Tatizo la umeme halitakuja liishe

Tatizo la umeme halitakuja liishe

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,768
Reaction score
49,940
Kwenye masuala ya management, tunasema mafanikio yoyote yanategemea aina watu ulio nao. People are the hub of the success wheel.

Aina ya watu ulio nao ndio wanaamua kampuni/taasisi/serikali, ifanikiwe au ishindwe kabisa. Haijalishi una pesa kiasi gani, haijalishi una vifaa kiasi gani, kama watu ulio nao hawana uwezo, utaanguka tu. Kama una watu wa hovyo, wanaweza kutumia pesa kununua mitambo na vifaa hovyo, wanaweza kuipa kandarasi kampuni ya hovyo. Hata uwe na vifaa vizuri na vya kisasa kiasi gani, ukiwa na operators wa hovyo, vyote vitakufa na hutaambulia chochote.

Wote tunajua jinsi huduma ya umeme ilivyo duni nchini mwetu. Siyo kwa sababu hakuna maji au gas, siyo kwa sababu hatuna nguzo au nyaya, wala siyo kwa sababu hatuna mitambo ya kuzalishia umeme. Tunaona barabara zinazojengwa kabla hazijamakizika zinaanza kuwekwa viraka, n.k; kila mahali ni hovyo. SABABU KUBWA NI KWAMBA HATUNA WATU SAHIHI WENYE UWEZO.

Kwa ujumla Serikali yetu haijawahi kufanya chochote kile kwa weledi na kwa mafanikio. Waliopo Serikalini hawanahata uwezo wa kumpata mkandarasi mzuri wa kuweza kujenga barabara kwa viwango bora.

Maadam umeme unaendelea kuzalishwa na shirika la TANESCO ambalo lipo chini ya Serikali, tusitarajie ufanisi wowote ule hata siku moja. Watanzania tukubali kuwa haya ndiyo ni maisha yetu ya kila siku. Aina ya watu waliopo huko Serikalini na namna wanavyopatikana, tusitarajie mafanikio yoyote zaidi ya hadithi za kila siku zisizoendana na uhalisia. Serikalini tuna watu mabingwa wa kuendesha mambo kwa ulaghai na uwongo. Na wao hiyo huiita ndiyo siasa ya Tanzania.

Siyo kwamba nchi haina watu wenye uwezo. Watanzania wenye uwezo wapo, na wengine wanafanya kazi hata nje ya Tanzania wakiwa na heshima kubwa kutokana na weledi wao. Lakini hata ndani ya nchi wapo ambao wangeweza kuleta mabadiliko makubwa.

Lakini watu wenye akili na uwezo mkubwa katika weledi, hata siku moja hawakubali kuwa machawa, huwa ni watu walionyoka, ni watu ambao siyo wanafiki, wao spade ni spade. Watu wa namna hiyo huwezi kuwakuta Serikalini. Kwa sababu serikalini sifa kubwa ya mtu kuteuliwa kuongoza taasisi zilizo chini ya Serikali ni uchawa, unafiki na kujuana. Na wanaoweza kufanya hayo ni wale tu wenye akili ndogo na uwezo mdogo ambao huwa wanataka kuziba pengo la upungufu wao katika uwezo na akili kwa unafiki wa kusifia na kujikomba kwa watawala. Na kwa sababu Serikali inapenda sana kusifiwa, itaendelea kuwa na aina hiyo hiyo ya watu, na Watanzania wataendelea kuishi kwa kupewa huduma duni.

Kupunguza tatizo hilo la kuwa na watu wenye uwezo duni kwenye taasisi zilizo chini ya Serikali, ilikuwa ni ile katiba ya Jaji Warioba. Yaani watu wapewe nafasi mbalimbali kwa kuangalia weledi wao na kwa kufuata kanuni za ajira. Rais asijihusishe kabisa na uteuzi wa wakuu wa kuendesha hizo taasisi. Rais abakie na mamlaka ya kuwateua mawaziri basi. Wengine wote wapatikane kwa weledi wao na siyo kupewa nafasi hizo kwa hisani ya Rais.
 
Mzizi wa Tanesco utakatwa baada ya kuundwa serikali mpya yenye katiba mpya kali isiyoruhusu kusamehe madeni makubwa ya Tanesco kwenye nchi kama Zanzibar kisha mzigo tubebe sisi afu tushindwe kununua vifaa endeshi vya shirika.
 
Kuna watu kabisa wanategemea watapa ufanisi kutoka kwenye serekali hii. Sijawahi kuona chochote kinachoendeshwa kwa ufanisi na serekali hii.
Huwezi kuona kwa sababu wewe ulishajipofusha akili na macho yako na hivyo kuona maruerue tu mbele yako. Siku ukiacha akili yako na macho yako yakatizama mambo katika uhalisia wake kwa hakika utaona maajabu makubwa sana yaliyofanywa na serikali ya Rais wetu mpendwa Na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mama Samia Suluhu Hasssan.

Utaona mapinduzi katika Secta ya kilimo kulikowekezwa mabilioni ya pesa ambapo sasa bajeti ni Billion 970 ,utaona mapinduzi katika Afya ambako zaidi ya Trilioni sita zimetiririshwa huko,utaona mapinduzi katika Elimu,nishati, miundombinu,uchumi na maeneo karibu yote utakakopeleka jicho lako utaona mafanikio makubwa yaliyofikiwa na kupatikana.
 
Kuna mitambo fulani naona imeharibika inabidi inunuliwe mpya ifungwe 😄
Au kuna system imezingua kwa hiyo inahitajika bilion 10 kuboresha system mpya 😄

Kwa kwa kwa

Ova
 
Kwenye masuala ya management, tunasema mafanikio yoyote yanategemea aina watu ulio nao. People are the hub of the success wheel.

Aina ya watu ulio nao ndio wanaamua kampuni/taasisi/serikali, ifanikiwe au ishindwe kabisa. Haijalishi una pesa kiasi gani, haijalishi una vifaa kiasi gani, kama watu ulio nao hawana uwezo, utaanguka tu. Kama una watu wa hovyo, wanaweza kutumia pesa kununua mitambo na vifaa hovyo, wanaweza kuipa kandarasi kampuni ya hovyo. Hata uwe na vifaa vizuri na vya kisasa kiasi gani, ukiwa na operators wa hovyo, vyote vitakufa na hutaambulia chochote.

Wote tunajua jinsi huduma ya umeme ilivyo duni nchini mwetu. Siyo kwa sababu hakuna maji au gas, siyo kwa sababu hatuna nguzo au nyaya, wala siyo kwa sababu hatuna mitambo ya kuzalishia umeme. Tunaona barabara zinazojengwa kabla hazijamakizika zinaanza kuwekwa viraka, n.k; kila mahali ni hovyo. SABABU KUBWA NI KWAMBA HATUNA WATU SAHIHI WENYE UWEZO.

Kwa ujumla Serikali yetu haijawahi kufanya chochote kile kwa weledi na kwa mafanikio. Waliopo Serikalini hawanahata uwezo wa kumpata mkandarasi mzuri wa kuweza kujenga barabara kwa viwango bora.

Maadam umeme unaendelea kuzalishwa na shirika la TANESCO ambalo lipo chini ya Serikali, tusitarajie ufanisi wowote ule hata siku moja. Watanzania tukubali kuwa haya ndiyo ni maisha yetu ya kila siku. Aina ya watu waliopo huko Serikalini na namna wanavyopatikana, tusitarajie mafanikio yoyote zaidi ya hadithi za kila siku zisizoendana na uhalisia. Serikalini tuna watu mabingwa wa kuendesha mambo kwa ulaghai na uwongo. Na wao hiyo huiita ndiyo siasa ya Tanzania.

Siyo kwamba nchi haina watu wenye uwezo. Watanzania wenye uwezo wapo, na wengine wanafanya kazi hata nje ya Tanzania wakiwa na heshima kubwa kutokana na weledi wao. Lakini hata ndani ya nchi wapo ambao wangeweza kuleta mabadiliko makubwa.

Lakini watu wenye akili na uwezo mkubwa katika weledi, hata siku moja hawakubali kuwa machawa, huwa ni watu walionyoka, ni watu ambao siyo wanafiki, wao spade ni spade. Watu wa namna hiyo huwezi kuwakuta Serikalini. Kwa sababu serikalini sifa kubwa ya mtu kuteuliwa kuongoza taasisi zilizo chini ya Serikali ni uchawa, unafiki na kujuana. Na wanaoweza kufanya hayo ni wale tu wenye akili ndogo na uwezo mdogo ambao huwa wanataka kuziba pengo la upungufu wao katika uwezo na akili kwa unafiki wa kusifia na kujikomba kwa watawala. Na kwa sababu Serikali inapenda sana kusifiwa, itaendelea kuwa na aina hiyo hiyo ya watu, na Watanzania wataendelea kuishi kwa kupewa huduma duni.

Kupunguza tatizo hilo la kuwa na watu wenye uwezo duni kwenye taasisi zilizo chini ya Serikali, ilikuwa ni ile katiba ya Jaji Warioba. Yaani watu wapewe nafasi mbalimbali kwa kuangalia weledi wao na kwa kufuata kanuni za ajira. Rais asijihusishe kabisa na uteuzi wa wakuu wa kuendesha hizo taasisi. Rais abakie na mamlaka ya kuwateua mawaziri basi. Wengine wote wapatikane kwa weledi wao na siyo kupewa nafasi hizo kwa hisani ya Rais.
Umeongea uhalisia kabisa. Serikalini kuna watendaji ambao uwezo wao ni wa kawaida sana na wanajaribu kulificha hilo kwa mbwembwe za maneno, kufoka foka, na kusifia

Wenye uwezo hawadumu kwasababu wenzao wanawaona kama hawaendani nao. Wanapotoa mawazo yaliyokinyume na mipango na matarajio ya wengine

Hata hivyo hili kwa kiasi kikubwa linachangiwa na kuwa na viongozi wa aina hiyo hiyo kwenye top position

Kiongozi ndio dira ya taasisi. Yeye ndio mwenye maono na watu wote wanasubiri wafuate mwongo atakaotoa

Inapotokea kiongozi akawa hana dira wala mwelekeo, anapenda mapambio kuliko uhalisia. Akiambiwa kwa maneno anaamini pasipo kufanya ufuatiliaji wale wote waliochini yake wata underperform kwasababu always human being are lazy. Mfanyakazi yoyote anahitaji close supervision ili uone matokeo chanya

Nchi itapiga hatua na kuachana na hayo yote uliyosema endapo tutapata viongozi wenye maono na wasioamini katika kukwezwa kwa maneno na sifa zisizo na msingi
 
Mzizi wa Tanesco utakatwa baada ya kuundwa serikali mpya yenye katiba mpya kali isiyoruhusu kusamehe madeni makubwa ya Tanesco kwenye nchi kama Zanzibar kisha mzigo tubebe sisi afu tushindwe kununua vifaa endeshi vya shirika.
Kwa sasa umeme na hudumu ya umeme ni ya uhakika hapa nchini ,ambapo hakuna changamoto kama ilivyokuwa swali.ambapo ukiona umeme haupo basi ujuwe kunakuwa kumejitokeza hitilafu ndogondogo ambazo kushughulikiwa na kumalizwa kwa haraka. Na pia taarifa hutolewa haraka sana na mamlaka kuwapatia taarifa watanzania.
 
Mimi napinga haya mambo ya gridi ya taifa ya jumla jumla, yaani ukianguka waya kibaha, mpaka Tarime na biharamulo hakuna umeme.

Gridi ivunjwe vunjwe kikanda, kanda ya ziwa na kanda ya kati watumie rusumo na malagalasi, kanda ya kati watumie mtera na kidatu na umeme wa jua na upepo. Kaskazini watumie pangani, ukanda wa pwani gesi.

Hii haimaanishi gridi ya taifa ife, hapana, tuwe na standby modes za kuchukua nafasi kwa haraka inapotokea dharura.

Ikitokea hali ya vita, mtu anapiga kombora kitu kimoja tu, nchi mzima gizani.

Tusiweke mayai yote katika kapu moja
 
Kwenye masuala ya management, tunasema mafanikio yoyote yanategemea aina watu ulio nao. People are the hub of the success wheel.

Aina ya watu ulio nao ndio wanaamua kampuni/taasisi/serikali, ifanikiwe au ishindwe kabisa. Haijalishi una pesa kiasi gani, haijalishi una vifaa kiasi gani, kama watu ulio nao hawana uwezo, utaanguka tu. Kama una watu wa hovyo, wanaweza kutumia pesa kununua mitambo na vifaa hovyo, wanaweza kuipa kandarasi kampuni ya hovyo. Hata uwe na vifaa vizuri na vya kisasa kiasi gani, ukiwa na operators wa hovyo, vyote vitakufa na hutaambulia chochote.

Wote tunajua jinsi huduma ya umeme ilivyo duni nchini mwetu. Siyo kwa sababu hakuna maji au gas, siyo kwa sababu hatuna nguzo au nyaya, wala siyo kwa sababu hatuna mitambo ya kuzalishia umeme. Tunaona barabara zinazojengwa kabla hazijamakizika zinaanza kuwekwa viraka, n.k; kila mahali ni hovyo. SABABU KUBWA NI KWAMBA HATUNA WATU SAHIHI WENYE UWEZO.

Kwa ujumla Serikali yetu haijawahi kufanya chochote kile kwa weledi na kwa mafanikio. Waliopo Serikalini hawanahata uwezo wa kumpata mkandarasi mzuri wa kuweza kujenga barabara kwa viwango bora.

Maadam umeme unaendelea kuzalishwa na shirika la TANESCO ambalo lipo chini ya Serikali, tusitarajie ufanisi wowote ule hata siku moja. Watanzania tukubali kuwa haya ndiyo ni maisha yetu ya kila siku. Aina ya watu waliopo huko Serikalini na namna wanavyopatikana, tusitarajie mafanikio yoyote zaidi ya hadithi za kila siku zisizoendana na uhalisia. Serikalini tuna watu mabingwa wa kuendesha mambo kwa ulaghai na uwongo. Na wao hiyo huiita ndiyo siasa ya Tanzania.

Siyo kwamba nchi haina watu wenye uwezo. Watanzania wenye uwezo wapo, na wengine wanafanya kazi hata nje ya Tanzania wakiwa na heshima kubwa kutokana na weledi wao. Lakini hata ndani ya nchi wapo ambao wangeweza kuleta mabadiliko makubwa.

Lakini watu wenye akili na uwezo mkubwa katika weledi, hata siku moja hawakubali kuwa machawa, huwa ni watu walionyoka, ni watu ambao siyo wanafiki, wao spade ni spade. Watu wa namna hiyo huwezi kuwakuta Serikalini. Kwa sababu serikalini sifa kubwa ya mtu kuteuliwa kuongoza taasisi zilizo chini ya Serikali ni uchawa, unafiki na kujuana. Na wanaoweza kufanya hayo ni wale tu wenye akili ndogo na uwezo mdogo ambao huwa wanataka kuziba pengo la upungufu wao katika uwezo na akili kwa unafiki wa kusifia na kujikomba kwa watawala. Na kwa sababu Serikali inapenda sana kusifiwa, itaendelea kuwa na aina hiyo hiyo ya watu, na Watanzania wataendelea kuishi kwa kupewa huduma duni.

Kupunguza tatizo hilo la kuwa na watu wenye uwezo duni kwenye taasisi zilizo chini ya Serikali, ilikuwa ni ile katiba ya Jaji Warioba. Yaani watu wapewe nafasi mbalimbali kwa kuangalia weledi wao na kwa kufuata kanuni za ajira. Rais asijihusishe kabisa na uteuzi wa wakuu wa kuendesha hizo taasisi. Rais abakie na mamlaka ya kuwateua mawaziri basi. Wengine wote wapatikane kwa weledi wao na siyo kupewa nafasi hizo kwa hisani ya Rais.
Ila watanzania nawaheshimu sana unaweza kuta hili la umeme kukatika ni deal limepangwa fedha za emergency zitoke watu wapigeeee parefu.
Hayo ndio maisha tunayoishi nchini kwetu deals deals..
 
Huwezi kuona kwa sababu wewe ulishajipofusha akili na macho yako na hivyo kuona maruerue tu mbele yako. Siku ukiacha akili yako na macho yako yakatizama mambo katika uhalisia wake kwa hakika utaona maajabu makubwa sana yaliyofanywa na serikali ya Rais wetu mpendwa Na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mama Samia Suluhu Hasssan.

Utaona mapinduzi katika Secta ya kilimo kulikowekezwa mabilioni ya pesa ambapo sasa bajeti ni Billion 970 ,utaona mapinduzi katika Afya ambako zaidi ya Trilioni sita zimetiririshwa huko,utaona mapinduzi katika Elimu,nishati, miundombinu,uchumi na maeneo karibu yote utakakopeleka jicho lako utaona mafanikio makubwa yaliyofikiwa na kupatikana.
Watu kama nyie ndio mtakuwa kuni za kukoleza moto kama kweli kiama kipo

Huko kwenye afya, vifo vinavyotokana na uzembe vinazidi kuongezeka kama bajeti yako hewa inavyoongezeka. Wagonjwa hospitali za serikali wanakazi ya kuangaliana na madaktari kana kwamba wao ndo dawa na vifaa tiba. Unahudhuria chumba cha daktari huku maduka ya dawa nje yanakungoja si kwa wagonjwa wa nje wala wanaolazwa, wote kazi ya daktari ni kuandika na kutoa maelezo kuwa hizi dawa hapa hakuna kanunue nje. Hiyo bajeti imeongezeka kwenye nini kama sio hewa?? au imeongezeka kwenye kupaka rangi majengo yavutie watazamaji

Kwenye Elimu mnatandaza mabanda ya kuku na kuziita shule. Shule hazina sifa ya kuitwa shule ila kwasababu watoto wa maskini mnawakusanya huko mnaziita shule. Kama ni shule kweli, mbona watoto wa vigogo hatuwaoni huko? Hata katibu kata hathubutu kumsomesha mtoto wake kwenye hayo mabanda ya kuku. Kataa kwa kuorodhesha viongozi wanaosomesha watoto kwenye shule za kata ukianza na sehemu

Mnawadanganya wakulima kuwa bajeti imeongezeka na masoko ya mazoa yao hakuna. Mpaka leo nchi yenye vyanzo kibao vya maji bado mkombozi wa wakulima wengi ni mvua. Katika ulimwengu wa sayansi na tecknolojia bado mkulima anategemea jembe la mkono

Nchi inadumazwa na watu kama nyie ambao macho na maskio yote yanasikiliza tumbo linataka nini badala ya kuangalia uhalisia
 
Kwa sasa umeme na hudumu ya umeme ni ya uhakika hapa nchini ,ambapo hakuna changamoto kama ilivyokuwa swali.ambapo ukiona umeme haupo basi ujuwe kunakuwa kumejitokeza hitilafu ndogondogo ambazo kushughulikiwa na kumalizwa kwa haraka. Na pia taarifa hutolewa haraka sana na mamlaka kuwapatia taarifa watanzania.
Sio kweli
 
Kwenye masuala ya management, tunasema mafanikio yoyote yanategemea aina watu ulio nao. People are the hub of the success wheel.

Aina ya watu ulio nao ndio wanaamua kampuni/taasisi/serikali, ifanikiwe au ishindwe kabisa. Haijalishi una pesa kiasi gani, haijalishi una vifaa kiasi gani, kama watu ulio nao hawana uwezo, utaanguka tu. Kama una watu wa hovyo, wanaweza kutumia pesa kununua mitambo na vifaa hovyo, wanaweza kuipa kandarasi kampuni ya hovyo. Hata uwe na vifaa vizuri na vya kisasa kiasi gani, ukiwa na operators wa hovyo, vyote vitakufa na hutaambulia chochote.

Wote tunajua jinsi huduma ya umeme ilivyo duni nchini mwetu. Siyo kwa sababu hakuna maji au gas, siyo kwa sababu hatuna nguzo au nyaya, wala siyo kwa sababu hatuna mitambo ya kuzalishia umeme. Tunaona barabara zinazojengwa kabla hazijamakizika zinaanza kuwekwa viraka, n.k; kila mahali ni hovyo. SABABU KUBWA NI KWAMBA HATUNA WATU SAHIHI WENYE UWEZO.

Kwa ujumla Serikali yetu haijawahi kufanya chochote kile kwa weledi na kwa mafanikio. Waliopo Serikalini hawanahata uwezo wa kumpata mkandarasi mzuri wa kuweza kujenga barabara kwa viwango bora.

Maadam umeme unaendelea kuzalishwa na shirika la TANESCO ambalo lipo chini ya Serikali, tusitarajie ufanisi wowote ule hata siku moja. Watanzania tukubali kuwa haya ndiyo ni maisha yetu ya kila siku. Aina ya watu waliopo huko Serikalini na namna wanavyopatikana, tusitarajie mafanikio yoyote zaidi ya hadithi za kila siku zisizoendana na uhalisia. Serikalini tuna watu mabingwa wa kuendesha mambo kwa ulaghai na uwongo. Na wao hiyo huiita ndiyo siasa ya Tanzania.

Siyo kwamba nchi haina watu wenye uwezo. Watanzania wenye uwezo wapo, na wengine wanafanya kazi hata nje ya Tanzania wakiwa na heshima kubwa kutokana na weledi wao. Lakini hata ndani ya nchi wapo ambao wangeweza kuleta mabadiliko makubwa.

Lakini watu wenye akili na uwezo mkubwa katika weledi, hata siku moja hawakubali kuwa machawa, huwa ni watu walionyoka, ni watu ambao siyo wanafiki, wao spade ni spade. Watu wa namna hiyo huwezi kuwakuta Serikalini. Kwa sababu serikalini sifa kubwa ya mtu kuteuliwa kuongoza taasisi zilizo chini ya Serikali ni uchawa, unafiki na kujuana. Na wanaoweza kufanya hayo ni wale tu wenye akili ndogo na uwezo mdogo ambao huwa wanataka kuziba pengo la upungufu wao katika uwezo na akili kwa unafiki wa kusifia na kujikomba kwa watawala. Na kwa sababu Serikali inapenda sana kusifiwa, itaendelea kuwa na aina hiyo hiyo ya watu, na Watanzania wataendelea kuishi kwa kupewa huduma duni.

Kupunguza tatizo hilo la kuwa na watu wenye uwezo duni kwenye taasisi zilizo chini ya Serikali, ilikuwa ni ile katiba ya Jaji Warioba. Yaani watu wapewe nafasi mbalimbali kwa kuangalia weledi wao na kwa kufuata kanuni za ajira. Rais asijihusishe kabisa na uteuzi wa wakuu wa kuendesha hizo taasisi. Rais abakie na mamlaka ya kuwateua mawaziri basi. Wengine wote wapatikane kwa weledi wao na siyo kupewa nafasi hizo kwa hisani ya Rais.
kuna hitilafu kidogo tu inashughulikiwa 🐒
 
Mimi napinga haya mambo ya gridi ya taifa ya jumla jumla, yaani ukianguka waya kibaha, mpaka Tarime na biharamulo hakuna umeme.

Gridi ivunjwe vunjwe kikanda, kanda ya ziwa na kanda ya kati watumie rusumo na malagalasi, kanda ya kati watumie mtera na kidatu na umeme wa jua na upepo. Kaskazini watumie pangani, ukanda wa pwani gesi.

Hii haimaanishi gridi ya taifa ife, hapana, tuwe na standby modes za kuchukua nafasi kwa haraka inapotokea dharura.

Ikitokea hali ya vita, mtu anapiga kombora kitu kimoja tu, nchi mzima gizani.

Tusiweke mayai yote katika kapu moja
Ni kweli naunga mkono hoja
 
make everything possible uwe online for more umeme updates 🐒

technical support teams, are on site working very hard, to restore huduma ya umeme katika hali ya kawaida..

resilience na subra ni muhimu sana on this 🐒
 
Huwezi kuona kwa sababu wewe ulishajipofusha akili na macho yako na hivyo kuona maruerue tu mbele yako. Siku ukiacha akili yako na macho yako yakatizama mambo katika uhalisia wake kwa hakika utaona maajabu makubwa sana yaliyofanywa na serikali ya Rais wetu mpendwa Na Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mama Samia Suluhu Hasssan.

Utaona mapinduzi katika Secta ya kilimo kulikowekezwa mabilioni ya pesa ambapo sasa bajeti ni Billion 970 ,utaona mapinduzi katika Afya ambako zaidi ya Trilioni sita zimetiririshwa huko,utaona mapinduzi katika Elimu,nishati, miundombinu,uchumi na maeneo karibu yote utakakopeleka jicho lako utaona mafanikio makubwa yaliyofikiwa na kupatikana.
Ww kwasababu umezaliwa na kukulia hapa hapa bila kutoka nje ya nchi, haya kwako inaweza kuwa ni mambo makubwa. Jitahidi utoke nje ya nchi ndio utajua uduni unaosababishwa na uzembe ulioko hapa nchini.
 
Pamoja na haya uliyosema ila tutakapofikia hatua ya kutenga siasa na taaluma tutafika mbali sana. Mathalan mtu akitaka kuwa mkurugenzi wa Tanesco sharti ateuliwe na Rais. Hii si sawa hata kidogo. Tukitaka kupata viongozi wenye sifa sharti waombe kazi, wafanyiwe usaili na wachujwe kwa sifa zao na sera zao juu ya kuendeleza shirika. Hili la kila kitu afanye Rais si sawa. Tutachelewa sana kwenye maendeleo
Umeongea uhalisia kabisa. Serikalini kuna watendaji ambao uwezo wao ni wa kawaida sana na wanajaribu kulificha hilo kwa mbwembwe za maneno, kufoka foka, na kusifia

Wenye uwezo hawadumu kwasababu wenzao wanawaona kama hawaendani nao. Wanapotoa mawazo yaliyokinyume na mipango na matarajio ya wengine

Hata hivyo hili kwa kiasi kikubwa linachangiwa na kuwa na viongozi wa aina hiyo hiyo kwenye top position

Kiongozi ndio dira ya taasisi. Yeye ndio mwenye maono na watu wote wanasubiri wafuate mwongo atakaotoa

Inapotokea kiongozi akawa hana dira wala mwelekeo, anapenda mapambio kuliko uhalisia. Akiambiwa kwa maneno anaamini pasipo kufanya ufuatiliaji wale wote waliochini yake wata underperform kwasababu always human being are lazy. Mfanyakazi yoyote anahitaji close supervision ili uone matokeo chanya

Nchi itapiga hatua na kuachana na hayo yote uliyosema endapo tutapata viongozi wenye maono na wasioamini katika kukwezwa kwa maneno na sifa zisizo na msingi
 
Back
Top Bottom