Ralph Tyler
JF-Expert Member
- Jul 31, 2015
- 2,827
- 3,569
kama mtu ana uhakika wa anachosema na anayo dhamira njema kwa mujibu wa imani yake, anaogopa nini kukisema?Anasema watu waseme kweli, je anamaanisha hilo? Ni vyema ukaijua tabia ya mtu. Huwa inasemwa tazama matendo na sio maneno. Mfano mrahisi ni jana, kuna mjumbe toka kanda ya kusini, alitoa malalamiko ya kuwa wapinzani wanatoka huko upinzani na kupewa nafasi. Majibu aliyopewa yalikuwa ni kebehi zaidi kuliko ilivyopaswa. Inaonekana unatetea jambo ambalo hujalifanyia utafiti.
Yote kwa yote ujumbe wa Ponda umefika, hata akichukuliwa hatua ni kwa mapungufu machache ya waraka wake, lakini ndani vya huo waraka kuna ukweli wa zaidi ya 80%. Na uzuri ukweli huwa unajitetea wenyewe. Ni watu wachache sana huwezi kusimamia hadharani ukweli ulio kinyume na watawala. Na hii ni toka zama za manabii.
Kama malalamiko haya ya waislamu ni ya kweli, kwanini Mufti hayasemi mbele ya Rais na hata hadharani?
Nakumbuka enzi za Mufti akiitwa Hemed bin Jumaa bin Hemed, kuna kijana wa kiislamu alikamatwa na kushitakiwa kwa kosa la kusema 'Yesu siyo Mungu', Mufti alitoka hadharani na kusema kuwa waislamu wote ndivyo wanavyoamini kuwa Yesu siyo Mungu, kwahiyo kumshikilia kijana huyo ni kama kumdhulumu haki yake ya kukiri anachoamini. Kama nakumbuka vizuri kijana yule alishinda rufaa yake, na ushindi wake kwa mtazamo wangu hauthibitishi kuwa Yesu siyo Mungu bali unathibitisha uhuru wa mtanzania kuamini dini anayoitaka ilimradi hajavunja sheria.
Vivyohivyo kwa yanayolalamikiwa, kwanini Mufti asiyawakilishe serikalini aseme wazi kuwa hivi ndivyo waislamu wanavyotaka, pawepo mjadala na uchunguzi kuhusu haki iliyokiukwa kama ipo, muafaka upatikane.