TCRA huu wizi wa Makampuni ya simu mbona mmeufumbia macho? Angalieni Airtel

Wanacompasate kodi na ma fine waliyopigwa na serikali ya awamu ya 5
 
TCRA&mitandao ya simu ni genge la wahuni linalofanya kazi kwa weredi kumshughulikia mTz.
Muhasibu wa 'tusiaraei' ndo huyo anamiliki magari ya maana ya kwenda mikoani. Sasa hivi ana maji yake ya kunywa unategemea nini?!
 
Hiyo sms inakuja hata kama huna MB hata 1 kama mm sina data kama wk na najiunga halotel lakini kila siku naletewa sms kama hiyo
Mkuu unafaidika nn na huu utetezi wako? Watu wako serious wewe unaleta propaganda. Sms gani inakuja na idadi ya MB kama haujajiunga? Yaani nijiunge 1024mb then niambiwe nimetumia kadhaa zimebaki kadhaa halafu unasema ni sms ya kila siku. Basi angalau ungeona ubovu wa system yao kutoa taarifa za uongo, hilo nalo unatetea.
 
Kuna wakati Airtel unapata message kwamba bando lako limeisha wakati bado lipo!!

Sometimes wanakuwa off kwenye intenet kwa masaa kadhaa. Kama una bando la siku wakirudi na muda wako wa bando unakuta umeisha😂

Airtel inabidi waweke option kama hii mpya ya TIGO ya ku carry forward MB zako kama bado zipo na muda wake una expire!!
 
Chief. Nakuunga mkono ili swala sasa ni too much hata tigo wanacho haka kamchezo, nikikuwa na bundle la almost 2GB jana natazama salio lika soma 1Gb na vi mbs. Leo asubuh naambiwa umebakiza 284mbs nikashangaa sanaa na ukitazama
Matumiz ni ya kawaida tu. Kiukweli haya makampun yana fanya ujanja ujanja
 
Airtel nshawakimbia..kuna siku walinilamba 3gb ndani ya 2hrs nikasema huu ni upumbavu..net yenyewe haipo stable!!

Voda japo bundle linatembea sana lakini net yao haiyumbi yumbi, mwisho wa siku nimeona nifunge ndoa na voda tu.
Voda ndo bure kabisa siwataki hata.
 
Voda wana gharama kubwa lakini huduma zote zina viwango vya mwafrika
Kupiga
Sms
Internet
Mobile bank
 
Mm sijatetea kitu sababu hata silipwi,nimejibu hoja kwa hoja na ushahidi nikatoa sasa natetea nini? Mm nasema sababu ni mtumiaji wa Airtel sana.
 
Voda iko vizuri
hayajakufika hawa Voda ndio malejendari wanaiba mpaka salio la kawaida,sitaki hata kuwasikia.Bundle zenyewe ni ghali sana tena zile offer unaweza kupewa leo au wiki nzuri baada ya hapo zinakuja za hovyo kabisa ni dk tu Mb kiduchu.
 
Huko kwenye kuzingatia neno TAKRIBAN sijakuona kwenye maelezo yako.. Au kwako neno takriban lina maana gani kwenyw wizi huu..!?
 
Inabidi tuanzishe movement haya makampuni yamefumba masikio wanapewa faini hawaelewi.
 
Hili swala la kusema mitandao wanaiba MB inawezekana lina ukweli kulingana na anaesema ameonaje yeye mpaka kufikia kusema hivo.
Ila kwa upande wangu naona sasa hivi mitandao ya kijamii imekua mingi watu mnazurura mitandao yote, bado kuna apps zinazokula data background, sijui vitu gani vinaji update huko kwa simu yako ambayo hujui kuitumia unajua kupiga, kupokea na kupita mitandaoni.

Mtandao kama voda hauna kugoma goma mfano ukiingia instagram picha na video zinafunguka chap kwa haraka lazima MB zikimbie tofauti na yule anaetumia mtandao unaogoma goma.

Honestly sidhani kama wanaiba matumizi ya data ya miaka naona yamekua tofauti ukilinganisha na kipindi kile tunapewa MB 100 unakaa nazo hata siku tatu sababu tulikua tuna whatsapp tu ukienda sana Jf, Twitter au Facebook
 
Gharama ziko juu.

Ila hawaibi.
 
Na hapo kwenye kutumia takribani 90% kuna mdau mmoja kaelezea vizuri ambae hajaelewa ndio itakua tu kichwa kigumu hata darasani wanafunzi hawaelewi wote.
Kuna wakati mimi ikija hiyo msg ya 90% unakuta wananiambia mb zilizobaki 85, wakati mwingine 94 wakati mwingine 68 n.k

Na kujua salio lako lilobaki pia menu imetolewa hapo juu. Labda kosa lao hapo kubadilisha mfumo wa menu ya kuulizia salio bila kutoa taarifa kwa wateja.
 
Huko kwenye kuzingatia neno TAKRIBAN sijakuona kwenye maelezo yako.. Au kwako neno takriban lina maana gani kwenyw wizi huu..!?
Usitumie nguvu kuelewa! Mbona nimeandika pale mbele kwamba matumizi ya hilo neno hayahalalishi wizi huo?

Nimekwambia usicalculate asilimia halisi walizotaja kwakuwa wametumia neno takribani au hujui matumizi ya neno takribani?

Ni hivi; neno hilo linatumika kwenye makadirio hivyo ukiona neno takribani (almost) maana yake haijatimia vizuri (about to) au imezidi kidogo (not less than) na wala siyo halisi (not exactly).
 
Pamoja na neno takriban, zikiisha hizo 87 unakuwa huna MBs.... Sasa unaposema nisi-calculate kwa kutumia asilimia, SASA UTAJUWAJE KAMA UMEIBIWA? Maana ya uzi inapotea
 
Huu wizi umerudi upya airtel
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…