Tatizo la kumbukumbu iliyopitiliza

Tatizo la kumbukumbu iliyopitiliza

Kwani kuna shida kukumbuka vitu vilivyotokea zamani, mimi ni mmoja wao, huwa ninakumbuka vitu na matukio mbali mbali vilivyonitokea zamani wakati nakua, nina uncle wangu alifunga ndoa mwaka 1983 kijijini, juzi hapa tukawa tunapiga story za miaka ya nyuma nikamkumbusha juu ya harusi yake ilivyokuwa na sare ambazo mama zangu walishona, siku hiyo, akawa anashangaa bado nakumbuka wakati nilikuwa binti mdogo sana huo mwaka......Binafsi huwa naona ni NEEMA ambayo Mungu ameiachilia kwangu kukumbuka matukio vya miaka ya nyuma
Hakuna shida kwa upande mmoja kama ulivyoelezea ila kwa upande mwingine hua narudisha kumbukumbu ya mambo mabaya pia, maneno fulani ya kukera au harufu mbaya nilizokutana nazo hua zinabaki na kujirudia, sasa haya ndio huwa nataka niyasahau lakini ndio hivyo inakua vigumu kiasi ni rahisi pia kusababisha kutosamehe kirahisi
 
Hii kitu imekua inanitesa hata mimi , kuna mpaka ndoto niliziota nikiwa darasa la tano ila zinaendelea mpka leo kwa mfumo wa episodes 🤔
Kuhusu ndoto kuendelea kujirudia rudia hiyo sio issue ya kumbukumbu, hizo ndoto huitwa Recurring dreams.

Recurring dreams often signify unresolved conflicts, persistent stress, or unaddressed emotional needs that the subconscious mind is attempting to process.

Kuna kitu kinaendelea kwenye maisha yako au mpaka ukishughulikie ndipo zinakata hizo ndoto.
 
Kuhusu ndoto kuendelea kujirudia rudia hiyo sio issue ya kumbukumbu, hizo ndoto huitwa Recurring dreams.

Recurring dreams often signify unresolved conflicts, persistent stress, or unaddressed emotional needs that the subconscious mind is attempting to process.

Kuna kitu kinaendelea kwenye maisha yako au mpaka ukishughulikie ndipo zinakata hizo ndoto.
Sio kujirudia rudia ni ndoto ya 1996 ikaishia njiani ni kama inakuja kuendelea( mwendelezo 2025, hiyo ya kuna kitu kinaendelea siitaki kwa sababu nipo OK tu kwenye maisha yangu
 
Sio kujirudia rudia ni ndoto ya 1996 ikaishia njiani ni kama inakuja kuendelea( mwendelezo 2025, hiyo ya kuna kitu kinaendelea siitaki kwa sababu nipo OK tu kwenye maisha yangu
Ndio recurring dreams hizo mkuu iwe inajirudia au kufanya muendelezo, kwa sababu kipo kitu ndio ambacho ndio chanzo cha kupata hizo ndoto na kuna muda zinaweza kukata na kuja kurudi tena. Wewe unaweza ukaona upo ok ila hapo ni issue ya subconsious mind, ndoto zote zina sababu zake.

Mfano mimi kuna muda nilikuwa naota ndoto yenye kuhusiana na choo mara kwa mara japo mazingira yanabadilika ila lazima ihusiane na choo. Sikuwa nazingatia na ikaja kukata ila kuna muda ikarudi tena ndipo nilizingatia nikaja kuelewa ni jambo gani ndio lilikuwa nikifanya basi napata hizo ndoto nilikumbuka kipindi cha nyuma ambapo nilikuwa nikifanya hilo jambo na ndio kipindi nilikuwa naota hizo ndoto.
 
Tuanzie hapa,

Ulifaulu vp Olevel, A-level, na chuo

Maana ulichoongea hakikusaidiii

Angalau huku tutajua kumbukumbu zimekusaidia vp
Huko kote nilifaulu vizuri, sasa unaposema nilichoongea hakinisaidii sikuelewi una maanisha nini?
 
Mkuu nashukuru umeeleza kile ambacho unakipitia,naona tunafanana, tena bora umeingia deep hasa kwa mademu, mimi niliamua mengine nisiandike kiundani ila kiukweli kukumbuka vitu vingi sana wakati mwingine kunaleta huzuni kama utaamua kuzingatia.
Na kama kilikuwa kizuri basi kitaendelea kunipa furaha kila ninapokumbuka
Kiukweli nilishagundua kusahau siwezi kwahio hua naamua kuishughulisha akili kwa kusoma vitabu, makala au kuangalia movie tu.
Asante sana mkuu, tupo pamoja 💪
 
Hii ni kama mimi pia Huwa nawakumbuka watu kwa majina yao matatu ,hata nikikutana na mtu kariakoo afu nikutane nae sehem nyingine nakumbuka,me nakumbuka hata matukio ambayo yalitokea nikiwa na miaka mitatu
 
Hii ni kama mimi pia Huwa nawakumbuka watu kwa majina yao matatu ,hata nikikutana na mtu kariakoo afu nikutane nae sehem nyingine nakumbuka,me nakumbuka hata matukio ambayo yalitokea nikiwa na miaka mitatu
Aise, matukio ya miaka mitatu mbona balaa?😀
 
Nakumbuka sherehe ya ubatizo wangu nikiwa na 3 yrs na matukio mengi kibao
 
Dont blame yourrelf bt be proud my friend that means kichwa kipo fresh ngoja ifike mda wa kuambiwa baba shulen wamesema hivi mara huyu anakwambia baba yoyo chumvi imeisha mara kule mwingine anakwambia mbuzi kanywa kahawa ndo utajua hujui. So be proud hata kama sio ya msingi hiyo inakwambia ubongo bado haujakutana na ugoro
 
Back
Top Bottom