Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,460
- 39,927
Nimesikia mara kwa mara tena kwa lugha ya dharau ya aina fulani kuwa "Watanzania hawaju" na kuwa "Huko kijijini watu hawaelewi" na wengine wamefikia mahali pa kudai kuwa "wananchi hawana elimu ya kutosha ya uraia" na kuwa vitu hivyo ndivyo vinavyosababisha CCM ishinde.
Nimejiuliza swali moja: Mwaka 1995 (Nyerere akiwa bado hai) kwanini kulikuwa na mwamko mkubwa wa upinzani kuliko 2000, 2005 hasa tukiangalia matokeo ya Urais? Hili ukizingatia kuwa matumizi ya cellphones hayakuwepo, internet ndiyo kabisa, na vyombo vya habari bado vichache?
Hivi kweli tukilinganisha kuwa wananchi wa 1995 hawakuwa na uelewa wanachokitaka zaidi kulinganisha na hawa wa "digital age"?
Nakataa tatizo haliko katika uelewa wa Watanzania.. na tutadagangana tukifiria ati tukitoa elimu zaidi, matangazo ya kwenye TV kuhusu "usia wa Nyerere" n.k utawafanya watu waamke zaidi. Ni makosa kudhania kuwa elimu zaidi ya uraia itawafanya watu wachague upinzani na kuwa kueleza zaidi mabaya ya CCM kutawafanya waichukie.
Labda hatuangalii vitu kwa usahihi?
Nimejiuliza swali moja: Mwaka 1995 (Nyerere akiwa bado hai) kwanini kulikuwa na mwamko mkubwa wa upinzani kuliko 2000, 2005 hasa tukiangalia matokeo ya Urais? Hili ukizingatia kuwa matumizi ya cellphones hayakuwepo, internet ndiyo kabisa, na vyombo vya habari bado vichache?
Hivi kweli tukilinganisha kuwa wananchi wa 1995 hawakuwa na uelewa wanachokitaka zaidi kulinganisha na hawa wa "digital age"?
Nakataa tatizo haliko katika uelewa wa Watanzania.. na tutadagangana tukifiria ati tukitoa elimu zaidi, matangazo ya kwenye TV kuhusu "usia wa Nyerere" n.k utawafanya watu waamke zaidi. Ni makosa kudhania kuwa elimu zaidi ya uraia itawafanya watu wachague upinzani na kuwa kueleza zaidi mabaya ya CCM kutawafanya waichukie.
Labda hatuangalii vitu kwa usahihi?