Calnde
JF-Expert Member
- Oct 7, 2008
- 1,373
- 277
kufuatia njaa iliyokithiri somalia (haijawahi kutokea ndani ya miaka 60) Tanzania imeahidi kuisaidia Somalia tani 300 za mahindi. Huu ni moyo wa utoaji
na hakika likiwa limefanyika kwa moyo basi Mungu ataibariki Tanzania mara dufu.
Lakini kuna jambo moja tuu linanishangaza, hivi ni kweli Tanzania inawapenda watu wake? Leo bungeni nimewasikia wabunge kama watatu
wanalalamika majimboni kwao kuna njaa kali na chakula walichoahidiwa (iwe cha bure/au cha gharama nafuu/gharama halisi) hakijapelekwa zaidi ya
miezi miwili sasa. Huu ndo mwendelezo tabia ya kujali watu wa nje kuliko wazawa? Sipingi kusaidiwa kwa somalia, maana hakika tunapaswa kufanya
hivyo lakini maneno matakatifu yanasema mtu asiyewajali watu wa nyumbani mwake ameikana imani, ni mbaya kuliko asiye amini! Nawasilisha