Technology
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 769
- 284
Mwanasiasa mkongwe Mzee James Mapalala amefariki dunia leo katika hospitali ya Kairuki. Mungu amuweke mahali pema. Mzee Mapalala alizaliwa Februari Mosi, 1936.
Mtoto wa Mzee Mapalala, Bernard James amesema baba yake amefariki dunia leo saa 4:30 asubuhi hospitali ya Kairuki alikokuwa tangu wiki mbili zilizopita baada ya kusumbuliwa na maradhi ya kupumua.
Msiba uko nyumbani kwao Kinondoni.
Pia soma
====
Dar es Salaam. Mwanasiasa mkongwe nchini Tanzania, James Mapalala amefariki dunia katika hospitali ya Kairuki alikokuwa akipatiwa matibabu.
Akizungumza na Mwananchi leo Jumatano Oktoba 23, 2019 mtoto wa mwanasiasa huyo, Bernard James amesema baba yake amefariki dunia leo saa 4:30 asubuhi.
“Alikuwa hospitali tangu wiki mbili zilizopita baada ya kusumbuliwa na maradhi ya kupumua,” amesema James.
Amesema familia imekusanyika nyumbani kwao Kinondoni kupanga ratiba ya mazishi.
Mapalala aliyezaliwa Februari Mosi, 1936 ameacha mke na watoto kadhaa.
Alikuwa miongoni mwa wanasiasa wa kwanza waliojitosa kudai mfumo wa vyama vingi urejeshwe nchini Tanzania.
Kufuatia madai hayo, Mapalala alifungwa miaka miwili mkoani Lindi kuanzia mwaka 1986 hadi 1989 na baada ya kutoka aliwekwa kizuizini kwa kipindi cha mwaka mmoja katika kisiwa cha Mafia baada ya kuanzishwa chama cha siasa wakati sheria ilikuwa hairuhusu.
Alianzisha Chama cha Wananchi (CCW) mwaka 1991 na baadaye kiliungana na chama cha Zanzibar – Kamahuru na mwaka 1993 kuzaliwa Chama cha Wananchi (CUF).
Mtoto wa Mzee Mapalala, Bernard James amesema baba yake amefariki dunia leo saa 4:30 asubuhi hospitali ya Kairuki alikokuwa tangu wiki mbili zilizopita baada ya kusumbuliwa na maradhi ya kupumua.
Msiba uko nyumbani kwao Kinondoni.
James Mapalala: Mwanzilishi wa mageuzi aliyeishia kwenye mikosi
HARAKATI za mageuzi nchini zina historia ndefu, zikianza kabla ya uhuru ambapo wa wananchi kupitia vyama na vuguvugu za aina mbalimbali waliungana ili kuwaondoa wakoloni. Hadi mwaka 1961 chama cha Tanu kilichokuwa kikiongozwa na Mwalimu Julius Nyerere kilishinda uchaguzi na kuunda...
www.jamiiforums.com
Mapalala haweshi ndani ya CUF
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza na wananchi wa Kilwa katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijiji cha Magengeni Kilwa Kivinje katika ziara yake ya baadhi ya mikoa ya Tanzania Bara. Kama CUF iliweza kukaa pamoja na CCM iliyodaiwa...
www.jamiiforums.com
James Mapalala: Warioba amewavuruga CCM
FRIDAY, 28 MARCH 2014 James Mapalala (kulia) akiwa na Rais Jakaya Kikwete Mwanasiasa mwenye historia ya kipekee nchini, James Mapalala amesema ufafanuzi wa Rasimu ya Katiba uliotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, umekiacha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye wakati mgumu. Mapalala, ambaye...
www.jamiiforums.com
Yu wapi James Mapalala mwanzilishi wa CUF?
Huu mzozo aside, Mapalala anasema Hamad Rashid Mohammed ni mtu muhimu sana katika CUF kwa sababu ndiye mtu pekee anayeweza kwenda kutafuta fedha nchi za nje kwa ajili ya chama (kuomba misaada) ? Hawa ndio wanamapinduzi wetu jamani. ---- Ni kweli J. K. Mapalala alikuwa ni mmoja wapo katika...
www.jamiiforums.com
Zitto Kabwe: Buriani Mzee James Mapalala, Wajibu umeutimiza
Buriani Mzee James Mapalala, Wajibu umeutimiza Zitto Kabwe James Kabalo Mapalala ametangulia mbele ya haki. Mwenyezi Mungu ndiye anajua amali zake duniani na yeye ndiye atampima kwa matendo yake. Lakini Mzee huyu alitimiza wajibu wake kwa sisi wanadamu tunaoishi Tanzania. Mimi sikuwa...
www.jamiiforums.com
Dar es Salaam. Mwanasiasa mkongwe nchini Tanzania, James Mapalala amefariki dunia katika hospitali ya Kairuki alikokuwa akipatiwa matibabu.
Akizungumza na Mwananchi leo Jumatano Oktoba 23, 2019 mtoto wa mwanasiasa huyo, Bernard James amesema baba yake amefariki dunia leo saa 4:30 asubuhi.
“Alikuwa hospitali tangu wiki mbili zilizopita baada ya kusumbuliwa na maradhi ya kupumua,” amesema James.
Amesema familia imekusanyika nyumbani kwao Kinondoni kupanga ratiba ya mazishi.
Mapalala aliyezaliwa Februari Mosi, 1936 ameacha mke na watoto kadhaa.
Alikuwa miongoni mwa wanasiasa wa kwanza waliojitosa kudai mfumo wa vyama vingi urejeshwe nchini Tanzania.
Kufuatia madai hayo, Mapalala alifungwa miaka miwili mkoani Lindi kuanzia mwaka 1986 hadi 1989 na baada ya kutoka aliwekwa kizuizini kwa kipindi cha mwaka mmoja katika kisiwa cha Mafia baada ya kuanzishwa chama cha siasa wakati sheria ilikuwa hairuhusu.
Alianzisha Chama cha Wananchi (CCW) mwaka 1991 na baadaye kiliungana na chama cha Zanzibar – Kamahuru na mwaka 1993 kuzaliwa Chama cha Wananchi (CUF).