tatizo la hasira za mara kwa mara

Even me I have the same problem ila kwangu historical background imechangia ila nataka niwe normal hii situation inaniboa msaada wadau

Pole sana mkuu,una puliza moshi kama avatar inavo onesha?
Nahisi inaweza kuwa ina changia pia.
 
...Very good advice

Solution nyingine ni kujipa muda kabla ya kukabili issues. Mfano mtu akikuudhi sana, usimkabili. Ondoka, take a walk ama lala au angalia tv. Kesho utakuwa umeshafikiria vya kutosha. Utakuwa more calm. Inasaidia sana kuamua kuwa huwezi kushughulikia issue ukiwa upset unless ni ugonjwa ama kitu kitacholeta hasara ya pesa.
 
Hua nina hasira sometimes,ila niliambiwa ni kwasababu nilikaa sana
kure ukuryani miaka 15 ya kwanza ya kuishi kwangu,na enzi hizo
tulikua tukienda kuchunga,kwenye kuwinda ndege,sungura,swala,nungu nungu
ilikua ni ubabe mtupu mkinasa,.....sasa hasira za kukatiwa kipande kidogo unakaa nazo mwezi mzima.

Atleast zinapugua siku hizi,kunywa maji ya uvugu vugu,mtegemee Mungu kwa kila jambo.
Ikatae historia mbaya,angalia mbele ambapo kuna tumaini jipya.

Ni ngumu,lakini ingawa sikua kama ulipo,nimeweza kuvuka hali yangu ya kukasirika kwa 90% hadi sasa.
Ingawa hizo 10% zenyewe niki kasirika dah.
 
Sio ndo ataongeza tatizo? Akitokea kupenda timu af matakeo ya hiyo timu yawe sio mazuri .. Akishabikia timu ka yangu ya Liverpool ataishia kuongeza tatizo, ka ana roho nyepesi.

Ha ha ha,ume nikumbusha huyu shabiki wa Yanga.
Au ndo mshkaji?

[video]http://external.ak.fbcdn.net/safe_image.php?d=AQALn2GvleVPu XmX&url=http%3A%2F%2Fvthumb.ak.fbc dn.net%2Fhvthumb-ak-snc6%2Fs403x403%2F246383_10152 164078230531_10152164072850531 _8294_271_b.jpg&jq=100[/video]
 
I have two books, kimoja kinaongelea how to overcome unwanted chronic habits. Nakumbuka nilikinunua moshi cathedral bookshop. Sikumbuki kilipo, nilitaka kukupa author. Kingine kinaonhelea how to manage your phobias. Nilikisoma lakini hakijaweza kuniponya from the fear of death. Siwezi kuaga maiti na nikiona a dead person it will haunt me for months kiasi cha kushindwa kuingia bedroom alone hata mchana. Nimejikubalisha and i dont freak over it. i hang on the beautiful memories inanisaidia nisipate wazimu.
 
Pole sana mkuu,una puliza moshi kama avatar inavo onesha?
Nahisi inaweza kuwa ina changia pia.

Nina muda Sasa since nimeacha CHA Arusha Mimi source ya Kuwa hivyo naijua issue ni how to overcome the anger problem, sometime na overreact on very minor issues
 
Wanajamii kuna tatizo ambalo linasumbua muda mrefu, ambalo ni kuwa na hasira sana. Hii imenipelekea niwe mwingi wa lawama hata pasipo na msingi. sina simile hata kidogo imepelekea my wife aishi maisha ya kukereka sana, hii inanikosesha raha sana imenibidi niwe mtu pombe ili kupunguza Stress. tatizo nimekua nalo toka utotoni. Naomba kama mtu anaeweza nisaidia kuondokana na Hili tatizo.

Ukiendelea na hiyo tatizo lako halitaisha.
 
Pole sana ndugu
tatizo hilo kweli ni kubwa na lina kera sana japo kwa afrika hatulipagi uzito unaostahili
pili nikupe pongezi kwa kutambua kuwa ni tatizo, na kuwa tayari kulitatua ama kuondokana nalo
moja wapo ya jinsi ya kulitatua ni kutafuta jambo la kufanya au kufanya jambo unalopenda pale unapohic kuudhika. kwa mfano mimi napenda sana muziki na novel, so nikowa bored au nikizingulia hasa home na ma wife, huwa naingia zangu chumbani then full blast ya muziki wa raggae au rnb. au nikiona siku hiyo hata mziki hauingii, nachukua zangu kitabu nachopenda au nilichowahi kusoma hata kama nakisoma kwa mara ya saba, then natafuta kakivuli murua, nakula zangu novel
njia ya pili ni kufanya mazoezi, trust me! wakati mwingine hasira inatokana na mwili kuwa na nguvu nyingi isiyotumuka (un-burned energy), hivyo kufanya mazoezi; kwanza kutafanya mwili wako uwe poa yaani fit, na pili kuna activate mind sana, just try this, you will tell me
tatu ni kubadili mtazamo tu, think positive. mfano rais lincolin wa marekani aliwahi kupokea barua ikiwa na neno moja tu "stupid", badala ya kukasirika alisema hivi, "nimewahi kupokea barua nyingi sana, lakini zote zilikuwa zinaanza na ujumbe kisha jina la muhusika mwishoni, lakini barua hii ya leo imeanza na jina kisha aliyeandika akasahau kuweka ujumbe" so my ndugu, think positively, hakuna atakaye kuona zoba bali utaonekana mwenye hekima
karibu katika ulimwengu huru wa msongo
 
Inawezekana malezi

au hupendi ukweli
unapenda kuwa in denial...
sasa ukikutana na ukweli unashikwa na hasira

Kweli sipend kosolewa, lakini sio kwamba nakasirika, tatzo nalohisi kwang ni mzaz wangu, ambaye nilikuwa nikikosea unakuwa wimbo miaka nenda rud. Mfano kama niliwahi poteza kitu labda miaka ya tisin, siku ananiagiza kitu lazima achomekee na hicho kitu. Pili mzaz wangu hajawahi accept opinion zangu hata ziko sawa, Kwa hiyo nimejikuta nazikuza bila kuelimishwa mambo ya msingi mfano. Jinsi ku-behave mbele za watu, jinsi ya Kumhudumia mke wangu, haya yote nimefundishwa na marafiki zang na watu baki. Kwa hiyo nimekua huku nikiwa nakinyongo ndani yangu. Lakin pia alinipenda sana. Tatizo liko hAkuwah kuwa karib nami na kusikiliza yanayonisbu hata leo nikiomba mwambia ntaendelea pingwa. Nachoombea msaada ni kuzitoa hasira tu ambazo huwa zinasumbua.
 
me nafikiri tatizo la kukasirika hutokana na historia ya maisha aliyokulia/pitia mtu, so namshauri atafute washauri nasaha aseme nao!
 
Nakupongeza kwa kujikubari jinsi ulivyo,pili muombe mpenzi wako akubali tatizo ulilo nalo,Muhimu mkabidhi Mungu udhaifu wako huo ulionao..omba jitahidi kuingia kwenye vikundi vya maombi mshirikishe na mkeo pia shida uliyo nayo..Pombe siyo solution la tatizo lako ulilo nalo..Mtu mwenye hasira mara kwa mara ni ngumu pia kuweka husiano mzuri na wengine na mara nyingi maamuzi yake ya mwisho huwa ni mabaya zaidi hata kufikia kuua kwa kosa hata dogo

aksante. Lakini nahisi anaumia sana ndani ya nafsi yake, ingawa anavumilia
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom