TBC1: Ukweli wa yaliyojiri Arusha

Mwisho wao utafika tu kuna mambo ya kujisafisha si hilo la Arusha.
Wanajamii wenzangu nimefuatlia ktk vituo vitatu tofaut,ITV,TBC1 na CH10 na kugundua kuwa serikal imeandaa kipind hik maalum kwa ajil ya kulisafisha jesh la polis na kukichafua CDM,make mtangazaj ana sistza kuwa yote yalotokea lawama kw CDM,shame upon their faces.
 
chadema sio chama cha kisiasa ni chama cha fujo

Sema CCM ni Chama Cha Majambazi, wanutuibia kupitia mikataba ya kinyonyaji, "DOOR WAZI", Richard wa Monduli, IPTL, RITES, NETGROUP Soln, Kagoda, Deep Greed, Meremeta, MOVE & PICK (Movenpic), Makampuni ya madini, aah mengi hayaishi!

Ile documentary ya polisi ni upuuzi mtupu, kwanini waliwakamata viongozi wa CHADEMA kwenye maandamano? Wange waacha wakaendelea na maandamano yao kisha wawatafute baadaye wakawahoji!

Polisi wasifikiri wamewaogopesha watu wa Arusha, sana sana wanawakomaza na kuwafanya sugu!
 
Nashukuru kwa kutujulisha kilichojiri. Kumbukeni hata kipindi cha uchaguzi hiyo Idara ya Habari sijui Uchafuzi ilitumika kuwadanganya watu kwamba serikali imefanya mambo mengi lakini watu hawakuelewa kitu waliwachagua CHADEMA.

Mara nyingi ukijitetea sana mtu atajiuliza kwa nini unatumia nguvu nyingi kijitetea? unaficha mambo.

Note: Kesi iko mahakamani wao wanatoa documentary je hawaingii uhuru wa mahakama?
 
Ndio wanawasha moto wa mabadiliko mana wengi wanapiga simu nakudai sehemu askari anavunja vioo vya gari ionyeshwe.
 
Naona wanasafisha Njia Ili Mkulu ( JK ) Apite/atoe Kauli ha ha ha
 
Nimeangalia, pamoja na kuficha mengine, bado wanachi wanatakiwa kutii vyombo vya dola, iwe dola ya ccm au chadema au cuf au ppt. kumbuka wao wanaenda na wamelelewa kufanya kazi kwa amri, na ukizingatia mawe yalirushwa kuwashambulia police, hata hasira za kawaida zingemfanya mwanadamu huyu aliyevaa kombati apige! ndio
 
Hivi hawa Polisi na hiyo documentary wanataka tuelewe na kuamimi nini? JK NA SEREKALI YAKE NI IMEKAMILIKA NA ISILAUMIWE? Jk na serekali yake ni adilifu? CCM NA KIKWETE WALIKUWA WAPI HADI HALI IKAFIKIA PALE?
Kweli CCM NA SEREKALI WAMEIONGOZA NCHI KWA NAMNA YA KUEPUSHA MAUAJI YA ARUSHA? No wasilete utani!
Watu 3 waliokufa wangetanguliwa na vifo vya Mafisadi wa 3. Ninge muunga JK MKONO!
Tuongelee the real source! Sio kutuwekea vi docmentary vya kipuuzi hapa!
POLISI WAKAPAMBANE NA MAGAIDI MAFISADI WA DOWANS, EPA NK CHADEMA HAWATAHITAJI MAANADAMANO!
 
Jeshi la polisi lisijidanganye kwamba linaweza kujisafisha lenyewe kwa hizo Propoganda zao.Tangu lini Hakimu akajihukumu kwenye kesi yake mwenyewe(Conflict of Interest).Njia Pekee ya kutatua hili swala ni kuundwa kwa Tume huru yakimahakama kufanya uchunguzi wa hili swala na wale wote watakaobainika kuhusika kuua na kujeruhi Mkondo wa Sheria uwaadhibu na kwakufanya ivyo Wananchi Watarudisha Imani ktk Jeshi la Polisi ila Kuingiza Propaganda kwenye swala lililogharimu maisha ya Watu na wengine kusababishiwa Ulemavu wa Maisha hakutawasaidia.
 
Jeshi la polisi kujisafisha kwa Arusha haiwezekani labda kwa Pwani. Si ndio jeshi hili hili liliuwa vijana wawili (Mtui na mwenzake) pale Kijenge Arusha vipi akina Sabinus Chigumbi wale wafanyabiashara wa madini na dereva taxi...... Hata wajaribu kujisafisha kwa satellite haitawezekani mikono yao imejaa damu zisizo na hatia.
 
It took almost 8 days to release that movie!!! wangekuwa wakweli siku ile ile au baada ya siku moja wangeonesha hiyo documentary kuthibitisha walichofanya.. Lakini siku nane na kwa picha za kuunga na zingine zikiwa ni wakati wa mazishi ya waliouwawa!!! Ni yale yale ya World Economic forum ya miti inayotakiwa kuota kwa miaka zaidi ya mitatu ikaota kwa siku mbili..!!!!
 
Tanzania kweli kuna mambo. Tunajua polisi wamemaliza kazi yao Arusha kwa kufuata maagizo ya viongozi wao. wananchi waliambulia kupigwa mabomu ya machozi, kupigwa risasi za moto na kupoteza mali na roho za ndugu zao.

Kinachowafanya sasa waanze kujitetea ni nini? wanajitetea dhidi ya nani? kama wanajitetea dhidi ya raia wanafanya makosa makubwa wala utetezi wao hauwezi kukubalika kamwe kwa sababu haki haitendeki hata sasa. utetezi wao hauwezi kukubalika kwa sababu upande wa pili katika sakata hilo haujapewa nafasi ambayo wao wamejipa. Pamoja na hilo bado utetezi wao haujibu maswali ya msingi kama: kwanini walikuwa wakivamia magari na kuvunja vioo vya magari? nani ataamini kama waliokuwa katika magari walikuwa wanaandamana? Raia wa Kenya aliyeuawa alikuwa akiandamana kweli?
 
Nimeangalia, pamoja na kuficha mengine, bado wanachi wanatakiwa kutii vyombo vya dola, iwe dola ya ccm au chadema au cuf au ppt. kumbuka wao wanaenda na wamelelewa kufanya kazi kwa amri, na ukizingatia mawe yalirushwa kuwashambulia police, hata hasira za kawaida zingemfanya mwanadamu huyu aliyevaa kombati apige! ndio


Jielimishe kwanza ndio utajua kuwa hata uraiani si kila mtu anaweza kumilikishwa siraha ya moto. Siraha ina maadili yake hakuna excuse za kitoto kama kusema hasira ndio ilipelekea askari kutumia excessive force ili kuua na si kuwatawanya!
 
Kuwa na akili wewe. WHO IS THE SOURCE OF THE PROBLEM, yule aliyeanza kupiga watu mabomu au yule aliyekataa kuonewa kupigwa mabomu. CCM ina take advantage kwamba watanzania wengi bado wanauelewa mdogo, hivyo kupotosha habari kwao si big issue.


The source is a bunch of opportunistic armature politicians who incited their followers to disobey a lawful order.
Their evil agenda is to gain political and financial mileage by exploiting disadvantaged youth.
That goal must be achieved by all means even by killing innocent people.

I hope now you know!
 
Habari maelezo wanachojaribu kutuambia ni kuwa yale tuliyoyaona kwenye" movie"yao ndo yaliyohalalisha polisi kupiga watu risasi za moto na wliosababisha ni CHADEMA.Mimi nachojiuliza tu kati ya CDM na polisi ni nani aliyemuua mwenzake,nani aliyeanza kupiga mabomu?hivi mara ngapi watu wanakwenda kuwatoa watu polisi hivi ni lazima wafanye fujo okey CDM ndo wakorofi sawa hata tukikubali hii ndo inahalalisha wao kututwanga risasi hovyo na la Mbeya andaeni movie nyingine muiite "LAKUVUNDA HALINA UBANI"halafu mtafute chama cha siasa kimoja mkilaumu.
 
The source is a bunch of opportunistic armature politicians who incited their followers to disobey a lawful order.
Their evil agenda is to gain political and financial mileage by exploiting disadvantaged youth.
That goal must be achieved by all means even by killing innocent people.

I hope now you know!

propagandist.

kwa mara nyingine tena mumenoki!!!
 
The source is a bunch of opportunistic armature politicians who incited their followers to disobey a lawful order.
Their evil agenda is to gain political and financial mileage by exploiting disadvantaged youth.
That goal must be achieved by all means even by killing innocent people.

I hope now you know!

Tuambie waliouawa walikuwa maeneo gani na walikuwa wanafanya nini? mbona hakuna anayezungumzia kifo cha raia wa Kenya, je naye alikuwa anaandamana? tumesikia mara ngapi kuwa raia wasio na hatia huuliwa na polisi na mwisho wa siku polisi wapo salama? hukumbuki wale wafanya biashara wa Dar na dereva taksi? Tumesikia Mbeya kwamba watu wameuawa vile vile. Ni lini mtatuambia kuwa polisi walikuwa na makosa? sasa hvi wameanza kujitetea wao kwa sababu kwa gharama za raia hao hao waliowaonea
 
Back
Top Bottom