachokiona karibu.
 
....mchunguZI uko sahihi kabisa!!! Sheria ni kwa kibaka wa Manzese tu si kwa kikwete au miraji au rizi1 au makamba! wizara zimekaukiwa mbaya sana. OC (other charges) za mwezi wa 8, 9 na 10 katika vituo, idara, taasisi za serikali ni kituko. kuna waliotumiwa milioni 2. ukiuliza, unaambiwa bootlickers wa CCM wamepewa order kama kuna fungu linashangaashangaa linabebwa kwenda kwenye kampeni yet unabana pua mtoto wa kiume eti 'CCM inafuata sheria'!!!
 
achaneni na huyu ****, amefadhilwa na mafisadi, ajue hapa ni kwa great thinkers, hapa siyo kwako nenda kaendelee kulamba viatu vya makamba
 
****, ni mtu anayetumiwa bila kujua kuwa anatumiwa, kwa hasara yake mwenyewe na kwa faida ya anayemtumia
 
TCRA Wanapaswa kutoa maelezo ya Kutosha iweje Mlaji wa Huduma ya Mawasiliano akamuliwe Pesa Pasipo ridhaa yake?
 
TCRA+VODACOM+MAKAMPUNI YA SIMU YANAVYOKATA MICHANGO KWA AJILI YA CCM
Napenda kuchukua fursa hii kuutarifu umma wa watanzania unyonyaji unaofanywa na makampuni haya ya simu bila hata watanzania kugutuka ili wote tuone kama kuna fair play katika uchaguzi huu
1. Baada ya changia CCM kwa sms kushindikana sasa wamebuni njia mbadala nayo ni kutoza asilimia 10% ya kila salio unaloweka na linakatwa wakati unapopiga simu nao sio instant…kama tulivyozoea na hii ni kwa wateja wa simu zote kama hupendi kuendelea kuchangia mafisadi tafadhali tuma neno HAPANA kwenda namba 15016 (Hii ndio proof ya ninachosema) Huu ni UONEVU WA WAZI WAZI
2 Baada ya ujumbe wa kashfa ambao TCRA waliukanusha kuwa hawahusiki tena kupitia TV ya TBC asubuhi wakati wa kipindi cha jambo leo Uchunguzi wangu wa siku tatu umeonyesha kuwa kati ya watu mia niliozungumza nao walioutumiwa ujumbe ule wa kumkashifu Dr Slaa basi 100% wanamiliki mtandao wa Vodacom(TCRA MTUJIBU HIZI NAMBA ZOTE ZILIPATIKANA WAPI?)


Kaka, ninamiliki namba za Tigo na Zain (Airtel). Je, hata sisi ambao hatuko kwenye mtandao wa VodaCom, nasi tunakatwa huo mchango bila hiari yetu?

Nimetuma neno HAPANA kwenda namba hiyo, 15016, kupitia namba yangu ya Tigo, lakini sikupata majibu.

Au wameshtuka, sasa hawajibu baada ya sisi kugundua tunaibiwa?

Asante kwa taarifa.
 
ni kuhujumu wafuja jasho..menejimenti ya TCRA wanastahili kuwajibika ktk hili..
 
Back
Top Bottom