figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,895
Mwenyekiti wa Umoja wa Jumuia ya Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa wa Dodoma, Salome Kiwaya amefariki dunia kufuatia ajali iliyohusisha magari matatu leo mkoani Dodoma.
Pia alikuwa Mwandaaji wa Miss Dodoma na Kanda ya Kati. Ikumbukwe ndiye aliyemtoa Miss Tanzania 1995, Emilly Adolf. R.I.P Mama Kiwaya
Ajali hii imetokea leo katika eneo la Emaus, Mkoani Dodoma ambapo imehusisha gari kubwa mbili na moja dogo aina ya Toyota Noah. Inadaiwa kuwa Mtu mmoja amepoteza maisha na wengine kadhaa kujeruhiwa. Chanzo cha ajali hiyo bado hakijafahamika mpaka sasa.
Askari Polisi wakiwa eneo la tukio kuokoa majeruhi.
Pia alikuwa Mwandaaji wa Miss Dodoma na Kanda ya Kati. Ikumbukwe ndiye aliyemtoa Miss Tanzania 1995, Emilly Adolf. R.I.P Mama Kiwaya
Ajali hii imetokea leo katika eneo la Emaus, Mkoani Dodoma ambapo imehusisha gari kubwa mbili na moja dogo aina ya Toyota Noah. Inadaiwa kuwa Mtu mmoja amepoteza maisha na wengine kadhaa kujeruhiwa. Chanzo cha ajali hiyo bado hakijafahamika mpaka sasa.
Askari Polisi wakiwa eneo la tukio kuokoa majeruhi.