TBC watangaza rasmi kuonesha Bunge live

TBC watangaza rasmi kuonesha Bunge live

mcfm40

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2010
Posts
4,452
Reaction score
3,152
Ni kupitia TBC2. Wanadai wataonesha saa 3 asubuhi saa sita mchana, saa kumi na moja jioni na saa 4 usiku (recorded). Chanzo TBC

Naona hatimaye wamebana wee wameachia. Ila nina maswali kadhaa:

Je, TV binafsi zitaruhusiwa kurusha pia?
Je Je huo muda TBC wanarusha live watu watakuwa hawafanyi kazi? Kwa sababu walisema mwanzo lengo la kuzuia ni ili watu wafanye kazi!

Je, kwa nini wameamus kulificha bunge kwenye channel ya kulipia, yaani TBC2? Je kuangalia bunge likijadili mambo yetu wananchi ni luxury?

Je wale wasioweza kulipia hiyo channel hawana haki ya kuwasikia wawakilishi wao wakizungumzia matatizo yao bungeni?

Nina maswali mengi,
Hata hivyo niwapongeze wahusika kwa kukubali kwambs hapa walichemka! Naamini huu utakuwa mwanzo wa kuturudishia wananchi haki yetu ya kufuatilia kikamilifu yanayofanywa na wawakilishi wetu!
 
Wanaficha nini ? Na wanaogopa nini? Watanzania wan vitu vyao wanavyoangalia kama serikali hii ita navyo hakuna haja kuficha bunge! Serikali iliyopita ndio iliharibu kila kitu kwenye rushwa na ufisadi! Sasa wanaogopa nini?
 
Wengine tulijua na tukasema mapema kuwa wameshajua wamechemsha na watajirudi tu sasa yametimia.

Huu ni mwanzo ila baada ya muda watarudisha matangazo hayo TBC1.Ni rahisi zaidi kuanzia TBC 2 kwanza alafu baadae warudishe TBC 1.Ni mkakati tu huo baada ya kugundua makosa yao.
 
ni ajabu sana mambo tunayojadili kama wananchi hayana impact yoyote kwa manifaa ya maendeleo ya mtu mmoja mmoja.
 
ni ajabu sana mambo tunayojadili kama wananchi hayana impact yoyote kwa manifaa ya maendeleo ya mtu mmoja mmoja.

Kama kisheria ni haki ya kuona Bunge basi haijalishi Nina pata hasira au faida ila kwa sababu ni haki yangu basi shurti nilione tuache siasa
 
Watu wengi vijijini hata mijini hawana access na Tbc2 maana kwenye ving'amuzi vingi (hapa niko tayari kukosolewa)hii Chanel iko kwenye parkage za kulipia wakati TBC iko free everywhere.Jiulize kwanini hawaonyeshi kupitia TBC 1?
 
Umesahau ya kua tuko katika ulimwengu wa digital hata hiyo TBC1lazima ulipie.
 
Shida unapokuwa Wabunge wanaokwenda kujipendekeza kwa serkali badala ya kuisimamia.Ndugai na wenzake historia itawahukumu kwa kutudisha karne ya kumi na nane.Wameligeuza bunge kuwa taasisi butu kabisa.Na wabunge wa CCM wametumbukia kwenye mtego.Kwa mfano hawa wa viti maalum toka CCM wanasikitisha kabisa kuna haja ya kubadilisha mfumo wa jinsi wanavyopatikana,Kwa kweli wanatia aibu kabisa mhimili wa bunge.
 
Wanaficha nini ? Na wanaogopa nini? Watanzania wan vitu vyao wanavyoangalia kama serikali hii ita navyo hakuna haja kuficha bunge! Serikali iliyopita ndio iliharibu kila kitu kwenye rushwa na ufisadi! Sasa wanaogopa nini?
Hao wote ni wa serikali iliyopita. Yaani ni copy edit and paste
 
TBC 2 ni kituo cha kulipia !
bado tatizo liko pale pale !
Hapo mwenye uwezo kama Mimi tutafaidi
Je masikini wa local wataona je ??
Hapa mbwembwebtu kazi 2020
 
Tunataka bunge live kupitia star tv, itv na Azam au radio full time tume miss kweli kweli Kwa kweli wakati wa awamu ya nne tulifaidhi sana.
 
Back
Top Bottom