Tanzania yahofiwa jinsi inavyoshughulikia Janga la Corona

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,011
9,878
Mkurugenzi wa kituo cha kudhibiti magonjwa Barani Afrika ameelezea wasiwasi wake kuhusu namna Tanzania inavyokabiliana na mlipuko wa Virusi vya Corona.

Dkt. John Nkengasong aliiambia BBC hakuwa na data za kutosha za kufahamu hali ilivyo nchini Tanzania. Alisema kituo cha kudhibiti magonjwa kimeanzisha jitihada za pamoja za kupambana na virusi hivyo.

"Tunaendelea kutumaini na kuiomba Tanzania kuripoti hali ilivyo ili tuweze kufanya kazi kwa pamoja na kuondoa virusi hivi katika bara hili," alisema. Alisisitiza kuwa kuna uhitaji wa mataifa yote ya Afrika kushirikiana katika hili.

"Tunaendelea kuwasiliana na Tanzania lakini bado hatujapata majibu ambayo tunayatarajia," alisema. Rais wa Tanzania John Magufuli amesisitiza kusema kuwa taifa lake liko salama.

Tanzania inajiandaa kufanya uchaguzi mwezi Oktoba na shamrashamra za Uchaguzi zimeanza. Wananchi wengi wa taifa hilo wamekuwa wakiendelea na shughuli zao bila kuvaa barakoa na wala kuzingatia kukaa mbali.
 
tuna mambo mengi ya kushughulikia, corona haifiki hata kwa malaria. Ogopa Taifa likianza kujielewa. Hii ni sawa na jirani aanze kulaumu mbona kwake umeme umekatika kwa jirani unawaka, hajui Kama jirani anatumia jenereta. Songa mbele Rais Magufuli, tuko pamoja. Tanzania moja, Taifa moja
 
Wapewe taarifa au lipoti ipi wakati kila siku mheshimiwa rais wetu anasema hakuna korona,sasa wao wanataka waambiwe kuwa kunawagonjwa Millioni sita ndo wajue hiyo ndo taarifa sahihi.

Kule wanakotoa taarifa sahihi kuna jipya gani ? Kuna kitu gani kimebadilika?

Huu ni upuuzi watuache
 
Ninachoshangaa mimi kwanini ushirikiano kwenye covid-19 na sio Malaria?

Jirani akifanya fumigation wewe usipofanya mbu hupumzika tu kwenda kwa aliyefanya fumigation, ila tena hurudi kutokea kwa jirani ambaye hakufanya fumigation.

Mkitaka kufikia malengo ya pamoja lazima muwe mnakubaliana issues. Tanzania haikubali lolote la wenzao, lakini wanataka wao wakubaliwe ya kwao.

Tanzania wangeiacha tu, imeshakuwa sugu kwenye hili.
 
Back
Top Bottom