Tapeli yamtokea puani, tumbo lajaa maji

Tapeli yamtokea puani, tumbo lajaa maji

Kweli hii ni janja ya kunasa watu iweje aweke na namba ya simu hapo
 
😁 😁 😁 😁 😁 😁 😁 😁 iyo vocha ya laki siitaki atume muhamala
 
Wale matapeli mje mjifunze kwa mwenzenu yamemkuta ya kumkuta na wewe ulie fanya hii msaidie mwenzio acha roho mbaya..
Za mwizi ni 40 hatimayeView attachment 1217126
Kitu kama hiki kimetokea kama wiki imepita pale mbezi kwa msuguli.

Nilikuwa natoka zangu mbezi Mwisho naelekea ubungo, nafika pale mbezi kwa msuguli naona pembezoni mwa road kuna dogo anafinywa, anachezea kichapo. Kwa haraka haraka alionekana hazidi miaka 20, ni kadogo mno hadi muonekano.

Ikabidi nikatoka road, nikasogea. Sasa ile nashuka naona naratibu watu wanasogea zaidi na silaha walizozipata kwa urahisi, mwenye jiwe, fimbo, tairi na wengine wakigeuka Tyson. Nilicho waza ni kumchomoa kwanza ili nisikie nin chaendelea, maana raia unaweza kuta wanaua hata mtu bila hatia kisa, hata kasingiziwa mwizi na binti waliye kwazana tu.

Ikabidi nami nikajiunga kumsukum sukuma dogo, na kumpiga kofi za mgongoni, kumshtua tu pia raia wasiweke upinzani wa awali namimi. Vuta mkanda kijana wa huyo dogo nikamweka, biti kidogo kwa washkaj wale boda boda watulie.

Haikiwa rahisi kama mwalimu wa darasa kuwatuliza watoto wa shule ya msingi. Lakini shukrana iliwezekana. Story ilivyoenda dogo ni kweli aliiba tigo pesa, alifanya utapeli kwa kuelekezwa na watu walikuwa wamepaki pembeni na gari, baada ya tukion kunuka, wale wakakimbia na gari.

Kufupisha hadithi dogo nilimtoa hapo, lakini kubwa zaidi watu wawe makini mno, wizi wa tigopesa bado upo, mbinu nyingi lakini ya kijinga zaidi ambayo unaweza kujinasua nayo ni kuwa usitume pesa bila kupewa pesa kwanza.

Maana dogo alipoona mbinu elekezi zimegoma ndio akaomba awekew fedha, ilipowekwa akajifnaya amesahau kwenye iliyopaki, wale wa gari walipo wekewa hela waka washa gari kumsubili dogo kwa mbele, ndipo alipodakwa sasa na wadau.
 
Mleta uzi hautupati..Najua umetega ili watu waje wasaidiwe kuwakomesha wezi wao ....Tumestuka
 
Aliyemfanyia hivyo amefanya padogo Sana, angevimbisha na kichwa akitembea ajihisi Kama kabeba kontena.
 
Huu uzi ni utapeli mpya tuwe makini waungwana.
Naaam, ukiingia kingi tu umeliwa, mara nyengine matapeli hutumia njia mfano wa hii sasa kama wewe ushapigwa na bado una kiwewe hasira na mawenge ya kupigwa ni lazma uingie pm kuanza kuulizia aliye mjaza maji huyo tapeli anapatikana wapi ili nawe ukamchome sindano aliyekutapeli, kumbe unakwenda kumalizwa na tapeli mwengine.
Kaa mbali ukishaumizwa, jigange majeraha yako, jipange upya anza upya tayari ushapatata somo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom