Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,333
- 9,755
Ndugu zangu Watanzania,
Rais samia jasiri muongoza njia,mama wa shoka,chuma cha Reli,Nuru ya wanyonge,Shujaa wa Afrika,Sauti ya wa Afrika,Mtetezi wa wanyonge anawasikiliza watanzania wote. masikio yake yapo wazi kusikiliza Sauti,kero, changamoto na malalamiko na mafanikio kutoka katika vinywa vya watanzania wote. Natambua ya kuwa wengine wanakuwa na hamu ,kiu na shauku kubwa sana ya kutaka kufikisha kero zao moja kwa moja wamuonapo ana kwa ana mh Rais awapo ziarani,Natambua wengine wanamuona Rais samia kama mkombozi wao,Natambua matumaini makubwa watanzania waliyobeba katika vifua vyao juu ya kupata suluhu wamuonapo Rais samia karibu yao.
Ndio maana unaona watanzania wengine wakiomba kupewa nafasi wafikishe kero zao,shida zao, changamoto zao, matatizo yao na mizigo yao ili wasaidiwe na mh Rais ,ili watue mizigo yao. Natambua kuwa wengine wanakuwa wamepita katika ofisi mbalimbali na wamekosa majibu ya kueleweka kutoka kwa viongozi wahusika ,hivyo wamuonapo mh Rais inakuwa ni kama kuona nuru katikati ya Giza Tororo kando kando ya daraja la miti. Wanakuwa wanaona ndio Tumaini na faraja yao ya mwisho ,ndio mtu wa mwisho anayeweza kuwafuta machozi,kuwatua mizigo na kuwapatia majibu ya kueleweka na kuridhika.Ndio maana wengine wanakuwa wanapambana kupata fursa walau ya kupata fursa ya kutoa na kusema neno kwa Rais wao ili kupata kulifikia sikio lake na hatimaye kauli yake itakayo ponya na kuondoa dukuduku lao.
Lakini jambo ambalo ningependa lifahamike ni kuwa ni jambo gumu na lisilowezekana kwa Mh Rais kuweza kusikiliza kero ya mwananchi mmoja mmoja kati ya maelfu ya wananchi wanaokuwa wamesimama pembezoni mwa barabara kumsubiri mh Rais au awapo katika mkutano wa hadhara. Ni ngumu sana ndugu zangu kwa jambo hili kufanyika. Hasa kwa kuzingatia Ratiba ya mh Rais,uwingi wa watu,ugumu wa kuweza kusikiliza kila mtu. Jiulize atatumia muda au siku ngapi kusikiliza kero za maelfu ya watu wanaokuwa wamehudhuria? Nani anaweza kufanikiwa katika jambo hili? Vipi maeneo mengine nayo wanayokuwa wanamsubiri mh Rais? Nao watatumia muda gani kwa kila mtu kufikisha kero yake binafsi hadi ya mirathi au kuzulumiana ardhi au mali alizoacha marehemu?
Ikumbukwe ya kuwa Ukitaka kulazimisha kutoa majibu ya papo kwa papo unaweza kujikuta unatoa maamuzi yanayoumiza upande wa pili ambao ulikuwa na haki ila haukusikilizwa. unauimiza upande wa pili kwa kuwa ulikuwa huna taarifa za kutosha juu ya mgogoro husika na unachukua maamuzi ya kuumiza kwa kuwa tu mleta malalamiko alitunga uongo kwa kulia machozi na kugaragala chini kwenye vumbi hadi huruma zinakushika na kutoa maamuzi ya kumpa haki asiyostahili kupewa ,halafu kumbe madai yake siyo ya kweli ila tu katumia nafasi hiyo kupika uongo wake. Mwisho wa siku ikionekana ni uongo na Rais alifanya maamuzi ya upendeleo inakuwa inaleta picha mbaya kwa Taasisi ya Urais na Rais mwenyewe kwa kuonekana inafanya na kuchukua hatua kwa mihemuko na kukurupuka pasipo kuwa na Taarifa sahihi juu ya jambo fulani ,hasa kwa kuzingatia unaletewa taarifa au jambo ghafla ghafla tu bila kujuwa undani wake na kiini chake.
Ndio maana kwa Ma Rais na viongozi walioiva Aina ya Rais Samia na wenye kujuwa maana ya uongozi na namna ya kutatua na kumaliza migogoro , kero na changamoto za mtu mmoja mmoja huwezi ukawakuta wakikurupuka kutoa maamuzi ya papo kwa papo bila Taarifa za kina kiganjani pao.huwezi ukawakuta wakipaniki na kutoa majibu au suluhisho kwa hisia tu za namna mtu alivyojieleza mbele yao,maana kuna watu anaweza kutunga uongo kwa hisia kali mpaka machozi yakakutoka .Na katika hili nafikiri mnakumbuka mama mmoja miaka kadhaa nyuma ambaye alijitokeza hadharani kuelezea mbele ya Rais ambaye alikuwa mgeni Rasmi siku ya mahakama kwa hisia kali ,machozi ya uchungu na kupiga magoti mbele ya Mh Rais ili asaidiwe mgogoro wake ambao alidai Anaonewa na kupokwa haki yake, lakini mwisho wa siku ikaja kugundulika kuwa alikuwa muongo na alimdanganya mh Rais.
Kuna wale wanaouliza kuwa kama mh Rais hawezi kumsikiliza mtu mmoja mmoja kwanini anasimama njiani na barabarani? Jibu ni kuwa mh Rais anasimama barabarani ili kuwasalimu wananchi wote wanaokuwa wamehudhuria na kusimama Eneo hilo. Pili mh Rais anasimama kusikiliza kero , changamoto na matatizo ya wananchi wa Eneo hilo kupitia mwakilishi wao ambaye ni mbunge,na baada ya hapo ndipo Rais hujibu mwenyewe pamoja na kuwapa nafasi wasaidizi wake na wateule wake wakiwepo mawaziri kila mmoja kwa wizara yake kwa kadri ilivyoguswa na muwakilisha wa wananchi ambaye ni mbunge na kutoa majibu kwa niaba ya serikali,mwisho pia kama kuna nyongeza katika majibu ya waziri ndipo naye Rais huongezea na kutoa majibu na ufafanuzi wa mambo mengine mengi yatakayo tekelezwa na serikali yake Eneo hilo au jimbo hilo hata kama hayajaulizwa au kuombwa hapo na mbunge husika.
Ikumbukwe kuwa huku mikoani mh Rais anawasikiliza wananchi kila iitwayo leo kupitia wakuu wa mikoa na wilaya na wengine wengi ambao wapo ofisini kwa ajili ya kupokea kero na changamoto za wananchi na kuzipatia majibu. Hivyo ni jukumu la wananchi kufika katika ofisi za viongozi wetu hawa ambao ni wawakilishi wa Mh Rais ili kupatiwa ufumbuzi wa kero zao. Pia waweza fikisha na kupaza sauti zao kupitia wabunge wetu au madiwani wetu.
Mwisho na kwa umuhimu wa kipekee kabisa napenda niendelee kutoa Rai yangu kwa waheshimiwa wakuu wa mikoa na wilaya kuhakikisha kuwa mnatoka maofisini na kwenda kwa wananchi kuwasikiliza kero zao,kupokea changamoto zao na kutatua shida zao. Shukeni kwa wananchi,Teremkeni kwa watu, kaeni na watanzania kuwasikiliza kero zao. Wapokeani watanzania katika ofisi zenu na kuwapa majibu ,wasikilizeni kwa umakini na unyenyekevu.jiwekeni katika hali ya kufikika katika ofisi zenu. Mkiona watu wananyayua mabango au kupigana vikumbo kutaka kuwasilisha kero kwa mh Rais ni lazima ninyi kujitathmini na kujiuliza kwanini imekuwa hivyo na nani hakutimiza vyema wajibu wake.
Watanzania Tuendelee kumuamini mh Rais wetu na kuendelea kumuunga mkono kwa kuwa ni msikivu na ndio maana kwa unyenyekevu na upendo mkubwa sana anatufuata watanzania huku tunakoishi ili kutusikiliza kero zetu kupitia wabunge na wawakilishi wetu tulio nao. Mama samia ni mama mwenye huruma na upendo mkubwa sana kwetu watanzania.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Rais samia jasiri muongoza njia,mama wa shoka,chuma cha Reli,Nuru ya wanyonge,Shujaa wa Afrika,Sauti ya wa Afrika,Mtetezi wa wanyonge anawasikiliza watanzania wote. masikio yake yapo wazi kusikiliza Sauti,kero, changamoto na malalamiko na mafanikio kutoka katika vinywa vya watanzania wote. Natambua ya kuwa wengine wanakuwa na hamu ,kiu na shauku kubwa sana ya kutaka kufikisha kero zao moja kwa moja wamuonapo ana kwa ana mh Rais awapo ziarani,Natambua wengine wanamuona Rais samia kama mkombozi wao,Natambua matumaini makubwa watanzania waliyobeba katika vifua vyao juu ya kupata suluhu wamuonapo Rais samia karibu yao.
Ndio maana unaona watanzania wengine wakiomba kupewa nafasi wafikishe kero zao,shida zao, changamoto zao, matatizo yao na mizigo yao ili wasaidiwe na mh Rais ,ili watue mizigo yao. Natambua kuwa wengine wanakuwa wamepita katika ofisi mbalimbali na wamekosa majibu ya kueleweka kutoka kwa viongozi wahusika ,hivyo wamuonapo mh Rais inakuwa ni kama kuona nuru katikati ya Giza Tororo kando kando ya daraja la miti. Wanakuwa wanaona ndio Tumaini na faraja yao ya mwisho ,ndio mtu wa mwisho anayeweza kuwafuta machozi,kuwatua mizigo na kuwapatia majibu ya kueleweka na kuridhika.Ndio maana wengine wanakuwa wanapambana kupata fursa walau ya kupata fursa ya kutoa na kusema neno kwa Rais wao ili kupata kulifikia sikio lake na hatimaye kauli yake itakayo ponya na kuondoa dukuduku lao.
Lakini jambo ambalo ningependa lifahamike ni kuwa ni jambo gumu na lisilowezekana kwa Mh Rais kuweza kusikiliza kero ya mwananchi mmoja mmoja kati ya maelfu ya wananchi wanaokuwa wamesimama pembezoni mwa barabara kumsubiri mh Rais au awapo katika mkutano wa hadhara. Ni ngumu sana ndugu zangu kwa jambo hili kufanyika. Hasa kwa kuzingatia Ratiba ya mh Rais,uwingi wa watu,ugumu wa kuweza kusikiliza kila mtu. Jiulize atatumia muda au siku ngapi kusikiliza kero za maelfu ya watu wanaokuwa wamehudhuria? Nani anaweza kufanikiwa katika jambo hili? Vipi maeneo mengine nayo wanayokuwa wanamsubiri mh Rais? Nao watatumia muda gani kwa kila mtu kufikisha kero yake binafsi hadi ya mirathi au kuzulumiana ardhi au mali alizoacha marehemu?
Ikumbukwe ya kuwa Ukitaka kulazimisha kutoa majibu ya papo kwa papo unaweza kujikuta unatoa maamuzi yanayoumiza upande wa pili ambao ulikuwa na haki ila haukusikilizwa. unauimiza upande wa pili kwa kuwa ulikuwa huna taarifa za kutosha juu ya mgogoro husika na unachukua maamuzi ya kuumiza kwa kuwa tu mleta malalamiko alitunga uongo kwa kulia machozi na kugaragala chini kwenye vumbi hadi huruma zinakushika na kutoa maamuzi ya kumpa haki asiyostahili kupewa ,halafu kumbe madai yake siyo ya kweli ila tu katumia nafasi hiyo kupika uongo wake. Mwisho wa siku ikionekana ni uongo na Rais alifanya maamuzi ya upendeleo inakuwa inaleta picha mbaya kwa Taasisi ya Urais na Rais mwenyewe kwa kuonekana inafanya na kuchukua hatua kwa mihemuko na kukurupuka pasipo kuwa na Taarifa sahihi juu ya jambo fulani ,hasa kwa kuzingatia unaletewa taarifa au jambo ghafla ghafla tu bila kujuwa undani wake na kiini chake.
Ndio maana kwa Ma Rais na viongozi walioiva Aina ya Rais Samia na wenye kujuwa maana ya uongozi na namna ya kutatua na kumaliza migogoro , kero na changamoto za mtu mmoja mmoja huwezi ukawakuta wakikurupuka kutoa maamuzi ya papo kwa papo bila Taarifa za kina kiganjani pao.huwezi ukawakuta wakipaniki na kutoa majibu au suluhisho kwa hisia tu za namna mtu alivyojieleza mbele yao,maana kuna watu anaweza kutunga uongo kwa hisia kali mpaka machozi yakakutoka .Na katika hili nafikiri mnakumbuka mama mmoja miaka kadhaa nyuma ambaye alijitokeza hadharani kuelezea mbele ya Rais ambaye alikuwa mgeni Rasmi siku ya mahakama kwa hisia kali ,machozi ya uchungu na kupiga magoti mbele ya Mh Rais ili asaidiwe mgogoro wake ambao alidai Anaonewa na kupokwa haki yake, lakini mwisho wa siku ikaja kugundulika kuwa alikuwa muongo na alimdanganya mh Rais.
Kuna wale wanaouliza kuwa kama mh Rais hawezi kumsikiliza mtu mmoja mmoja kwanini anasimama njiani na barabarani? Jibu ni kuwa mh Rais anasimama barabarani ili kuwasalimu wananchi wote wanaokuwa wamehudhuria na kusimama Eneo hilo. Pili mh Rais anasimama kusikiliza kero , changamoto na matatizo ya wananchi wa Eneo hilo kupitia mwakilishi wao ambaye ni mbunge,na baada ya hapo ndipo Rais hujibu mwenyewe pamoja na kuwapa nafasi wasaidizi wake na wateule wake wakiwepo mawaziri kila mmoja kwa wizara yake kwa kadri ilivyoguswa na muwakilisha wa wananchi ambaye ni mbunge na kutoa majibu kwa niaba ya serikali,mwisho pia kama kuna nyongeza katika majibu ya waziri ndipo naye Rais huongezea na kutoa majibu na ufafanuzi wa mambo mengine mengi yatakayo tekelezwa na serikali yake Eneo hilo au jimbo hilo hata kama hayajaulizwa au kuombwa hapo na mbunge husika.
Ikumbukwe kuwa huku mikoani mh Rais anawasikiliza wananchi kila iitwayo leo kupitia wakuu wa mikoa na wilaya na wengine wengi ambao wapo ofisini kwa ajili ya kupokea kero na changamoto za wananchi na kuzipatia majibu. Hivyo ni jukumu la wananchi kufika katika ofisi za viongozi wetu hawa ambao ni wawakilishi wa Mh Rais ili kupatiwa ufumbuzi wa kero zao. Pia waweza fikisha na kupaza sauti zao kupitia wabunge wetu au madiwani wetu.
Mwisho na kwa umuhimu wa kipekee kabisa napenda niendelee kutoa Rai yangu kwa waheshimiwa wakuu wa mikoa na wilaya kuhakikisha kuwa mnatoka maofisini na kwenda kwa wananchi kuwasikiliza kero zao,kupokea changamoto zao na kutatua shida zao. Shukeni kwa wananchi,Teremkeni kwa watu, kaeni na watanzania kuwasikiliza kero zao. Wapokeani watanzania katika ofisi zenu na kuwapa majibu ,wasikilizeni kwa umakini na unyenyekevu.jiwekeni katika hali ya kufikika katika ofisi zenu. Mkiona watu wananyayua mabango au kupigana vikumbo kutaka kuwasilisha kero kwa mh Rais ni lazima ninyi kujitathmini na kujiuliza kwanini imekuwa hivyo na nani hakutimiza vyema wajibu wake.
Watanzania Tuendelee kumuamini mh Rais wetu na kuendelea kumuunga mkono kwa kuwa ni msikivu na ndio maana kwa unyenyekevu na upendo mkubwa sana anatufuata watanzania huku tunakoishi ili kutusikiliza kero zetu kupitia wabunge na wawakilishi wetu tulio nao. Mama samia ni mama mwenye huruma na upendo mkubwa sana kwetu watanzania.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.