TBS na Serengeti Global, huu ni wizi wa wazi na hatutakubali

Mtimti

JF-Expert Member
Feb 23, 2008
942
644
Nimesoma taarifa kuwa TBS wamewapa tenda kampuni ya SERENGETI GLOBAL SERVICE ya London kuwa wakaguzi wa magari yote yanayotoka uingereza na kuyatoza gharama ya dola za kimarekani 200. Nikiwa kama mkazi wa Uingereza na nikiwa kama mdau wa usafirishaji wa magari nasema wazi kuwa hiki kitu hakikubaliki, na ni kutuletea usumbufu usio na sababu sisi watanzania tunaokaa mbali London. Tbs inaonesha hawajui wanachokifanya au wameshinikizwa kuwapa tenda Serengeti kwa sababu za kisiasa au wanaendeleza upuuzi waowaliofanya siku za nyuma hapa uingereza.

Kipindi cha nyuma magari yalikuwa yanasafirishwa bila kukaguliwa,baada ya Tbs kuanzisha utaratibu wa magari kutoka nje yanayoingizwa Tanzania yawe yamekaguliwa ndipo hapa Uingereza deal hilo akapewa mtoto wa aliyekuwa mkurugenzi wa TBS (Mamamutabazi(R.I.P)), huyu kijana alikuwa ana kiofisi chake London hivyo ukiwa nagari yako unataka kusafirisha na upon nje ya London ulikuwa unamtafuta kwa simu na mnalipana kisha anakutumia cheti. Hivyo kulikuwa hakuna ukaguzi wowote bali ni ulaji tu alikuwa amepewa kijana . baada ya miaka kadhaa TBS walimnyima huyujamaa kutoa hii huduma .

Kwanini sikubaliani na TBS kuwapa zabuni hii(sijui kama kweli wameshinda tenda au wamewapa tu kama walivyompa mtoto wa mama mutabazi)

Magari yote yanayokuja t Tanzania kutoka u Uingereza huwa lazima yawe na M.O.T(ministry transport test), hii inakuwa nitest kwa gari yako kama ina viwango vya usalama barabarani na usalama wa mazingira, maana kuna mitambo ambayo ni computerized inayolipima gari lako kuanzia engine mpk moshi inaouzalisha kisha unapewa certificate kutoka DVLA(driver and vehicle licensing agency), hawa dvla ndio wanaotoa leseni zote za udereva hapa uingereza. Hivyo basi hapa utaona kuwa magari yote yanayokuja Tanzania kutoka uingereza huwa yana viwango na yanafaa kwa matumizi ya barabarani maana hakuna mtu anayenunua gari ambayo haijapass MOT

Kwanini Serengetihawakidhi vigezo?

Serengeti hawana mtambo wa ukaguzi wa gari tofauti na ukaguzi unaofanywa na mawakala wanaofanya MOT hapa uingereza. Mitambo wanayotumia na cheti watakachotoa ni sawa na cheti ntakachopata sehemu yoyote hapa uingereza nikipeleka gari yangu kuifanyia ukaguzi. Hivyo hapa utaona kabisa kuwa TBS wamewapa jamaa njia ya kutuibia pesazetu

Serengeti wana ofisi moja tu tena ipo hapo tilbury(east london) na ina wafanyakazi hawazidi watano,je inaweza kuhudumia kila mtanzania aliyepo kona za uingereza? Kumbuka uingereza ina bandari zaidi ya nne .na kwanini nifuate hii huduma London wakati mi naishi nje ya London na huku nnapoishi kuna bandari na huwa naitumia? Hata kama waoSerengeti wanasema wana mawakala u Uingereza nzima (kitu ambacho si kweli, )basi hao mawakala si ndio hawahawa tunaowatumia kila siku kufanya MOT ambao wao wanachaji pounds 30-50?.....kama kuna ukaguzi wanaofanya ni tofauti na wanavyofanya ukienda kupasisha gari yako kwenye MOT basi chris lukosi aje hapa aseme na mimi ntakuwa wa kwanza kumuomba msamaha

Ushauri wangu kwa serikali na pia watu wenye dhamana basi walikemee hili, serikali ifikie mahali iwe inafikiria njia za kutupunguzia mizigo sisi wananchi tunaoishi nje na sio kutuongezea gharama zisizokuwa na sababu. Ushuru tu wa gari upo juu sana halafu bado hawa TBS wanatuongezea huu upuuzi wa kuwapa watu ulaji kwa kutunyonya kimacho macho.

Hili suala siku si nyingi ntatafuta waandishi na radio stations za Dar ili niliseme vizuri..aksanteni
 

Attachments

  • tbs.jpg
    tbs.jpg
    96.1 KB · Views: 417
Mkazi wa uingereza mjini ama vijijini?Hujui ni dharau kuandika jina la nchi kwa herufi ndogo?
Nahisi harufu ya mgongano wa maslah hapa kwa hiyo malizaneni juu kwa juu hapa nyumbani tuna mambo mengi tu yanayotusibu hizi tenda za kukagua hata midoli peaneni tu hazituhusu!
 
Mkazi wa uingereza mjini ama vijijini?Hujui ni dharau kuandika jina la nchi kwa herufi ndogo?
Nahisi harufu ya mgongano wa maslah hapa kwa hiyo malizaneni juu kwa juu hapa nyumbani tuna mambo mengi tu yanayotusibu hizi tenda za kukagua hata midoli peaneni tu hazituhusu!

Si lazima kuchangia, ungepita kimya kimya ungekuwa muungwana zaidi
 
Mtimti,

Brotherly Advise:
Unamjua Chris Lukosi, ungemwita kwanza uongee naye kwanza halafu ndiyo ujue mambo yenyewe yalivyo. Hii biashara ya mwenzio usiharibu!! Look for another business, hiyo kapata mwenzio mpongeze na umsaidie afanye vizuri!!.

Hata hivyo umefanya advertising kwake!!
 
hahahah...wonders never cease in this beloved country of ours. Hivi Chris Lukosi na kulialia kooote humu dhidi ya Chadema na kuipamba CCM..all HE wanted was this tender/business opportunities? Ama kweli...kua uyone..siyo maghorofa.......cant believe hawa ndo diaspora.....wenye so called mawazo mpya....by he ay ni huyu huyu Lukosi alimpiga vita sana Willy Mutabazi aliyepewa tender mwanzoni..

All I can say yana mwisho....
 
Mtimti,

Brotherly Advise:
Unamjua Chris Lukosi, ungemwita kwanza uongee naye kwanza halafu ndiyo ujue mambo yenyewe yalivyo. Hii biashara ya mwenzio usiharibu!! Look for another business, hiyo kapata mwenzio mpongeze na umsaidie afanye vizuri!!.

Hata hivyo umefanya advertising kwake!!

Mi sina sababu ya kuharibu biashara yake ila nnachopinga ni kulipishwa dola 200 kwa ukaguzi ambao unafanywa kwa pounds 35 (chini ya dola 70) na kupewa hati ambayo nnayo na ipo valid kwa kipindi hicho.
Na hii kampuni haina mtandao mpana wa kuwafikia watanzania wote wanaoishi UK. hivi leo kama mtu yupo Scotland anataka kusafirisha gari yake Tanzania watamfikia vipi huyu mtu kukagua gari yake? Kama sio kumwambia awe na MOT certificate then wao wamtumie cheti tu chenye nembo ya kampuni yao na kumchaji hizo dola 200
 
kwa maneno mengine TBS imewapa tenda CHADEMA DIASPORA. Kwa hili nawapongeza walau sasa watakuwa na vyanzo vya pesa nje ya nchi baada ya yule jamaaa kufungwa kule Arusha. Wakati huo huo wanasema kuwa Waziri husika Abdalla Kigoda kala pesa zaodi ya dola laki 2 za rushwa kwa ajili ya hii tenda.


Nchi hiii naona bora kila mmoja ale chake tuuuu gamna namna
 
Ndio maaana Criss simuoni humu siku hizi, kumbe tenda zimeongezeka sasa, inabidi uwashawishi wakubali na uraia wa nchi mbili Criss.
 
kwa maneno mengine TBS imewapa tenda CHADEMA DIASPORA. Kwa hili nawapongeza walau sasa watakuwa na vyanzo vya pesa nje ya nchi baada ya yule jamaaa kufungwa kule Arusha. Wakati huo huo wanasema kuwa Waziri husika Abdalla Kigoda kala pesa zaodi ya dola laki 2 za rushwa kwa ajili ya hii tenda.


Nchi hiii naona bora kila mmoja ale chake tuuuu gamna namna

Sijajua kama ulichokiandika ulidhamiria au ni vile tu hauna taarifa sahihi. Labda ungejiuliza hao wamiliki wa Serengeri Global Services Ltd ni wanachama wa chama gani. Wakati mwingine kukaa kimya huficha mambo mengi.
 
Tostop to use Serengeti Global Services (LTD) in UK for Vehicle Inspection beforeShipping to Tanzania



2Q==




Diaspora Uktz
London, United Kingdom



SAY NO TO DOUBLE TAXATION BY THE TANZANIA GOVERNMENT (TBS)
From the 16 March 2015 the Tanzania Government in conjunction with the TanzaniaBureau of Standards (TBS) have announced a new scheme relating to the processof exporting cars from abroad.

UK residents are required to provide their vehicles to an appointedindependent agency namely Serengeti for inspection before they are consideredsafe to be shipped to Tanzania. This process will cost $200.00 per car.
However, every car owner in the UK is required by law to undergo thesame process this new scheme is providing in regards to the vehicles they own.This test is conducted by the UK Ministry of transport for vehicle and roadsafety and costs £50.00 per car. The process is completed by a highly qualifiedagent utilizing unique engineering equipments for the purpose. These arequalified and very competent agents with years of experience and reliabilitybehind them and operates within highly acceptable standards the world over.
Now, considering that our cars (Tanzanians living in the UK) havealready been certified safe by qualified and experienced agency, we fail tounderstand the purpose of this scheme.
Tanzanians who reside in the UK rejects this idea in the strongest andabsolute terms, for, we feel that, it is wrong, unfair and very questionable inevery sense of imagination. We strongly feel that this scheme has got nothingto do with safety standards but a dubious operation to make money that will notbenefit our country or our people in any practical aspect.
We therefore request the Government of Tanzania to abandon this exercisewith immediate effect as it is an absolutely unnecessary exercise which willbenefit no one other than the authors of this scheme
Letter to
Tanzania Goverment
Foregn Affiars
Tanzania Bureau of Standard (TBS)
To stop to use Serengeti Global Services LTD in UK for VehicleInspection before Shipping to Tanzania
 
Hivi huyo Christ Lukosi bado yuko Chadema au kasharudi CCM?

Nashukuru sana TBS kuwapatia hii tenda CHADEMA
 
Kwa mtu anaekaa Glasgow nae inabidi gari alipeleke kwenye ofisi zao Tilbury au inakuwaje?

How practicable is it for all the residence wanaokaa sehemu mbalimbali za UK na wanatumia different agents.

Na certificate ya roadworthy ya UK ina matatizo gani ambayo hipo kwenye database ya taifa?

Yaani hawa jamaa kwa kodi, lakini hakuna anaefikiria kupunguza matumizi ya posho za serikari. Kupunguza matumizi pia ni namna moja wapo ya kuongeza kipato cha maendeleo na miradi sio kila siku kodi tu na charges kila kukicha.

Tuna maraisi na wizara luluki mpaka mawaziri wengine atuwajui sisi raia, huko kwenye serikari za mitaa ndio salalee inafikia hatua raia are confused who is responsible for what, mkuu wa mkoa anawaambia watu wahame, mayor anasema wabaki alikadhalika madiwani ndio wanaogawa viwanja kwa matumizi: kasheshe wote hao wana maofisi kwa gharama za walipa kodi.
 
Waswahili tujizoeze kuwa tunaandika kiswahili tu kwa sababu kiingereza kinatugonga sana.

Hata hivyo tatizo la wasafirisha magari wa UK kwenda Tanzania linatokana na mfumo dhaifu wa nchi yetu ambapo sheria inaweza kutungwa kwenye deski la bosi badala ya bunge.

Ninadhani kuwa hili la kutaka Serengeti Freight Forwarders ndio wawe na exclusive rights kuhusu magari yanayotoka UK kwenda Tanzania ni matokeo ya rushwa tu, ikiwa ni nje kabisa ya sheria za nchi.
 
Hata hivyo tatizo la wasafirisha magari wa UK kwenda Tanzania linatokana na mfumo dhaifu wa nchi yetu ambapo sheria inaweza kutungwa kwenye deski la bosi badala ya bunge. Ninadhani kuwa hili la kutaka Serengeti Freight Forwarders ndio wawe na exclusive rights kuhusu magari yanayotoka UK kwenda Tanzania ni matokeo ya rushwa tu, ikiwa ni nje kabisa ya sheria za nchi.
Maajabu na nchi nyingine nazo mbona hakuna checks za mara mbili na wakala kitanzania kuhusika au magari yanayotoka UK ndio mabovu sana.
 
Bosi wa hii kampuni ni kamanda wa CHADEMA UK.

Safi sana mkuu. Na ile CHOPA itabidi isafirishwe na SERENGETI GLOBAL

 
Last edited by a moderator:
Mkuu ulieleta hii dhread, jaribu kurekebisha kidogo ili isomwe kiurahisi.

Hata hivyo hii "milking scheme" ipingwe kwa nguvu zote na watanzania wote wale wasogusa na mirija ya ufosadi na wale walokabwa na mirija hiyo.

Mkuu Chris Lukosi naona amesotea kweli hii deal maana alipigwa chini alipokwenda CHADEMA na baada ya kurudi CCM amepewa hii tender.

Huu ni UFISADI na unafanyika mchana kweupe. MOT sehemu zingine bila service inafanywa kwa hata paundi 27! ikiwa ni bei ya offer.

Kama hakuna ataketoa pamba masikioni kusikia hoja hii basi itabidi kuvitaarifu vyombo vinavohusika hapo UK na ikiwezekana hao Serengeti wachunguzwe biashara yao.

Mimi ntakuwa mmoja wa wafuatiliaji wa karibu wa hii issue.

Tumechoshwa na tabia hii ya UFISADI wa kijinga ambao umetapakaa hadi nchi za watu.
 
Bosi wa hii kampuni ni kamanda wa CHADEMA UK.

Safi sana mkuu. Na ile CHOPA itabidi isafirishwe na SERENGETI GLOBAL



Hapana, nadhani wewe unaishi dunia ya Dinosaurs. Mzee Lukosi Alishajitoa Chadema takribani miaka mitatu sasa; mpaka leo yeye ni kada wa CCM damu damu. Pitia threads nyingi humu JF utaelewa ninachoandika; dunia ya siku hizi inabidlika the speed of light. Na wewe unatakiwa kuwa informed kwa spidi hiyo hiyo.
 
Last edited by a moderator:
Bosi wa hii kampuni ni kamanda wa CHADEMA UK.

Safi sana mkuu. Na ile CHOPA itabidi isafirishwe na SERENGETI GLOBAL



Yupo ccm baada ya kula rambirambi za mar mwangosi
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom