TASAF walamba TZS383bn

TASAF walamba TZS383bn

Mshindi wa Vita

JF-Expert Member
Joined
Mar 5, 2025
Posts
260
Reaction score
98
TZS383bn za Rais Samia zatunisha mfuko TASAF

Rais Samia ameongeza kiwango cha fedha kwa ajili ya kunusuru kaya masikini kutoka TZS580.2bn mwaka 2020 hadi TZS962bn mwaka 2024 ikiwa ni ruzuku ikilenga kuongeza kipato cha kaya masikini ili ziweze kumudu gharama za maisha na mahitaji ya msingi. Kupitia Mpango huu wa kunusuru Kaya Masikini (TASAF) idadi ya wanafuika imeongezeka kutoka 5,000,000 hadi 5,202,655 mwaka 2024 sawa na ongezeko la wanufaika wapya 202,655

HATIMAYE WASIOJIWEZA WALAMBA TZS383BN ZA SAMIA
 
Hua nikisikiaga mambo yanayohusu tasaf hua naskia kulia ama kinyaa...kutamka hayo mabilioni raha sana ...ila nasema leo hakuna watu watakufa vifo vibaya kama wanaofanya kazi tasaf ...
Kaya maskin hizo unakuta kaya Moja unawapa laki 1 ama elfu 30 kwa mwaka sjui ..Sasa ikifika wakat hela zimetoka mtu alifanyiwa tathmini apewe 40,000/- , siku ya malipo na Hali yake ngumu Anatoka Kijijini mbali kabisa anakuja mjini benki kuchukua just elfu 40 , ajabu unakuta Kuna elfu 20 tu, wamepiga panga 20, Sasa wangap wanafanyiwa hivyo ..hii nchi Kuna watu watakufa midomo wazi
 
Deni la taifa linaonyesha Kila mtanzania anadaiwa million 8 umefikia wapi kulipa deni lako?
 
Kuna Babu Mmoja analipwa elf Kumi na mbili mia Tano (12500) Kwa mwezi
 
TZS383bn za Rais Samia zatunisha mfuko TASAF

Rais Samia ameongeza kiwango cha fedha kwa ajili ya kunusuru kaya masikini kutoka TZS580.2bn mwaka 2020 hadi TZS962bn mwaka 2024 ikiwa ni ruzuku ikilenga kuongeza kipato cha kaya masikini ili ziweze kumudu gharama za maisha na mahitaji ya msingi. Kupitia Mpango huu wa kunusuru Kaya Masikini (TASAF) idadi ya wanafuika imeongezeka kutoka 5,000,000 hadi 5,202,655 mwaka 2024 sawa na ongezeko la wanufaika wapya 202,655

HATIMAYE WASIOJIWEZA WALAMBA TZS383BN ZA SAMIA
Waneemeke wasiojiweza na isiwe hongo ya uchaguzi.
 
watu wanajipigia tu imagine kuna mwamba kajenga hadi gest kupitia pesa za walala hoi
Inauma sana mzee kumbe na wewe unawafahamu ...Hao nasema watakufa midomo wazi...wazee familia maskin wanachukuliwa sana pesa zao hizo..na watu wametajirikia kupitia wazee hao waliochoka na kaya maskin ....
 
  • Thanks
Reactions: Sax
Kuna Babu Mmoja analipwa elf Kumi na mbili mia Tano (12500) Kwa mwezi
Na unakuta labda alitakiwa alipwe laki Moja..nyingine 90 imepigwa panga na wale majamaa ....nimeshakutana na hao wazee hua nawaonea huruma sana sana ...hii nchi ni laana tupu
 
Huo mpango badala ya kuwasaidia kaya maskini umezidi kuwadidimiza na kunufaisha hao wanaogawa hizo fedha
 
Ufuatiliaji na uwajibikaji sifuri.
Zinaliwa na wenye dhiki ya Mbwa.
 
Km namuona mzee fulani, atakavyomalizia ile mansion yake,
Na wale mapacha wa mchepuko awapeleke huko 🇮🇳 wakasome Udaktari.

Watu wanakula pesaa bhanaa. Lol
 
Ivi si wafanye research waone kama hizi hela zina Tija.
Sasa kumpa mtu mwenye watoto 6 elf 70 kwa mwez inasaidia nini.
Izo hela si bora wajenge barabara
 
Back
Top Bottom