Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,478
- 39,998
Nimesikia mara kwa mara tena kwa lugha ya dharau ya aina fulani kuwa "Watanzania hawaju" na kuwa "Huko kijijini watu hawaelewi" na wengine wamefikia mahali pa kudai kuwa "wananchi hawana elimu ya kutosha ya uraia" na kuwa vitu hivyo ndivyo vinavyosababisha CCM ishinde.
Nimejiuliza swali moja: Mwaka 1995 (Nyerere akiwa bado hai) kwanini kulikuwa na mwamko mkubwa wa upinzani kuliko 2000, 2005 hasa tukiangalia matokeo ya Urais? Hili ukizingatia kuwa matumizi ya cellphones hayakuwepo, internet ndiyo kabisa, na vyombo vya habari bado vichache?
Hivi kweli tukilinganisha kuwa wananchi wa 1995 hawakuwa na uelewa wanachokitaka zaidi kulinganisha na hawa wa "digital age"?
Nakataa tatizo haliko katika uelewa wa Watanzania.. na tutadagangana tukifiria ati tukitoa elimu zaidi, matangazo ya kwenye TV kuhusu "usia wa Nyerere" n.k utawafanya watu waamke zaidi. Ni makosa kudhania kuwa elimu zaidi ya uraia itawafanya watu wachague upinzani na kuwa kueleza zaidi mabaya ya CCM kutawafanya waichukie.
Labda hatuangalii vitu kwa usahihi?
Mkuu Mwanakijiji, naona kwenye hii hoja yako dhana ya elimu umeipatia maana nyembamba sana.
Mfano uliotumia wa Mrema/ Upinzani mwaka 1995 hautoshelezi kujenga hoja kuwa wananchi wana elimu ya kutosha ya uraia au hawana. Pengine, mfano huo huo unaweza kuwa kigezo tosha kujenga hoja kuwa Watanzania ni malimbukeni inapokuja kwenye kupiga kura. Mwaka 1995 kura alipigiwa Mrema na siyo upinzani (kwa maana ya Sera zao). Iwapo kama Watanzania wangekuwa wamepigia kura kwa sababu ya Sera wanazo zikubali za Upinzani ni dhahiri kuwa mpaka leo Upinzania ungekuwa na nguvu sababu sera zao hazijabadilika sana. Tena zaidi kwa sababu CCM wamejiwekea madoa kutokutimiza baadhi ya sera zao.
Leo hii Kwa kiwango kikubwa sana CCM inapigiwa kura kwa sababu ni CCM ( the brand) na uwepo wao karibu na Wananchi (nyumba kumi, Serikali za Mtaa n.k). Huenda utakubaliana na mimi kuwa yakifanyika majaribia ya kuondoa viongozi wote kutoka CCM na kuwahamishia Chadema na wale wa Chadema kuwaleta CCM (wa hame na sera zao au sera za Chadema ziwe CCM na vice versa)...ukifanyika uchaguzi CCM yenye wakina Mbowe na Dr Slaa itashinda bila ubishi.!!
Sasa kama tatizo sio Elimu (kwa mapana yake) basi nitakuwa wa kwanza kukubali sijui maana ya Elimu.
Nimesikia mara kwa mara tena kwa lugha ya dharau ya aina fulani kuwa "Watanzania hawaju" na kuwa "Huko kijijini watu hawaelewi" na wengine wamefikia mahali pa kudai kuwa "wananchi hawana elimu ya kutosha ya uraia" na kuwa vitu hivyo ndivyo vinavyosababisha CCM ishinde.
Nimejiuliza swali moja: Mwaka 1995 (Nyerere akiwa bado hai) kwanini kulikuwa na mwamko mkubwa wa upinzani kuliko 2000, 2005 hasa tukiangalia matokeo ya Urais? Hili ukizingatia kuwa matumizi ya cellphones hayakuwepo, internet ndiyo kabisa, na vyombo vya habari bado vichache?
Hivi kweli tukilinganisha kuwa wananchi wa 1995 hawakuwa na uelewa wanachokitaka zaidi kulinganisha na hawa wa "digital age"?
Nakataa tatizo haliko katika uelewa wa Watanzania.. na tutadagangana tukifiria ati tukitoa elimu zaidi, matangazo ya kwenye TV kuhusu "usia wa Nyerere" n.k utawafanya watu waamke zaidi. Ni makosa kudhania kuwa elimu zaidi ya uraia itawafanya watu wachague upinzani na kuwa kueleza zaidi mabaya ya CCM kutawafanya waichukie.
Labda hatuangalii vitu kwa usahihi?
Nimesikia mara kwa mara tena kwa lugha ya dharau ya aina fulani kuwa "Watanzania hawaju" na kuwa "Huko kijijini watu hawaelewi" na wengine wamefikia mahali pa kudai kuwa "wananchi hawana elimu ya kutosha ya uraia" na kuwa vitu hivyo ndivyo vinavyosababisha CCM ishinde.
Nimejiuliza swali moja: Mwaka 1995 (Nyerere akiwa bado hai) kwanini kulikuwa na mwamko mkubwa wa upinzani kuliko 2000, 2005 hasa tukiangalia matokeo ya Urais? Hili ukizingatia kuwa matumizi ya cellphones hayakuwepo, internet ndiyo kabisa, na vyombo vya habari bado vichache?
Hivi kweli tukilinganisha kuwa wananchi wa 1995 hawakuwa na uelewa wanachokitaka zaidi kulinganisha na hawa wa "digital age"?
Nakataa tatizo haliko katika uelewa wa Watanzania.. na tutadagangana tukifiria ati tukitoa elimu zaidi, matangazo ya kwenye TV kuhusu "usia wa Nyerere" n.k utawafanya watu waamke zaidi. Ni makosa kudhania kuwa elimu zaidi ya uraia itawafanya watu wachague upinzani na kuwa kueleza zaidi mabaya ya CCM kutawafanya waichukie.
Labda hatuangalii vitu kwa usahihi?
"Watanzania hawaju" na kuwa "Huko kijijini watu hawaelewi" na "wananchi hawana elimu ya kutosha ya uraia" na kuwa vitu hivyo ndivyo vinavyosababisha CCM ishinde.
Labda hatuangalii vitu kwa usahihi?
Mkjj, kwanza kabisa ahsante kwa hoja.
Pili, naona hili swala la 'mwamko vs elimu' ni gumu kulielezea hata kwako (mmoja wa wachache wenye upeo na udadisi mpana zaidi na hali ya kisiasa hapa Tz kuliko tuliowengi). Kwa maelezo machache uliyojaribu kutoa hapo juu, kuna maswala yaonekana kujikanganya moja juu la jingine. Kwa maoni yangu kuhusu huu mkanganyiko, ni dhahiri kwamba kuna kitu hakipo. Kitu hicho nadhania ni research ya hili swala kwa undani zaidi. Kwani pale unapotaja kutokuwepo kwa mapungufu ya elimu, au hiyo elimu ya uraia, na wakati huohuo kutaja kwamba mwamko wa wananchi katika ku-support upinzani ulikuwa mkubwa zaidi huko nyuma sembuse na sasa hivi kwenye digital age; hapo panakuwa na mambo yaliyojichanganya. Na katika kujaribu kuchanganua na kupata majibu, inabidi kujiuliza baadhi ya maswali:
-- Je, hapo awali mwamko huo unaousema wa wananchi kujua wanachokitaka ulisababishwa na nini? Elimu yao kiujumla, au elimu ya uraia?
-- Je, elimu ya uraia inapatikana vipi hivi sasa kulinganisha na hapo awali?
-- Je, influence ya Mwl. Nyerere ilitawala kwa kiwango gani katika swala zima kulinganisha na sasa? Bado ipo au ilishajifia?
-- Je, mwananchi mwenye elimu kutoka kwenye mitaala yetu tuliyoizoea anatofauti gani na yule mwenye elimu ya uraia pekee?
-- Je, kwa wenzetu wanaochagua upinzani, au wale wanao badilisha serikali zao mara kwa mara zinapovurunda kupitia demokrasia ya uchaguzi wanafanikisha hilo kutokana na yapi?!
-- Je, elimu ya uraia na kuwepo kwa upinzani mkubwa kivyama kunaendana na tabia za watu (jamii) wa pahala fulani?!
-- Je, swala la elimu kiujumla (ya mitaala na uraia) linachangamana vipi na swala la mwamko wa kisiasa?! Yanaendana, ni lilelile, au hayafungamani?
Maswali ni mengi, na kwa kweli kama nilivyodokezea hapo awali, hili linapelekea kuwepo kwa kila aina ya research kwenye nyanja hii, haswa pale zinapoonekana kutokuwepo kabisa kwenye jamii yetu tangu mfumo wa vyama vingi ufurumke!
Mkjj, nimetumia neno 'ufurumke' hapo juu makusudi, kwani namna jinsi vyama vya upinzani viliposhika hatamu awali ilikuwa kwa mfurumko. Kuna jambo ambalo nimeshaongelea nawe mara nyingi, naro ni swala la wananchi kuwa na uwezo wa kung'amua ubaya na uzuri wa viongozi walionao sasa hivi na hapohapo kujua kuwa wana nguvu kubwa ya kidemokrasia ya kumng'oa kiongozi yeyote yule waliomchagua wao pale wanapoona amekejeli matakwa yao na kutotimiza ahadi zake. Sasa kama hili ni swala la elimu kiujumla, kama hili ni swala la elimu ya uraia, au kama hili ni swala la mwamko wa kisiasa pekee; hapa ndipo penye kuhitaji majibu kwa maoni yangu.
Katika kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi kisiasa, natamani sana kama Mwl. Nyerere kutokana na influence yake alipokuwa hai na akiwa bado ndani ya CCM angeli-endorse kuvunjwa-vunjwa kwa CCM na kukifanya kiwe vyama viwili vinavyotofautiana katika baadhi ya mambo, au kuivunja kabisa na kuiweka kibindoni kwa muda, nchi kuongozwa by an interim government, kisha kutangaza mchakato wa kuunda vyama vya kisiasa, vile vyenye mrengo wa kushoto, kulia na vile vya mrengo wa kati. Well, hii ni ndoto iliyochelewa, CCM ilishabarikiwa kuwa na nguvu and I think Mwl. Nyerere must have known the foreseeable problem but chose to ignore it. Naongelea tamanio hili kuwepo wakati wa mwanzo wakati wa Nyerere, kwani CCM imekuwa na disproportional advantage over other parties. Wakati vyama vingine vinaanzishwa, CCM ilikuwa na financial backup ya kutosha, vitega uchumi kama viwanja vya michezo na majengo vilikuwa na bado viko mikononi mwake. Kujulikana na kuwa favourite party kulikuwa na bado kunaendelea kuwa. Hivyo platform nzima ya kuwepo kwa vyama vingi haikuwa stable na hiyo hilo kwa maoni yangu laweza kuwa jambo moja ambalo limezorotesha upinzani kwa mapana.
Swala la kuaminika kwa Nyerere na influence yake katika society ni moja ya jambo muhimu kwenye hii equation ya elimu ya uraia-vs-mwamko wa kisiasa. Mwamko ulipo sasa hivi unaweza kuwa umezorota kulinganisha na wakati ule wa mwanzo kutokana na ukweli kwamba wananchi wengi walimwamini sana Mwl. na bado wengi wanaendelea kuamini mambo yake mengi (wengine hata kuamini bado yu hai!), hata sisi hapa mtandaoni wengi wetu tunamkubali kuwa he was a patriotic person na tunaenzi mengi aliyotuachia. Lakini katika kuenzi haya mengi aliyotuachia, tunasahau mojawapo ya aliyotuachia ni CCM. Personally, I wish he quitted from CCM na kukifanya kisimame dede chenyewe (not forgetting that kilisha simama tayari) just for the sake of trying to put all parties on an equal footing. Kwani kutofanya hivyo ameicha CCM na ameacha legacy kwamba CCM ni chama cha Nyerere na kilichoikomboa Tanzania. Kwenye jamii ya watu ambao elimu ya msingi ni darasa la saba na vyanzo vya habari kijamii kwa ukubwa viko controlled na CCM, bila shaka wanajamii wengi watakuwa ni wanaCCM. That plus the current voracious propaganda machinery iliyopo ndani ya CCM isiyo na lengo la kuendeleza upinzani (kama moja ya nguvu ya kuleta mabadiliko chanya Tz) kama jinsi vile mwasisi Nyerere angelipenda iwe bali kuuua kabisa kabisa; hapo wananchi wanakuwa na only one option, nayo ni CCM. Maana through media wanakuwa wametishiwa kuhusu upinzani na kulaghaiwa vya kutosha.
Swala la elimu ya uraia-vs-mwamko wa kisiasa linaweza pia kuchanganuliwa kwa kuangaliwa kwa kuweka jicho la kengeza kwa wenzetu waliofanikiwa katika haya. Jicho la kengeza maana jamii zinatofautiana, Watanzania siyo Wakenya, siyo Wahispania, siyo Waingereza na siyo Wazimbabwe wala Waamerika. Inabidi kuangalia pahala tu pale system zinapo-cross link. Katika mfumo wetu wa vyama vingi, ni wapi jamii yetu inafanana na hizo nyingine, kielimu za mitaala, elimu ya uraia au basi hili swala zima tunalolipatia jina la 'mwamko wa kisiasa'. Je, wamefanikisha vipi hayo yote kwenye ulimwengu huu wa utandawazi hali hapa kwetu upinzani ukififia?!
Ngoja niishie hapa, ila kama nilivyosema Mkjj, hili swala tunaweza kulikimbia kuwa siyo tatizo la elimu, au basi kusema kwamba ni tatizo la elimu ya uraia; lakini ukweli unabakia palepale, tatizo lipo na tatizo hili la wananchi kutokuwa na nia au uwezo wa kung'amua viongozi bora ni wapi na wale wanaovurunda ni wapi kisha kuwabadilisha chaguzi zinapotokea limetapakaa nchini mwetu. Ni tatizo sugu na nitatizo linalozidi kuturudisha nyuma kama Taifa. Laiti tu wananchi wa Tanzania wangeliweza kutambua wana nguvu kubwa sana kama raia wa Taifa hili (isiyo hitaji elimu wala mwamko wa kisiasa) ya kuweza kubadilisha viongozi wabovu, nchi yetu ingelishapiga hatua kubwa. Tatizo, chama kilichopo madarakani, CCM yaonekana kabisa haitaki wananchi watambue nguvu hii.
Ahsante.
Steve Dii
Nimesikia mara kwa mara tena kwa lugha ya dharau ya aina fulani kuwa "Watanzania hawaju" na kuwa "Huko kijijini watu hawaelewi" na wengine wamefikia mahali pa kudai kuwa "wananchi hawana elimu ya kutosha ya uraia" na kuwa vitu hivyo ndivyo vinavyosababisha CCM ishinde.
Nimejiuliza swali moja: Mwaka 1995 (Nyerere akiwa bado hai) kwanini kulikuwa na mwamko mkubwa wa upinzani kuliko 2000, 2005 hasa tukiangalia matokeo ya Urais? Hili ukizingatia kuwa matumizi ya cellphones hayakuwepo, internet ndiyo kabisa, na vyombo vya habari bado vichache?
Hivi kweli tukilinganisha kuwa wananchi wa 1995 hawakuwa na uelewa wanachokitaka zaidi kulinganisha na hawa wa "digital age"?
Nakataa tatizo haliko katika uelewa wa Watanzania.. na tutadagangana tukifiria ati tukitoa elimu zaidi, matangazo ya kwenye TV kuhusu "usia wa Nyerere" n.k utawafanya watu waamke zaidi. Ni makosa kudhania kuwa elimu zaidi ya uraia itawafanya watu wachague upinzani na kuwa kueleza zaidi mabaya ya CCM kutawafanya waichukie.
Labda hatuangalii vitu kwa usahihi?
Wasomi sio tu wanatuangusha kwenye kupiga kura lakini pia kwenye kushirki kuomba nafasi za kuchaguliwa na kupigiwa kura. Mimi naamini wananchi wa vijijini ndio tulioathirka zaidi na sera za CCM, sisi ndio tunao tembea umbali mrefu kufuata kuni, maji, zahanati, shule, nk. sisi ndio kila siku tunatoa michango ya kujenga madarasa na vyoo vya shule pesa zinazoishia mikononi mwa wenyeviti wetu wa halmahsauri za wilaya, madiwani na watendaji wa wilaya na madarasa hayaishi miaka nenda rudi. Kwa ujumla tumechoshwa na tunataka sana mageuzi na kuweka watu wapya kutoka vyama mbadala, lakini wapi tunashindwa??? Kwanini hatuwezi??
Tunashindwa kutekeleza dhamira yetu hiyo kwasababu Vyama vya upizani na wasomi wanatuangusha. Vyama vaya upinzani Wanateua wagombea wazuri na wenye sifa nzuri kugombea mijini na sio vijijini, majimbo ya vijijini ambayo wapinzani waliweka wagombea wazuri kama akina Slaa, akina Zitto, Ndesamburo, wapinzani walishinda, lakini majimbo ya sisi wengine wanaweka mtu hawezi hata kueleza chama chake kinaamini nini??
Nitawapa mfano wa jimbo langu la Makete:
Mwaka 1995 jimbo la Makete lilikuwa na wagombea wawili wa ubunge Aliyekuwa anatetea nafasi hiyo Mh. Tuntemeke Sanga akipambana na msomi wa Form six mwenye diploma ya uhasibu(UDP), sasa utaona mwenyewe nchi nzima ilikuwa inamfahamu Bw. Tuntemeke kwa Makeke, ubishi, uwezo wa kujenga hoja na msimamo thabiti, achilia mbali shule yake ya degree 5, unadhani wananchi wa Makete wangeweza kuweka rehani jimbo lao kwa kijana wetu wa form six ambaye hana uzoefu kwenye medani za kisiasa?
Mwaka 1997 Mh. Tuntemeke alifariki ukaitishwa uchaguzi mdogo. CCM walimteua Dr. Hassy Kitine (PhD) wakati huku upinzani ukimteua mgombea wao kwa ticket ya NCCR- Mageuzi (Form IV hana hata cheti cha kozi) Wote mnamfahamu Kitine kuwa alikuwa ni Mkurugenzi wa usalama wa Taifa, na mkuu wa mkoa wa Tanga, na baadaye waziri unadhani ingekuwa rahisi kwa huyo mpinzani kushinda kwa kungalia CV tu achilia mbali kutumia vijana wake wa UWT kufanya kile kinachowezekana kufanywa. Lakini pia Wananchi wa vijijini sio washamba kiasi hicho cha kulinganisha Form IV na PhD na kwenda kwa Form IV bila sababu za kueleweka.
Mwaka 200 yakarudiwa yale yale Kitine akashinda tena
Mwaka 2005. CCM walimteua Registrar wa DIT Dr. Binilith Mahenge (PhD) Upinzania ukamsimamisha mgombea kupitia CHADEMA safari hii tena kijana wa Form IV, pamoja na uwiano mbaya wa uzoefu na elimu wa wapinzani na wagombea wa CCM bado unakuta hawa wagombea wa Upinzani wanapata kura za kutosha kitu amabacho naamini kama wananchi wa kijijini wangeletewa wagombea wazuri kutoka upinzani wangewachagua tu. Baada ya uchaguzi huyu kijana akarudisha kadi ya CHADEMA akapewa utendaji wa kata, sasa hivi anafisadi nchi kwa kwenda mbele, mbolea za ruzuku, ndio fringe benefit zake.
Wasomi sio tu washiriki kwenye modahalo na kupiga kura naamini kama watashiriki kugombea na kutafuta nafasi za kuongoza kutoka huko vijijini watatusaidia sana watanzania. Bila kubadirisha namna wagombea wanavyokuwa allocated, Bunge litaendelea kutawaliwa na CCM
Mkuu upo sahihi kuwa kuwahukumu wagombea kwa elimu yao ya darasani sio sahihi, nakubalina na wewe, pia uko sahihi kuwa wagombea wenye Elimu ndogo wanaweza wakawa viongozi wazuri zaidi na watakaowajibika kwa wananchi NAKUBALIANA.lakini hufikiri kuwa judge wagombea kwa elimu ya darasani - hususan ukizingatia wananchi wetu wengi hawajapata elimu ya kutosha ya darasani- ni sawa?
Maana inawezekana form six akawa anawajibika vizuri kwa wananchi