Tatizo la masikio: Nimepoteza usikivu baada ya kuumwa Malaria kali

Benatia

Senior Member
Nov 14, 2019
122
274
Habari za wakati huu wakuu, natumaini sote humu ni wazima wa afya, na kama kuna ambao labda hali zao kiafya sio njema Mungu awasaidie ili muweze kupata unafuu.

Nimeamua niandike huu uzi nikiwa na huzuni kubwa sana moyoni kwa hili janga lililo nitokea.

Mwaka 2013 mwezi wa 8 nikiwa nasoma kidato cha pili niliugua Malaria kali sana iliyopeleka mpaka kufika hatua ya kutishia maisha yangu, naweza kusema zilikuwa zimebaki dakika kadhaa tu huenda nisingekuwepo tena hapa duniani.

Lakini Mungu ni mwema sana hatimaye niliweza kupona kabisa.

Sasa wakati naelekea kupona ghafla masikio yangu yalianza kupoteza usikivu. Yaani ilikuwa kama masihara tu masikio yangu yaliziba kabisa kiasi ambacho sikuweza kusikia mpaka muda huu ninapoandika hapa. Pia ikumbukwe kwamba nilizaliwa masikio yakiwa mazima kabisa bila tatizo lolote.

Halafu kuna jambo lingine ambalo huwa linanichanganya ni kwamba tangu nipoteze usikivu ndani ya masikio yangu kuna miungurumo fulani hivi ya ajabu ambayo huwa siielewi kabisa.

Kwa kweli naumia sana kila nikitafakari hatma ya maisha yangu ya baadae na ukizingatia mimi bado ni kijana mdogo tu mwenye miaka 22, ndoto zangu zote zimezima kabisa.

Msaada jamani kama kuna mtu yeyote mwenye utaalamu kuhusu masikio anisaidie please!

Asanteni!🙏
 
Pole sana mkuu iyo ndo madhara ambayo yanabaki ukikoswa koswa na jeneza,pole sana hapo nenda ccbrt uone kama kuna uwezekano wa kuwekewa ata vifaa,kutokusikia inaumiza kuna dogo nae mtot mdogo ajaweza kuongea aliumwa sana alikula sindano nyingi za cristpen mpka akazibuka now hasikii hata na kuongea hawezi vizuri maana alikua bado hajajifunza kuongea ko kapata ububu na ukiziwi apo apo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
nenda hosp. zenye uwezo zaidi utakuwa poa mkuu Mungu ni mkubwa
 
Pole sana mkuu iyo ndo madhara ambayo yanabaki ukikoswa koswa na jeneza,pole sana hapo nenda ccbrt uone kama kuna uwezekano wa kuwekewa ata vifaa,kutokusikia inaumiza kuna dogo nae mtot mdogo ajaweza kuongea aliumwa sana alikula sindano nyingi za cristpen mpka akazibuka now hasikii hata na kuongea hawezi vizuri maana alikua bado hajajifunza kuongea ko kapata ububu na ukiziwi apo apo

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante mkuu.. nitajaribu kufata ushauri wako...kwa kweli inauma sana hasa ukikumbuka ulizaliwa mzima kabisa afu baae unakuja kukumbwa na haya masaibu.dah!...
 
Mkuu cha kwanza kabisa kubali hali yako kwamba sasa wewe ni kiziwi

Ukishaikubali hali yako utaona maisha yanasonga tu
Hili tatizo likishatokea halitibiki la sivyo utapoteza hela na muda sana

Karibu PM kwa ushauri zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana mkuu. Tatizo Kama hili lilinipata na mimi kupitia ugonjwa Kama huo wa malaria nikiwa std seven 2001. Nikamuachia mungu ,nikajipa nguvu nikasonga mbele mpaka chuo kikuu na MA nimeiweka kibindoni pia. Jikaze usiwaze sana .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom