Tarime kuna tatizo na tatizo si CHADEMA, ni Barrick

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,011
Tarime kuna tatizo na tatizo si CHADEMA, ni Barrick

Lula wa Ndali-Mwananzela
RAIA MWEMA
Mei 25, 2011

TATIZO la Tarime si CHADEMA. Naam, lipo tatizo Tarime na ni tatizo la muda mrefu sana kwa yeyote mwenye kufuatilia historia ya eneo hilo. CHADEMA na CCM wanafunua tatizo ambalo lipo hapo, na kwa kadri ya kwamba watu wanafikiria tatizo hili ni la kisiasa ndivyo ambavyo tatizo hili litaendelea kuchukua mwanga wa kisiasa.

Tatizo la CHADEMA linahusiana kwanza kabisa na raslimali za watu. Huwezi kuwa na matajiri wanaonufaika na raslimali; huku wakiwa wamezungukwa na maskini ambao wanashindwa kupata nafasi ya kutumia raslimali hizo.

Kwa muda mrefu kumekuwa na matatizo kuanzia ya kutumia maji ya mto na sasa zaidi kutumia ardhi kama sehemu ya kujipatia maisha yao. Wananchi wa Tarime wanajikuta wanasukumizwa pembezoni mwa mafanikio.

Mgongano kati ya wachimba madini wadogowadogo na kampuni kubwa ya madini ya Barrick haujaanza leo na haujaanzia Tanzania tu. Kuna kitu ambacho hakiko sawa kati ya mahusiano kati ya kampuni hiyo ya Canada na wananchi ambao wanaishi karibu na machimbo yake.

Mapema mwaka huu, Barrick wamejikuta kwenye matatizo huko Papua New Guinea na tayari walishakuwa na migogoro huko Chile na hata Marekani kwenyewe. Matatizo haya yanahitaji kuangaliwa kwa karibu; kwani bila kuyashughulikia mgongano huu utaendelea na siyo Tarime peke yake lakini sehemu nyingine nchini.

Maafa yaliyotokea hayakupaswa kutokea na tusipoangalia yataaendelea kujitokeza tena na tena. Jambo ambalo linaonekana ni la hatari zaidi ni kuwa kuna kasumba ya kuwaona Watanzania ni waleta matatizo na katika jitihada ya kuwafurahisha wawekezaji, basi, tuko tayari kufanya lolote kwa hawa Watanzania wenzetu ili “wawekezaji wasije wakasita kuwekeza nchini”.

Kwa sababu hiyo, juhudi kubwa inatumiwa na vyombo vya dola na hata viongozi wa kitaifa kuhakikisha kuwa mikataba ya madini ina vipengele vinavyoweka jukumu la serikali ‘kushughulikia’ wananchi wake ili wachimbaji wafanye kazi kwa amani.

Matokeo yake ni kuwa mahali popote ambapo madini yatagunduliwa na leseni kutolewa kwa kampuni ya kimataifa, serikali itatakiwa kufanya lolote linalowezekana kuwaondoa wananchi pale ili makampuni hayo yafanikiwe.

Kwa kufanya hivyo, japo jambo hilo linaonekana ni dogo lakini halizingatii hisia za watu kwenye ardhi “yao”. Watanzania kama binadamu wengine wanaamini wana haki katika ardhi yao; kwani ndio mahali pekee katika sayari hii ya dunia ambapo kwa haki kabisa wanapaswa kupata maisha yao.

Hatari yake ni kuwa Serikali ya CCM inaendeleza hizi fikra za kuwafurahisha wageni dhidi ya wananchi. Kuanzia kashfa ya kwanza ya Loliondo, Yaeda Chini, Bulyanhulu, Tarime, Buzwagi na hata Geita huko tayari wananchi wameanza kuona mwendelezo wa tabia ya kuwaona wananchi kama wanaingilia “eneo la wawekezaji”.

Yaani wananchi walioishi katika maeneo fulani kwa miaka na miaka leo wanaambiwa eneo hili ambalo lina utajiri wa dhahabu limeuzwa. Matokeo yake ni kuwa wananchi wanaona kuwa raslimali zao ambazo ni urithi wao unachukuliwa kama zawadi kwa wageni.

Kwa mfano, habari zilizoandikwa na gazeti hili wiki iliyopita kuhusu kusafirishwa kwa nyara za serikali usiku wa manane kunawakumbusha Watanzania habari kama hizo wakati fulani ambapo vitu kama hivyo vilijulikana au pale ambapo wawindaji wa kimataifa waliruhusiwa kuua wanyama wetu na wakati mwingine kuondoka na wengine ili wakapambe bustani zao huko Mashariki ya Kati.

Watanzania hawa wafanye nini wanapoona urithi wao unauzwa kwa wageni kama njugu kwa kisingizio cha “kuvutia wawekezaji”?

Hapa ndipo mgongano wa kifikra unapotokea sasa ambapo viongozi wa serikali na hasa vyombo vya dola vikitekeleza sera ya uwekezaji ya CCM vinapogongana na eneo ambalo lina viongozi wa Upinzani ambao sera yao ni kulinda maslahi na raslimali za taifa ili ziweze kutumika vizuri kuinua maisha yao. Hivyo, mgongano wa Tarime ni zaidi ya raslimali; kwani pia unahusisha utu wa wananchi wenyewe.

Wananchi hawawezi kujihisi kuwa ni wageni katika taifa lao na hasa yanapotokea mauaji. Kuna mtu katika Jeshi la Polisi ambaye hajui kuzuia maandamano au vurugu bila kuanza kumwaga risasi. Tumeliona Arusha mapema mwaka huu, na tumeshawahi kuliona huko nyuma huko huko Tarime.

Pamoja na kufanya Tarime kuwa mkoa maalumu wa Polisi, ni wazi kuwa juhudi za kuleta amani na utulivu zimeshindikana; kwani dhana ambayo inaongoza ina makosa.

Huwezi kuleta amani kwa kuleta polisi wengi, au kwa kuua watu wengi zaidi. Jamani, hili somo kwanini ni gumu hivyo wenzetu kulielewa? Kama ingekuwa rahisi hivyo, Assad wa Syria angekuwa anakula kuku kwa mrija tu baada ya kuua wananchi wake 700!

Kama kuua wananchi wanaopinga serikali au kupigania haki yao ingekuwa inatosha kuwanyamazisha, mauaji ya Sharpeville na yale ya Soweto yangeweza kuwafanya watu wa Afrika Kusini kukubali ubaguzi. Risasi hazijawahi kuzuia fikra za utu na kudai uhuru popote pale duniani.

Isitoshe, Serikali ya Tanzania haina risasi za kutosha kuwamaliza Watanzania wote wanaopinga uovu na maonevu. Serikali inakuwa kama kikolezo tu cha kizazi kingine.

Jamani; kama risasi zingewatisha watu, basi, baada ya mauaji yale ya Arusha wasingejitokeza tena watu kuandamana. Na naomba niwe mbebaji wa habari mbaya kwa watawala – kwa kadri wanavyozidi kumwaga damu ya Watanzania ndivyo wanavyowafanya Watanzania kuanza kuona kuwa hawana cha kupoteza isipokuwa utu wao.


Na habari kuwa Mbunge wa Singida Mashariki na mwanaharakati ambaye anajua sana siasa za Tarime, Tundu Lissu kuwa aliwekwa ndani pamoja na wenzake; huku polisi wakizingira mochwari ambapo miili ya wana Tarime ilikuwa imehifadhiwa kusubiri ibada, zinashtua. Kumfunga Lissu au kuwafunga wale wote watakaokuja Tarime hakutoshi kuzuia fikra za mabadiliko, na serikali isipokuwa makini katika hili, amani inaweza kuvunjika zaidi Tarime.

Nawasihi sana watawala wetu na viongozi wetu wa kisiasa kukaa chini mara moja na kuzuia kulipuka kwa jambo hili kwa kutumia hekima zaidi kuliko kutumia nguvu. Risasi hazitazuia hili, jela hazijawahi kufunga fikra huru.

Ni mazungumzo tu yanayoweza kutuliza mambo. Na hapa naamini watu wa Barrick wana maswali ya kujibu; kwani tukianza kufuatilia na kuangalia mahusiano yao na vyombo vya dola na wananchi, tutaona jinsi gani kuna kitu hakiko sahihi.

Vinginevyo, Barrick ifunge mgodi huo na kuondoka; kwani uwepo wake haustahili kifo cha Mtanzania hata mmoja. Jamani, hizo dhahabu hazitaoza lakini katika umaskini wetu tusiwe tayari hata kuuza utu wetu.

Kama uwepo wa migodi hii unatufanya tuuane na kufungana na kupigana virungu, basi haitustahili. Tutumie hekima lakini kama hakuna wenye hekima kati yetu, tufunge mgodi ili watu wa Tarime watafute mambo mengine ya kufanya. Hatuwezi kukaa kama taifa katika hali ya wasiwasi wa kudumu.
 
Migodi haichochei maendeleo kwa kutoa misaada. Jo'burg, Perth, Adelaide haikufika hatua ya maendeleo iliyo nayo eti kwa sababu migodi ilikuwa inatoa misaada kwa halmashauri za miji hiyo.

Kama Tanzania tunataka kuneemeka na madini yetu, shurti tujizatiti kama ifuatavyo;

1. Tujielimishe katika fani za jiologjia na uhandisi wa migodi ili tupate kazi za maana kwenye migodi

2. Wananchi wasio na elimu wajitahidi basi kuomba hata kazi za ulinzi ndani ya hiyo migodi. Ajira rasmi ya mtu mmoja inaweza ikasapoti mpaka wategemezi 20

3. Tujitahidi kuzalisha bidhaa bora na kuuza kwenye migodi; k.m. vyakula, usafiri wa wafanyakazi, mali ghafi kama potash

4. Tuwauzie umeme - Hapa itabidi tuongeze uzalishaji kwa kuvuna Steigler's Gorge, Kiwira Coal Power, Malagarasi HEP n.k.

Kwa hitimisho, Watanzania tuache hii tabia ya kujikalia tu na kutegemea kuwa alimradi nchi yetu ina dhahabu, basi ni stahili yangu kufaidika nayo. Ukitaka kufaidika na hiyo dhahabu, shurti ujihusishe katika mlolongo wa dhawabu (value chain) ya kuzalisha hiyo dhahabu.
 
Migodi haichochei maendeleo kwa kutoa misaada. Jo'burg, Perth, Adelaide haikufika hatua ya maendeleo iliyo nayo eti kwa sababu migodi ilikuwa inatoa misaada kwa halmashauri za miji hiyo.

Kama Tanzania tunataka kuneemeka na madini yetu, shurti tujizatiti kama ifuatavyo;

1. Tujielimishe katika fani za jiologjia na uhandisi wa migodi ili tupate kazi za maana kwenye migodi

2. Wananchi wasio na elimu wajitahidi basi kuomba hata kazi za ulinzi ndani ya hiyo migodi. Ajira rasmi ya mtu mmoja inaweza ikasapoti mpaka wategemezi 20

3. Tujitahidi kuzalisha bidhaa bora na kuuza kwenye migodi; k.m. vyakula, usafiri wa wafanyakazi, mali ghafi kama potash

4. Tuwauzie umeme - Hapa itabidi tuongeze uzalishaji kwa kuvuna Steigler's Gorge, Kiwira Coal Power, Malagarasi HEP n.k.

Kwa hitimisho, Watanzania tuache hii tabia ya kujikalia tu na kutegemea kuwa alimradi nchi yetu ina dhahabu, basi ni stahili yangu kufaidika nayo. Ukitaka kufaidika na hiyo dhahabu, shurti ujihusishe katika mlolongo wa dhawabu (value chain) ya kuzalisha hiyo dhahabu.

Wewe ni Punda mwenye magamba!

Tatizo letu ni tofauti na kwingineko huko ulikotaja....huko migodi ilichangia moja kwa moja kwenye uchumi, tena kwa kiasi kikubwa. Sisi tuliwapa offer ya kuchimba wakajilie kwao. Ndio maana wananch wana hasira.

Huwa napata taabu sana na watz wanaotetea huu uwekezaji kwenye madini....tuliuzwa..period!. Uchimbaji wa madini serikali yetu ilitakiwa iwe ina share za kutosha sisizo pungua 45%...mali ile ni yetu...huwezi ukampa mtu akachimba kwa kumililki 100%...only in Tanzania!

Angalia mikataba ya Mafuta na gesi inayoingiwa na TPDC kwa niaba ya serikali....government ownership is significant...na huwezi kulinganisha ugumu wa utafutaji mafuta & gesi na madini...madini ni rahisi mno.

Na alaaniwe Benjamin William Mkapa kwa kulisaliti taifa.
 
Tatizo la baadhi yetu ni kushindwa kuikubali dhana kwamba viongozi wetu wanatuzidi akili kwa mbali saaaana na kwa hiyo kila kitu wanachokiamua ni chema kabisa....Hawatakiwa kuhojiwa kwa lolote. Bora sie wengine tulishaacha kihere here na wivu wa kike...Tumejikalia na kusubiri kujifia kama dagaa wanaosubiri kuvuliwa kwa kokoro!!

Laiti wajukuu zetu wangepata lift ya kutembelea sayari nyingine ili wakirudi wasiwe tu na magamba bali vichwa hivi vya panzi!!
 
Kuna mtafiti mmoja alisema uchimbaji huu ukiendelea hivi kwa miaka 20, basi madini yetu yatakuwa yamepungua kwa zaidi ya asilia 90 au yameisha kabisa. Huwezi tu kusema eti madini hayaozi tuwaache wachimbe. Mwalimu nyerere alishawahi kusema kama haya madini hayana faida kwa Watanzania ni bora yaendelee kubaki huko ardhini kuliko kunufaisha maghachori. Watawala wenye uchu walivyokuja ndio mtindo wa kukwapua ukaanza!! Mutuachie madini yetu. Hata kama Barrick wanalipa vizuri wafanyakazi nina wasiwasi kwamba profit yao ni uncomparable na za hawa wafanyakazi.

Mi wasiwasi wangu mkubwa ni kuhusu Mafuta na Gesi inayopatikana Mtwara(Mnazi Bay). Kwawatawala kama hawa CCM wakiendelea, hayo mafuta na wakazi wa kule kusini sidhani kama watanufaika nayo. Na mauaji haya tunayoyashuhudia Tarime basi yatahamia Mkoa wa Mtwara pindi wakianza biashara hiyo rasmi. Tuseme NO kwa Serikali na Polisi wake.
 
Migodi haichochei maendeleo kwa kutoa misaada. Jo'burg, Perth, Adelaide haikufika hatua ya maendeleo iliyo nayo eti kwa sababu migodi ilikuwa inatoa misaada kwa halmashauri za miji hiyo.

Kama Tanzania tunataka kuneemeka na madini yetu, shurti tujizatiti kama ifuatavyo;

1. Tujielimishe katika fani za jiologjia na uhandisi wa migodi ili tupate kazi za maana kwenye migodi

2. Wananchi wasio na elimu wajitahidi basi kuomba hata kazi za ulinzi ndani ya hiyo migodi. Ajira rasmi ya mtu mmoja inaweza ikasapoti mpaka wategemezi 20

3. Tujitahidi kuzalisha bidhaa bora na kuuza kwenye migodi; k.m. vyakula, usafiri wa wafanyakazi, mali ghafi kama potash

4. Tuwauzie umeme - Hapa itabidi tuongeze uzalishaji kwa kuvuna Steigler's Gorge, Kiwira Coal Power, Malagarasi HEP n.k.

Kwa hitimisho, Watanzania tuache hii tabia ya kujikalia tu na kutegemea kuwa alimradi nchi yetu ina dhahabu, basi ni stahili yangu kufaidika nayo. Ukitaka kufaidika na hiyo dhahabu, shurti ujihusishe katika mlolongo wa dhawabu (value chain) ya kuzalisha hiyo dhahabu.

Nimekupataq The Stig,
Hata kodi hakuna sababu ya kukusanya, sisi tuwauzie huduma
Hata umiliki (share) hatuna sababu za kuwa nao sisi tusome tupate ajira.
Hata mining audit haihitajiki nkufanyika, sisi tujikite kuzalisha bidhaa bora ili tuwauzie
Tujitahidi kuzalisha umeme kwa wingi ili tuwauzie, hizo ni sera maridhawa za chama chetu magamba....
 
Migodi haichochei maendeleo kwa kutoa misaada. Jo'burg, Perth, Adelaide haikufika hatua ya maendeleo iliyo nayo eti kwa sababu migodi ilikuwa inatoa misaada kwa halmashauri za miji hiyo.

Kama Tanzania tunataka kuneemeka na madini yetu, shurti tujizatiti kama ifuatavyo;

1. Tujielimishe katika fani za jiologjia na uhandisi wa migodi ili tupate kazi za maana kwenye migodi

2. Wananchi wasio na elimu wajitahidi basi kuomba hata kazi za ulinzi ndani ya hiyo migodi. Ajira rasmi ya mtu mmoja inaweza ikasapoti mpaka wategemezi 20

3. Tujitahidi kuzalisha bidhaa bora na kuuza kwenye migodi; k.m. vyakula, usafiri wa wafanyakazi, mali ghafi kama potash

4. Tuwauzie umeme - Hapa itabidi tuongeze uzalishaji kwa kuvuna Steigler's Gorge, Kiwira Coal Power, Malagarasi HEP n.k.

Kwa hitimisho, Watanzania tuache hii tabia ya kujikalia tu na kutegemea kuwa alimradi nchi yetu ina dhahabu, basi ni stahili yangu kufaidika nayo. Ukitaka kufaidika na hiyo dhahabu, shurti ujihusishe katika mlolongo wa dhawabu (value chain) ya kuzalisha hiyo dhahabu.
Nani aliyetaka migodi itoe misaada?! Kwako wewe kuchochea maendeleo ni kwa migodi kutumia sumu kuwauwa wakazi wa maeneo husika na mifugo yao, halafu hakuna yeyote aliyechukuliwa hatua hadi sasa!!!
Na kwa taarifa yako wakazi wa maeneo hayo hawakuwa wamejikalia tu kama unavyokebehi leo... Hao ni watu ambao wamenyang'anywa migodi, mashamba na nyumba zao kwa mabavu, na sasa wananyang'anywa hata utu wao na vibaraka wa watawala na wezi wa kimataifa chini ya mwamvuli wa uwekezaji. Kama alivyosema ndugu mmoja hapo juu, alaaniwe Mkapa na wote walio/wanaoshiriki ktk kutenda uovu huu kwa raia wa Taifa hili.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Migodi haichochei maendeleo kwa kutoa misaada. Jo'burg, Perth, Adelaide haikufika hatua ya maendeleo iliyo nayo eti kwa sababu migodi ilikuwa inatoa misaada kwa halmashauri za miji hiyo.

Kama Tanzania tunataka kuneemeka na madini yetu, shurti tujizatiti kama ifuatavyo;

1. Tujielimishe katika fani za jiologjia na uhandisi wa migodi ili tupate kazi za maana kwenye migodi

2. Wananchi wasio na elimu wajitahidi basi kuomba hata kazi za ulinzi ndani ya hiyo migodi. Ajira rasmi ya mtu mmoja inaweza ikasapoti mpaka wategemezi 20

3. Tujitahidi kuzalisha bidhaa bora na kuuza kwenye migodi; k.m. vyakula, usafiri wa wafanyakazi, mali ghafi kama potash

4. Tuwauzie umeme - Hapa itabidi tuongeze uzalishaji kwa kuvuna Steigler's Gorge, Kiwira Coal Power, Malagarasi HEP n.k.

Kwa hitimisho, Watanzania tuache hii tabia ya kujikalia tu na kutegemea kuwa alimradi nchi yetu ina dhahabu, basi ni stahili yangu kufaidika nayo. Ukitaka kufaidika na hiyo dhahabu, shurti ujihusishe katika mlolongo wa dhawabu (value chain) ya kuzalisha hiyo dhahabu.

The Stig, yana mwisho haya....dont say that you were not warned!!! Kula leo, nikukule kesho!!
 
Ndugu yangu inawezekan hujui kinachoendelea nchi hii, mimi ni mwanaharakati na pia professional mimi ni Geologist mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka nane kwenye hii fani, nimefanya kazi ndani ya nchi na nje ya nchi pia,
1. Tuna vijana wengi tu wamesoma hizo fani ulizotaja na wengine wako nje ya nchi kutafuta maslahi zaidi, hapa tanzania and particular Barrick geologist mtanzania mwenye uzoefu kama mimi mshahara wake ni tsh 2500000 kwa mwezi kabla ya kodi na makato mengine, mzungu mwenye miaka mitano kazini ni manager na analipwa zaidi ya USD 40000 kwa mwezi na akiwa Tanzania kampuni humpatia kila kitu including pocket money ya zaidi ya tsh million moja kwa mwezi, hivyo basi angalia utofauti huo hapa nchini wanawekeza wanavuna na wanalipa vizuri watu wao tu siyo mzawa
2.Kazi za ulinzi migodini zinafanywa na makaburu, waindonesia na wafilipino mzawa ukiomba huaminiki hata kidogo, serikali yetu dhalimu imeshindwa kuzuia bogus expatriate wasiingie nchini saa hizi kuna migodi kama Buzwagi hata fuel attendant ni wazungu muulize ndugu yoyote aliyeko pale.
3. Maziwa, nyama , mchele na hata mboga za majni zinazoliwa mgodini hazinunuliwi Tanzania , zote zinatolewa nje ya nchi , hata ukizalisha huwezi kusupply maan hauko kwenye pronto
4. Ndugu yangu umeshwahi ona watanzania wanavyonyanyasika migodini lakini? au you are just saying, nenda mahakama ya kazi shinyanga ukaangalia kuna kesi ngapi za watanzania ambao wamekuwa terminated unfair, hiyo ni baadhi tu jamani.
Kampuni ya barrick ilishindwa kuchimba kwenye project ya Sedi belo africa ya kusini kwa sababu barrick ni matapeli walimtapeli karamagi na watanzania kwa ujumla, wana matatizo chile, Papua New Guinea na for your information ile trend ya North mara imeingia mpaka jimbo la Nyanza nchini kenya lakini hata kwenda kufanya utafiti huko hawataki na hawawezi kwa sababu ardhi ni mali ya wananchi na si kama kwetu hapa.
Nashangaa hata Barrick kuitwa African Barrick wakati wana project tanzania tu, nchi iliyo na watu waliolala na viongozi dhaifu kuliko hata somalia, nchi inayonyenyekea wezi, wazungu matapeli na wahindi, saa hizi hotel zote za kitalii tanzania , manager mkenya au mhindi, waitress na waiters wote wakenya,watanzania tutafanya kazi zipi
Any way kwa leo naishia hapo ila idara ya uhamiaji iko wapi>???????????????
3.
Migodi haichochei maendeleo kwa kutoa misaada. Jo'burg, Perth, Adelaide haikufika hatua ya maendeleo iliyo nayo eti kwa sababu migodi ilikuwa inatoa misaada kwa halmashauri za miji hiyo.

Kama Tanzania tunataka kuneemeka na madily ni yetu, shurti tujizatiti kama ifuatavyo;

1. Tujielimishe katika fani za jiologjia na uhandisi wa migodi ili tupate kazi za maana kwenye migodi

2. Wananchi wasio na elimu wajitahidi basi kuomba hata kazi za ulinzi ndani ya hiyo migodi. Ajira rasmi ya mtu mmoja inaweza ikasapoti mpaka wategemezi 20

3. Tujitahidi kuzalisha bidhaa bora na kuuza kwenye migodi; k.m. vyakula, usafiri wa wafanyakazi, mali ghafi kama potash

4. Tuwauzie umeme - Hapa itabidi tuongeze uzalishaji kwa kuvuna Steigler's Gorge, Kiwira Coal Power, Malagarasi HEP n.k.

Kwa hitimisho, Watanzania tuache hii tabia ya kujikalia tu na kutegemea kuwa alimradi nchi yetu ina dhahabu, basi ni stahili yangu kufaidika nayo. Ukitaka kufaidika na hiyo dhahabu, shurti ujihusishe katika mlolongo wa dhawabu (value chain) ya kuzalisha hiyo dhahabu.
 
Ndugu yangu inawezekan hujui kinachoendelea nchi hii, mimi ni mwanaharakati na pia professional mimi ni Geologist mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka nane kwenye hii fani, nimefanya kazi ndani ya nchi na nje ya nchi pia,
1. Tuna vijana wengi tu wamesoma hizo fani ulizotaja na wengine wako nje ya nchi kutafuta maslahi zaidi, hapa tanzania and particular Barrick geologist mtanzania mwenye uzoefu kama mimi mshahara wake ni tsh 2500000 kwa mwezi kabla ya kodi na makato mengine, mzungu mwenye miaka mitano kazini ni manager na analipwa zaidi ya USD 40000 kwa mwezi na akiwa Tanzania kampuni humpatia kila kitu including pocket money ya zaidi ya tsh million moja kwa mwezi, hivyo basi angalia utofauti huo hapa nchini wanawekeza wanavuna na wanalipa vizuri watu wao tu siyo mzawa
2.Kazi za ulinzi migodini zinafanywa na makaburu, waindonesia na wafilipino mzawa ukiomba huaminiki hata kidogo, serikali yetu dhalimu imeshindwa kuzuia bogus expatriate wasiingie nchini saa hizi kuna migodi kama Buzwagi hata fuel attendant ni wazungu muulize ndugu yoyote aliyeko pale.
3. Maziwa, nyama , mchele na hata mboga za majni zinazoliwa mgodini hazinunuliwi Tanzania , zote zinatolewa nje ya nchi , hata ukizalisha huwezi kusupply maan hauko kwenye pronto
4. Ndugu yangu umeshwahi ona watanzania wanavyonyanyasika migodini lakini? au you are just saying, nenda mahakama ya kazi shinyanga ukaangalia kuna kesi ngapi za watanzania ambao wamekuwa terminated unfair, hiyo ni baadhi tu jamani.
Kampuni ya barrick ilishindwa kuchimba kwenye project ya Sedi belo africa ya kusini kwa sababu barrick ni matapeli walimtapeli karamagi na watanzania kwa ujumla, wana matatizo chile, Papua New Guinea na for your information ile trend ya North mara imeingia mpaka jimbo la Nyanza nchini kenya lakini hata kwenda kufanya utafiti huko hawataki na hawawezi kwa sababu ardhi ni mali ya wananchi na si kama kwetu hapa.
Nashangaa hata Barrick kuitwa African Barrick wakati wana project tanzania tu, nchi iliyo na watu waliolala na viongozi dhaifu kuliko hata somalia, nchi inayonyenyekea wezi, wazungu matapeli na wahindi, saa hizi hotel zote za kitalii tanzania , manager mkenya au mhindi, waitress na waiters wote wakenya,watanzania tutafanya kazi zipi
Any way kwa leo naishia hapo ila idara ya uhamiaji iko wapi>???????????????
3.

mkuu post yako imenifanya nakaribia kutokwa an machzozi, mimi nilisoma na wazungu na nilikuwa nawapita darasani kama kawaida mzungu huyu huyu kwa vile ngozi yake yeye ni nyeupe anakuja kuajiriwa ajira sawa na mimi ila yeyey anapewa mshahara mkubwa kisa ati yeye ana ngozi nyeupe jamani, hivi ubaguzi utaisha lini jamani, kwanza wazungu wale magenius hawaji africa hata siku koja wanaokuja huku ni wale vilaza , nyie ngojeni mimi nikamate nchi siku moja .
 
Haya maneno yanauma sana. Kama mnakumbuka siku ya mwisho ya kufanya kampeni za mwaka 2010, akiwa anahojiwa na wandishi wa habari kwenye mhadhara. Jk mwenye alisema "wawekezaji wa madini wanatulalia sana tunapata mrahaba wa asilimia 3. Akaendelea kusema tuna mpango wa kuangalia upya mikataba na hawa wawekezaji. Hivi tumekuwa tukiibiwa tangu enzi za Mkapa, Jk ameingia mpaka miaka 5 imeisha ameshindwa kugundua na kuzuia huo wizi na mpaka sasa hivi hakuna jipya. Bulyanhulu watu wanafukiwa na vifusi Underground hakuna anaeweza kuhoji. Nyamongo mgodi ulimwaga sumu kwenye mto na kudhuru wananchi, hakuna aliye wajibika na waliodhulika hakuna aliye lipwa au kupewa fidia yeyote. Jamani hivi uonevu kama huu mpaka lini. Serikali inataka yote haya yaendelee na asiwepo mtu,chama,taasisi au kikundi flani kuingilia mambo haya. Yaani tuna viongozi wa ajabu sana. Tungekuwa na serikali iliyo makini tungegawana kinachopatika kwa proportinality ambayo ingeweza kusaidia maendelo ya jamii hasa maeneo yenye migodi, lakini serikali yetu wanakula viongozi, wazawa wa maeneo yanayochimbwa dhahabu wamesahaulika. Wananchi wakiwa kimya wanazidi kuliwa. Inabidi wadai haki yao wenyewe manake serikali haiwapiganii.
 
"Matokeo yake ni kuwa mahali popote ambapo madini yatagunduliwa na leseni kutolewa kwa kampuni ya kimataifa, serikali itatakiwa kufanya lolote linalowezekana kuwaondoa wananchi pale ili makampuni hayo yafanikiwe. "
Guys, naamini kabisa kosa lipo kwenye quote hapo juu. Chanzo cha hili tatizo ni compensation ya wazawa. Natumani kama wazawa wangepewa compnsation inayostahili, wasingeleta fujo hivi. Vile vile Barrick ni kampuni yenye uwezo wa kulipa compensation sahihi. Hata pale walipo contaminate maji, walipaswa kuliwalipa waathirika fidia inayostahili. Tatizo kama hili lipo sana kwa wazawa na wawekezaji wakubwa wa kilimo na madini. Kuna wawekezaji wengi wameingizwa mitini na "watendaji" wanaotoa leseni na hati miliki. Hawa watendaji or middlemen ndio chanzo kikuu cha haya matatizo. Hawawakilishi maslahi ya wananchi. Tena wengi wao utoa compensation kidogo sana or nothing at all na kutumia mabavu ya sheria uchwara kuwatoa wazawa sehemu hiyo. Ndio hawa hawa middlemen wanahonga serikalini na kudanganya ili wapate hizo leseni na hati kwa mwekezaji. At the end, wananchi wanamvamia mwekezaji. Kuna wawekezaji wengine wametumia zaidi ya $10mil kwenye shamba lakini maisha yao yakawa hatarini na mbunge aliyewasaidia kupata hilo shamba akawageuka. Ilikuwa wakati wa kampeni. Wawekezaji wa watu wamefuata sheria kudai haki yao mwishoe wakafunga virago na kuondoka. Hii si picha nzuri kwa nchi yetu. Victims ni both wawekezaji na wazawa. Lazima serikali iweke bayana sheria za kulinda haki za wananchi na wawekezaji ile wa-coexist in harmony.
 
Haya maneno yanauma sana. Kama mnakumbuka siku ya mwisho ya kufanya kampeni za mwaka 2010, akiwa anahojiwa na wandishi wa habari kwenye mhadhara. Jk mwenye alisema "wawekezaji wa madini wanatulalia sana tunapata mrahaba wa asilimia 3. Akaendelea kusema tuna mpango wa kuangalia upya mikataba na hawa wawekezaji. Hivi tumekuwa tukiibiwa tangu enzi za Mkapa, Jk ameingia mpaka miaka 5 imeisha ameshindwa kugundua na kuzuia huo wizi na mpaka sasa hivi hakuna jipya. Bulyanhulu watu wanafukiwa na vifusi Underground hakuna anaeweza kuhoji. Nyamongo mgodi ulimwaga sumu kwenye mto na kudhuru wananchi, hakuna aliye wajibika na waliodhulika hakuna aliye lipwa au kupewa fidia yeyote. Jamani hivi uonevu kama huu mpaka lini. Serikali inataka yote haya yaendelee na asiwepo mtu,chama,taasisi au kikundi flani kuingilia mambo haya. Yaani tuna viongozi wa ajabu sana. Tungekuwa na serikali iliyo makini tungegawana kinachopatika kwa proportinality ambayo ingeweza kusaidia maendelo ya jamii hasa maeneo yenye migodi, lakini serikali yetu wanakula viongozi, wazawa wa maeneo yanayochimbwa dhahabu wamesahaulika. Wananchi wakiwa kimya wanazidi kuliwa. Inabidi wadai haki yao wenyewe manake serikali haiwapiganii.
Hiyo ya kuangalia upya mikataba Kikwete ameisema tangu 2005 alipokuja na kaulimbiu win-win solution. Lakini tusisahau kuwa yeye ndiye anayejisifia kukata mbuga kuwatafuta akina Sinclair na mikataba kaisaini yeye. Sasa huyu huyu mchawi wetu anawezaje kugeuka kuwa tumaini letu? Haiwezekani. Mpaka tutakapopata serikali mpya nje ya CCM tutaendelea kuliwa na Barrick na kunyanyaswa na wawekezaji katika nchi yetu wenyewe.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
gam-masthead-red.png
web-tanz-barric_1280996cl-3.jpg

78614290-canadian-miner.jpg

Canadian miner Barrick Gold said it had struck a deal to buy Equinox Minerals

GEOFFREY YORK

NORTH MARA, TANZANIA- From Tuesday's Globe and Mail

Published Monday, May. 30, 2011 10:51PM EDT

Last updated Tuesday, May. 31, 2011 5:18AM EDT

Just two weeks after the fatal shooting of seven people at one of its Tanzanian gold mines, Barrick Gold Corp. is investigating allegations of sexual assault by about a dozen police and security guards at the same violence-plagued mine.

The Toronto-based corporate giant, the world's biggest gold miner, is already reeling from allegations of gang rape by its security guards at another of its subsidiaries, in Papua New Guinea.
The deaths and alleged abuses at the Barrick sites, which began years ago but failed to gain wide attention until recently, are accelerating Barrick's efforts to introduce stronger rules for investigating human-rights problems at its 26 mines around the world. The latest case comes as investors have been urging Canadian companies operating overseas in tough and lawless environments to push for more transparency instead of tolerating human-rights abuses.
Barrick recently became the first Canadian mining company to sign up to the Voluntary Principles on Security and Human Rights, an international set of guidelines for extractive industries, which oblige it to investigate and report any credible information about human-rights abuses at its workplaces.

At Barrick's controversial North Mara gold mine in Tanzania, investigators have interviewed about 10 women who allege that they were arrested at the mine site and sexually assaulted by company security guards or Tanzanian police over the past several years.

The allegations were discovered in the course of a review into a separate human-rights issue at the mine. A preliminary investigation by Barrick's subsidiary, African Barrick Gold, found that the allegations were credible.

African Barrick has sent in a team of independent investigators, headed by a former Australian police detective, to gather evidence in the case. The company has also given the evidence to the Tanzanian police, who have promised their own high-level investigation. The company says it is insisting on a full police investigation.

In most or all of the cases, the women told the investigators that they were taken to holding cells and coerced into sex by police and security guards, who threatened them with imprisonment if they refused.

In a statement to The Globe and Mail yesterday, Barrick said the allegations were "highly disturbing" and will be fully investigated and publicly reported. It also pledged to dismiss any employee involved in human-rights violations, or any employee who has knowledge of human-rights abuses and fails to report them.

"Barrick is deeply distressed by the evidence that has emerged," the company said.

"These deplorable crimes, if confirmed, are neither acceptable nor excusable. They send a clear message to us that we have not met the promises we have made to the community, and to ourselves, to pursue responsible mining in every location where we and our affiliates operate. We can, and will, do more."

For years, thousands of impoverished villagers around North Mara have routinely invaded the mine to grab rocks from its waste heaps, which can be processed into tiny bits of gold. There are daily confrontations between the invaders and the mine's security guards, usually reinforced by Tanzanian police.

On May 16, when an estimated 1,500 people invaded the mine, police opened fire and killed seven of them, according to a statement by Barrick. Twelve others were injured by the police gunfire. Police commanders have insisted that the police were acting in self-defence.

In previous clashes at North Mara over the past several years, at least seven other people – and perhaps many more – have been shot dead by police, according to Tanzanian media and other reports. Witnesses say the invaders are generally unarmed, although some carry hammers to break up the waste rocks and some throw stones at security vehicles when the guards try to disperse them.

In the remote highlands of Papua New Guinea, where Barrick owns 95 per cent of the Porgera gold mine, a report by Human Rights Watch this year concluded that the mine's private security force is implicated in "a pattern of violent abuses, including horrifying acts of gang rape."

The report documented five alleged incidents of gang rape by mine security personnel in 2009 and 2010, and a sixth case in 2008. One woman said she was gang raped by six guards after one of them kicked her in the face and shattered her teeth. Another said she and three other women were raped by 10 security guards, who forced her to swallow a used condom.

After it was contacted by the human-rights group, Barrick launched a series of investigations and eventually acknowledged there was "disturbing" evidence of abuses by some of its security personnel. It dismissed a number of employees, including some who knew of the misconduct and failed to report it. It also requested a police investigation, which led to a number of arrests.
 
Yeah ni vya kushangaza kweli; Serikali yetu inakadiri kumlinda Mwekezaji kuliko Mwananchi Wake...

Prejudice, not being founded on reason, cannot be removed by argument
 
Back
Top Bottom