Tanzia: Mwanajamvi afariki Dunia.

Tanzia: Mwanajamvi afariki Dunia.

wasaimon...REQUIEM: Pumziko la Milele umpe ee Bwana, Na mwanga wa Milele umwaangazie, apumzike kwa amani...> Roho za waumini wapate rehema kwa Mungu, Wapumzike kwa amani. Amina
 
Ama kwa hakika sisi sote tumetoka kwa MUNGU na bila shaka KWAKE tutarejea. MUNGU Atusamehe sote sisi na waliotutangulia. wao wametutangulia nasi tuko njiani....:crying::crying::crying::crying::crying::crying::crying::crying:
 
pole sana Bro wangu,nimeenda mchana msibani but nikashidwa kabisa kuingia nikaishia bondeni bar huku, nilisikia watu wakisema ni jmosi but sikuuliza wapi coz nilijua nitajua tu kwa namna yoyote ile, kuhusu mama Tony ndio alinifanya nikashindwa kuingia mana naambiwa akiingia mtu anaemjua inakuwa balaa, sina cha kusema kuhusu mama Tony,Mungu ampe nguvu/ujasiri, siwezi kusema sijui ataanzia wapi Mungu mwenyewe ana makusudi yake, roho inaniuma zaidi kwa Tony, alivyopambana kumtafutiaa shule nyingine ili amtoe kata, amepata hajapelekwa Sai kaondoka, yaani my bro, imeniuma sana sana sana, sina maelezo kabisa, na jana mida ya saa 4 nilikuwa kwenye kikao nikakuta missed call yake nikajua ananikumbushia kumtafuta huyo mtu tuliekuwa tuna shida nae leo so sikupiga nikijua nimeshamaliza hiyo ishu ni suala la kukutana, laiti ningemcal niongee nae ya mwisho., R.I.P my Bro Sai, sijui kama nitamsahau kirahisi, nikipata shida najua nina wa kumtafuta chap na nikatatuliwa chap, Mungu anajua kwanini.
Hii imenitoa machozi Live...na machozi ya mwanaume ni mabaya sana, maana yanaingia tumboni.
Mungu saidia.
 
Ooooh! rest in peace bro! .................. nasi twaja mbaya ni kutangulia!!!!!!!!!
Aaaaaamen!
 
RIP Wasaimon. Poleni wafiwa, Mungu awatie nguvu na kuwafariji katika kipindi hiki cha majonzi.
 
We know that you are going through a difficult time and no amount of words will help take the pain away. As hard as it seems, you will get through this difficult time and emerge stronger.

We are always around to help you through this trying period.

So sorry for the loss and may his soul Rest In Peace
 
Back
Top Bottom