Dr Matola PhD
JF-Expert Member
- Oct 18, 2010
- 56,289
- 92,371
Igunga kuna njaa inatishia kuuwa Watanzania, sasa kama Matonya nae siku anasaidia omba omba wenzake basi kweli uchumi wetu unapaa!
Rais Jakaya Mrisho Kikwete Mwandishi WetuSERIKALI imetangaza kuwa itatoa msaada wa tani 300 za mahindi, ili kuwasaidia watu 3.5 milioni wa Somalia kupunguza makali ya ukosefu mkubwa wa chakula unaowakabili. Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, ilieleza kuwa Tanzania pia imeahidi kutoa misaada mingine kwa nchi hiyo kwa kadri uwezo wa nchi unavyoruhusu . Mchango wa Tanzania umetangazwa wakati wa mazungumzo rasmi kati ya Serikali ya Tanzania na ile ya Jamhuri ya Somalia, na wakati wa futari ambayo Rais Jakaya Kikwete, alimwandalia mgeni wake Rais wa Somalia, Sheikh Sharif Sheikh Ahmed ambaye alikuwa katika ziara ya siku mbili ya kikazi nchini. Tunasikitika sana kuona matatizo makubwa ya ukosefu mkubwa wa chakula yanayoikabili nchi yako. Kama unavyojua Tanzania ni nchi maskini na uwezo wetu siyo mkubwa. Lakini tuna methali hapa isemayo kutoa ni moyo siyo utajiri. Kwa hiyo kwa moyo huo wa mtu maskini, tumeamua kutoa mchango wetu mdogo wa tani 300 za mahindi ambazo ni sawa na magunia 3,000 ili kusaidia ndugu zetu wa Somalia kukabiliana na hali ya njaa kubwa, Rais Kikwete alimwambia Rais Sheikh Ahmed. Aliongeza Rais Kikwete: Tunajua kuwa mahitaji yenu ni makubwa zaidi kuliko hiki kidogo tulichotoa. Lakini sasa ndiyo kwanza tumeingia katika msimu wa mavuno. Tutaangalia huko mbele kama tunaweza kuwachangia zaidi ndugu wetu wa Somalia. Tunazungumza pia na marafiki zetu ili tuwashawishi kuona kama nao wanaweza kuunga mkono jitihada za Serikali ya Jamhuri ya Somalia ya kuhakikisha inapata chakula cha kutosha ili kuokoa maisha ya mamilioni ya wananchi. Wakati wa futari ambayo Rais Kikwete alimwandalia Rais huyo wa Somalia katika Mwezi Mtukufu huu wa Ramadhani, Rais Kikwete alitoa mwito kwa kampuni zinazotengeza maji nchini kusaidia kuchangia upatikanaji wa maji kwa wananchi hao wa Somalia. Somalia inahitaji mamilioni ya lita za maji ili kukabiliana na ukosefu mkubwa wa chakula na maji. Tutazungumza na kampuni zinazotengeneza maji hapa nchini kama nazo zinaweza kuchangia kupambana na janga hili kubwa linalowakabili wananchi wa Somalia, Rais Kikwete alimwambia Rais wa Somalia katika shughuli ya futari. Shughuli hiyo ilihudhuriwa na watu wengi wakiwamo mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania, wakuu wa mashirika ya umma na binafsi nchini, mawaziri, makatibu wakuu na maofisa waandamizi wa Serikali na mawaziri wakuu wa zamani, Mzee Salim Ahmed Salim na Mzee Joseph Warioba. Katika mazungumzo hayo rasmi, Tanzania na Somalia, zimezungumza masuala mengi ambako nchi hizo zinaweza kushirikiana kuisaidia Somalia baada ya ujumbe wa nchi hiyo kuelezea maeneo ambako Tanzania inaweza kuisaidia Somalia kama katika mapambano ya pamoja dhidi ya ugaidi katika Bahari ya Hindi na kusaidia kufundisha wataalamu wa fani mbalimbali. Rais Kikwete pia alimpongeza Rais wa Somalia na ujumbe wake wa mafanikio ya kijeshi dhidi ya kikundi cha kigaidi cha El-Shabaab ambacho kimefukuzwa katika maeneo mengi ya Mji Mkuu wa Mogadishu ambacho kimekuwa kinayashikilia kwa muda mrefu. Rais pia alimpongeza Rais Sheikh Sharif Sheikh Ahmed kwa mafanikio yake mengine ya kuleta utulivu zaidi ndani ya Serikali yake na kuongeza muda wa utumishi wa Serikali na Bunge kama moja ya njia ya kuleta maelewano ndani ya Serikali, na kati ya Serikali na Bunge la nchi hiyo. Rais Ahmed ambayo aliwasili nchini juzi na asubuhi, aliondoka nchini jana baada ya kuwa kukutana na kuzungumza na waandishi wa habari kwenye Hoteli ya Kilimanjanro Hyatt Regency mjini Dar es Salaam. |