TANZIA: Mwanamuziki Mkongwe, Kassim Mapili amefariki dunia

MAKULUGA

JF-Expert Member
Jan 21, 2011
7,171
9,394
Mzee%2Bmapili.JPG


TANZIA

Mwanamuziki nguli wa dansi nchini, Kassim Mapili amefariki dunia.

Mwanamuziki huyo aliyetamba na bendi za Shikamoo Jazz na Polisi Jazz, amefia nyumbani kwake maeneo ya TIOT Tabata.

Mapili alihudhuria mazishi ya mwandishi Fred Mosha.

Marehemu alifariki ndani kwake akiwa amelala na hakuna aliyejua mpaka jioni hii majirani walipoingia kutokana na kutoonekana kwake kwa siku tatu. Wakachungulia ndani na kuuona mwili.

Polisi wakataarifiwa na kufika na kuvunja mlango na kuutoa mwili wa marehemu!

Inna Lillahi wa inna ilaihi raji'un!
Soma pia: Buriani Sajini Kassim Said Mapili

Mwanamuziki mkongwe wa muziki dansi Kassim Mapili akicharaza nyuzi za Gitaa lake chini ya Kundi zima la Mjomba Band.
MWANAMUZIKI mkongwe wa muziki dansi Kassim Mapili amefariki dunia akiwa chumbani kwake, Tabata jijini Dar es Salaam. Katibu mkuu wa Chama cha Muziki wa Dansi (CHAMUDATA) Hassan Msumari, amesema kuwa kifo cha Mapili kimegunduliwa usiku huu baada ya mlango wa chumba chake kuvunjwa.

Mlango huo ulivunjwa baada ya Kassim Mapili kutoonekana tangu alipokwenda kutazama mpira wa Arsenal na Barcelona Jumanne usiku.


Kwa mujibu wa Msumari, mara mlango ulipovunjwa Kassim Mapili alionekana akiwa ameshafariki akiwa amejifunga taulo, ishara inayoonyesha kuwa aidha alikuwa anakwenda kukoga au ametoka kukoga.

Jumatatu jioni Kassim Mapili alishiriki vizuri mazishi ya mwanahabari Fred Mosha makaburi ya Kinondoni ambapo alipewa wasaa wa kuongea machache na kama vile hiyo haitoshi, Mapili aliimba makaburini hapo kuomboleza kifo cha Fred Mosha.
 
Mwenyezi Mungu, amlaze mahali pema peponi Amina. Mzee wangu Khasimu Mapilli, nitaimisi sauti yako pale E. FM, kupitia kipindi chako cha mziki wa zamani.
 
Mwenyezi Mungu, amlaze mahali pema peponi Amina. Mzee wangu Khasimu Mapilli, nitaimisi sauti yako pale E. FM, kupitia kipindi chako cha mziki wa zamani.

Efm kipindi cha miziki ya zamani SI kinaendeshwa na mr kitime?
 
Ina maana marehemu alikua bachela,siku tatu nzima hadi majirani wanachungulia dirishani
 
Usishangae hao ndio vijana wa zamani!R.I.P Mapili
Hakupata kibanda hata chanika,zamani kujenga ilikua rahisi sana unalazimishwa kununua kiwanja haswa ukiwa na kazi,kijana huyo alikua bendi ya polisi anapata kila kitu
 

Mwanamuziki mkongwe wa muziki dansi Kassim Mapili akicharaza nyuzi za Gitaa lake chini ya Kundi zima la Mjomba Band.
MWANAMUZIKI mkongwe wa muziki dansi Kassim Mapili amefariki dunia akiwa chumbani kwake, Tabata jijini Dar es Salaam. Katibu mkuu wa Chama cha Muziki wa Dansi (CHAMUDATA) Hassan Msumari, amesema kuwa kifo cha Mapili kimegunduliwa usiku huu baada ya mlango wa chumba chake kuvunjwa.

Mlango huo ulivunjwa baada ya Kassim Mapili kutoonekana tangu alipokwenda kutazama mpira wa Arsenal na Barcelona Jumanne usiku.


Kwa mujibu wa Msumari, mara mlango ulipovunjwa Kassim Mapili alionekana akiwa ameshafariki akiwa amejifunga taulo, ishara inayoonyesha kuwa aidha alikuwa anakwenda kukoga au ametoka kukoga.

Jumatatu jioni Kassim Mapili alishiriki vizuri mazishi ya mwanahabari Fred Mosha makaburi ya Kinondoni ambapo alipewa wasaa wa kuongea machache na kama vile hiyo haitoshi, Mapili aliimba makaburini hapo kuomboleza kifo cha Fred Mosha.
 
maskini alale kwa amani tu wote njia yetu moja .. usikute alishabikia arsenal aiseee..
 
Kafa peke yanke ndani, majirani ndio walio tambua kutoonekana kwake, sasa subiri watakavyo jitokeza watu kudai urithi, heeee kila mmoja atadai yeye ndie muhusika na alikuwa na marehemu mpaka dakika ya mwisho. R.I.P majaliwa
 
Poleni wafiwa, wekeni basi angalao zilipendwa yake moja nzuri tuisikilize na kapicha tumuone jamani
 
Back
Top Bottom