TBC hawaishi kuchemka

TBC hawaishi kuchemka

Rais wa kwanza wa kuchaguliwa kidemokrasia nchini Afrika kusini ni Hayati Nelson Mandela.

Unapoanza kuongelea habari ya Rais wa kwanza kuchaguliwa Kidemokrasia ni slippery slope.

Nyerere, kwa mfano, alikuwa peke yake kwenye ballot box miaka yote, alifuta vyama vingi.

George Washington alipochaguliwa Rais wanawake wa Marekani walikuwa hawapigi kura. Walipoanza wanawake, weusi wakawa bado hawapigi kura.

Kwa hiyo kwa ujumla huwa tunaacha mambo ya kusema Rais wa Kwanza wa demokrasia ili kuepuka ubishabi. Kwa sababu hata hapa hapa Tanzania hatujui kwa uhakika Rais wa kwanza wa Kidemokrasia ni nani. Kama yupo.

Lakini Rais wa kwanza ni nani hatubishani.
 
ukumbuke mjane grace machel alikuwa wa mandela
Graca Machel ni Mjane. Amebahatika kuolewa na SAMORA Machel (Rais wa kwanza wa Msumbiji) na Nelson Rolihlahla Mandela (Mwafrika wa Kwanza kuwa Rais wa Afrika ya Kusini).
 
Mnanichanganya tu. Wengine wanaongelea raisi wa kwanza wa A.kusini, wengine wanaongelea mke wa kwanza wa Mandela. Mada hasa ni ipi?

Unauliza mada ni ipi kati Mke wa Kwanza na Rais wa Kwanza? Tuwaulize TBC!
 
TBC wanasoma taarifa ya habari ya saa moja asubuhi, sasa hivi.

Nimesikia wakimtaja mgeni aliyeko nchini kwa sasa:

MKE WA RAIS WA KWANZA WA AFRIKA KUSINI GRACA MACHEL

Jamani hawa watu wanahitaji msaada wa dharura, hawana ma editors.

Rais wa kwanza wa Afrika Kusini ndio nani?
Kwani hujui grece machel alikuwa mke wa mandela baana ya kuachana na win mandela.
 
Mandela ni raisi wa kwanza mweusi ila South afrika ina maraisi wengi tu Mandela sio wakwanza
 
Ni nchi gani ya Afrika iliyokuwa na Rais wakati ikitawaliwa???

Nchi ya Afrika Kusini ilipata uhuru mwaka gani???
wazungu makaburu wa apartheid hawakuwa wakoloni walikuwa ni raia weupe wa sa na waliishi na kujenga sauzi kama kwao na walikuwana marais na historia ya nchi yao
 
This wa kwanza south Africa anaitwa Charles Robert's 1960-1961.alifariki 1982.baadae kina Botha walifuata kabla ya Mandela
 
Unapoanza kuongelea habari ya Rais wa kwanza kuchaguliwa Kidemokrasia ni slippery slope.

Nyerere, kwa mfano, alikuwa peke yake kwenye ballot box miaka yote, alifuta vyama vingi.

George Washington alipochaguliwa Rais wanawake wa Marekani walikuwa hawapigi kura. Walipoanza wanawake, weusi wakawa bado hawapigi kura.

Kwa hiyo kwa ujumla huwa tunaacha mambo ya kusema Rais wa Kwanza wa demokrasia ili kuepuka ubishabi. Kwa sababu hata hapa hapa Tanzania hatujui kwa uhakika Rais wa kwanza wa Kidemokrasia ni nani. Kama yupo.

Lakini Rais wa kwanza ni nani hatubishani.
Rais wa kwanza Charles Roberts
 
First black president of South Africa Nelson Mandela... TBC ludini shule
 
TBC wanasoma taarifa ya habari ya saa moja asubuhi, sasa hivi.

Nimesikia wakimtaja mgeni aliyeko nchini kwa sasa:

MKE WA RAIS WA KWANZA WA AFRIKA KUSINI GRACA MACHEL

Jamani hawa watu wanahitaji msaada wa dharura, hawana ma editors.

Rais wa kwanza wa Afrika Kusini ndio nani?
Mi wasiwasi wangu ni kwako wewe uliyeitazana tbc badala ya kuiangalia tu.
 
Hapana, Winnie alikuja baadae.

Mkewe wa kwanza ni Evelyn Mase.

Mandela_e_Evelyn_1944.jpg


Kwa hiyo hata kama walikuwa wanaongelea mke wa kwanza wa Mandela, hakuwa Winnie wala Graca.

Nelson Mandela alikuwa ni reputed womaniser, kwa kiswahili muhuni. Julius Nyerere anatakiwa awe na nafasi ya taadhima kuliko Mandela in the pantheon of African history.

TBC hawawezi kujua mambo haya.
Kwani alikua dini gani?
 
Kwani alikua dini gani?


Ndio hapo sasa, hatujui hata ni dini gani huyu Mzee kutokana na jina la NELSON lakini kaoa mara kibao.

Well, even assuming Mandela ni Muislam ambae ni sawa kuoa mara nyingi, Mandela bado alikuwa na sifa ya kuwa off the chain philanderer , kiswahili fuska, ambae alikuwa analeta wasichana mpaka nyumbani kwa mkewe kama vile secretary wake Ruth na wengine wengi. Mkewe Evelyn akileta ubishi alikuwa anachapwa (alishamfungulia mashtaka Mandela kwa kumtandika.)

Zaidi ya Mama Maria, hakuna mwanamke duniani ambae amewahi kudai amelala kwenye kitanda cha Julius Nyerere. Na haikuwahi kusikika kamwe amemchapa Mama Maria.

Wazungu wanapotuandikia utukufu wa Nelson Mandela hawawezi kuona uchafu huu kama tatizo kwa sababu kwao sio uhuni. Marais wao wanafanya ngono Whitehouse! Mwalimu, kama tungekuwa tunajiandikia historia sisi wenyewe angekaa juu ya Mandela kwa misingi ya taadhima, uongofu na mapambano ya Mwafrika.

Source:
www.dailymail.co.uk/home/books/article-1288343/Womaniser-terrorist--portrait-young-Mandela-YOUNG-MANDELA-BY-DAVID-JAMES-SMITH.html
 
Back
Top Bottom