TANZIA: Mufti Issa Shaaban Bin Simba afariki Dunia

TANZIA: Mufti Issa Shaaban Bin Simba afariki Dunia

Nimeingia ofisi moja binafsi hapa jijini Mwanza nikiwa nahitaji kufanya shughuli fulani,ila nikaambiwa kuwa ofisi inafungwa kwa vile mufti wa Tanzania kafariki,wakasema wanafunga ofisi kufuatilia zaidi habari hizo,naomba kabla sijageuza kurudi Dar mwenye taarifa kamili atujulishe tafadhali,ili kama sio kweli niendelee kuwasubiri tukamilishe kazi yetu.
 
إِنَّا للهِ وَإِنَّـا إِلَيْهِ رَاجِعونَ
Habari zilizopatikana ni kwamba Sheikh Mkuu wa Tanzania
Issa Shaabani bin Simba amefariki Dunia.

Taarifa zinasema Mufti Simba amefariki asubuhi hii katika Hospitali ya TMJ ya jijini Dar es Salaam. Mufti amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya sukari kwa muda mrefu.
Source: ahbaabur blog
 
Inna lilah wainna ilaih Rajiun. Allaah (s.w) akusamehe mapungufu yako na akuwafikishe katika Jannat firdaous. Ameen
 
Polen sana , waislam.

Kwenye majonzi tupo pamoja regardless dini zetu
 
Habari nilizo zipata ni kua mufti Simba kafariki dunia mapema leo.

source Clouds fm leo tena.
 
Mbona kwake hapa Shinyanga Hamna dalili Ya msiba?
 
poleni waislamu wote na watanzania kwa ujumla, hakika sote ni wa mungu na kwake tutarejea
 
Poleni ndugu zetu Waislamu kwa kuondokewa na kiongozi wenu mpendwa, Mufti Issa Bin Shaban Simba. Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi.
 
RIP mufti Simba
hakika ulikuwa muelewa sana na nlikukubali sana...kuongozi taasisi nyenye migawanyiko si jambo rahisi ila alilimudu
 
Back
Top Bottom