housekeeper
Member
- Apr 21, 2020
- 31
- 104
habari wana jukwaa,
Natumai sote ni wazima wa afya njema, na poleni kwa wenye changamoto za aina mbali mbali.
Mimi ni kijana mwenye takribani miaka 32 kwa sasa.
Nina changamoto ya vitu ndani ya mwili wangu ambavyo nahisi inawezekana kuwa ni jini mahaba.
Baadhi ya changamoto nilizo nazo kwenye mwili wangu ni kama ifuatavyo.
1. Kuwashwa mwili hasa kwenye sehemu za siri.
2. Vitu kunitembea mwili kama sisimizi au wadudu wadogo ingawa ukipukuta hukuti chochote.
3. Kuota nimelala na mwanamke pembeni yangu hii inatokea hata mchana nikiwa nimelala.
4. Kuhisi nafanya mapenzi usingizini hadi kufikia mahali nafikia mshindo.
5. Ninapofanya mapenzi na mwanamke ni lazima mwanamke huyo aumwe tumbo au kuumwa baada ya siku kadhaa mbele (baada ya tendo).
Hizo ni Baadhi ya dalili na changamoto nilizo nazo ndani ya mwili wangu.
Nilifanikiwa kupata mtoto miaka ya nyuma ila mtoto ana changamoto ya kuumwa mara kwa mara hadi sasa ana miaka 10.
(Huumwa zaidi mapunye yasiyoisha, homa na UTI)
CHANZO: ilikua mwaka 2012 usiku wa manane, niliona nimelala na mtu pembeni ya kitanda na alikua na sura ya kike. (Ingawa sura sikuitambua.
Mwili ulianza kusisimuka kupita kiasi.
Nilihisi kitu kinatoka kichwani kama kinanivua ngozi (kama unachuna mbuzi halafu unaivua ngozi bila kutumia kisu) hadi sehemu za siri ndipo niliposhtuka na kuhisi kuna kitu kimetoka nikajiangalia sehemu za siri nikakuta Uume umesinyaa.
Toka hapo hadi leo nimekua nikiwashwa na kuhisi vitu kama vidudu au mchanga vinanitambaa ndani ya mwili.
NOTE: hadi sasa sijaoa ingawa nimepata huyo mtoto mmoja.
Kwa mwenye uelewa au mwenye msaada naomba msaada kwenye hili.
Hata kama kuna gharama nitajivuta ili niweze kujikomboa kwenye hii changamoto.
Asanteni na karibu kwa michango.
Natumai sote ni wazima wa afya njema, na poleni kwa wenye changamoto za aina mbali mbali.
Mimi ni kijana mwenye takribani miaka 32 kwa sasa.
Nina changamoto ya vitu ndani ya mwili wangu ambavyo nahisi inawezekana kuwa ni jini mahaba.
Baadhi ya changamoto nilizo nazo kwenye mwili wangu ni kama ifuatavyo.
1. Kuwashwa mwili hasa kwenye sehemu za siri.
2. Vitu kunitembea mwili kama sisimizi au wadudu wadogo ingawa ukipukuta hukuti chochote.
3. Kuota nimelala na mwanamke pembeni yangu hii inatokea hata mchana nikiwa nimelala.
4. Kuhisi nafanya mapenzi usingizini hadi kufikia mahali nafikia mshindo.
5. Ninapofanya mapenzi na mwanamke ni lazima mwanamke huyo aumwe tumbo au kuumwa baada ya siku kadhaa mbele (baada ya tendo).
Hizo ni Baadhi ya dalili na changamoto nilizo nazo ndani ya mwili wangu.
Nilifanikiwa kupata mtoto miaka ya nyuma ila mtoto ana changamoto ya kuumwa mara kwa mara hadi sasa ana miaka 10.
(Huumwa zaidi mapunye yasiyoisha, homa na UTI)
CHANZO: ilikua mwaka 2012 usiku wa manane, niliona nimelala na mtu pembeni ya kitanda na alikua na sura ya kike. (Ingawa sura sikuitambua.
Mwili ulianza kusisimuka kupita kiasi.
Nilihisi kitu kinatoka kichwani kama kinanivua ngozi (kama unachuna mbuzi halafu unaivua ngozi bila kutumia kisu) hadi sehemu za siri ndipo niliposhtuka na kuhisi kuna kitu kimetoka nikajiangalia sehemu za siri nikakuta Uume umesinyaa.
Toka hapo hadi leo nimekua nikiwashwa na kuhisi vitu kama vidudu au mchanga vinanitambaa ndani ya mwili.
NOTE: hadi sasa sijaoa ingawa nimepata huyo mtoto mmoja.
Kwa mwenye uelewa au mwenye msaada naomba msaada kwenye hili.
Hata kama kuna gharama nitajivuta ili niweze kujikomboa kwenye hii changamoto.
Asanteni na karibu kwa michango.