Tanzania: Vyama vya upinzani vyanyimwa ruzuku Rasmi

Ninavyowajua Chadema wangeyimwa cheki ya ruzuku lazima wangetoa tamko au kuitisha maandamano nchi nzima.
 
Kama kiongozi wa Chadema halafu kiawara cha nje kinasumbua ndo balaa ndo linapoanzia
 
Bado nangoja mwenelezo wa darasa hili!.
Wakuu tiririka zaidi ili niweze kuelewa nielimike.

hapo kuna vitu vitatu unaweza kujifunza....jinsi ya kuelezea jambo........jinsi ya kubishia jambo....la mwisho ni jinsi malipo ya ruzuku yanavyolipwa
 
Huu sasa ni upuuzi wa hali ya juu kuwahi kufanywa na ofisi ya msajili wa vyama vya siasa!
 
I always keep asking myself why CCM walikubali siasa ya vyama vingi?? maana kila kukicha wanatumia taasisi zao kama POLISI, MSAJILI WA VYAMA,USALAMA WA TAIFA, MAHAKAMA ili Kugandamiza demokrasia na kudhibiti wapinzani hata ikibidi kuuwa, Ulaghai, kubambikia watu kesi na kila aina ya manyanyaso na ubakaji wa demokrasia.Si waseme tuu nchi ni ya chama kimoja? Baba na Mama wa Demokrasia TZ alishakufa zamani, vyama vya upinzani vimabaki yatima.

Kumbe ulikuwa hujajua siri ya TZ kukubali mfumo wa vyama vingi? Ilikuwa mbinyo mkali sana toka nchi wafadhili. Hizi propaganda wanazotoa magamba kuwa wao waliridhia mfumo wa vyama vingi, ni uongo wa hali ya juu, na ndiyo maana ingawa kwa mujibu wa sheria za nchi yetu, vyombo vyote vya usalama vinatakiwa visijiingize kwenye siasa, lakini hali halisi inajidhihirisha bila shaka yoyote kuwa Jeshi la Polisi na Usalama wa Taifa, vyombo hivyo viwili vinatekeleza kwa asilimia 100, maelekezo ya kuminya vyama vya upinzani vinavyoonekana ni tishio kwa CCM, wanayopewa na watawala. Sasa na huyo Tendwa naye yumo kwenye huo mkumbo, na ndiyo maana hilo tukio haliwezi kushangaza sana, maana ni majuzi tu Tendwa alinukuliwa akisema kama Chadema wamesusa kufanya kazi na mimi, si wasuse na kuja kupokea ruzuku!!
 
Tendwa ni tikiti maji...

Kwa hisani ya wakulima

262851_141607072593034_100002312266278_260497_8104350_n.jpg
 
hizo ruzuku zitatoka tu...
huyo tendwa anajitafutia matatizo maana anawaoshea jina vyama vya upinzani.
alafu hiyo kazi imemshinda pia nahisi nguo zake za ndani zina bendera ya sisiem.
kiongozi kama huyu wa nini kwa faida ya Taifa labda anafaa kwa faida ya sisiem
kwa kauli kubwa HHHatumtakiiiiiiiiiiiii.................
 

Kwa watu wasiojua ukweli/uongo wanaamini kile wanachokisikia kiwe kweli au uongo.

Sasa wewe unaposema kuwa habari hii si ya ukweli, basi tunaomba utupe hizo habari ulizo nazo za ukweli.
:help:

Soma kwa kina post Namba 66 ya Deus Malya uone ufafanuzi kuhusiana na nafasi ya Tendwa kisha soma kwa makini post ya mleta mada anapokwambia baada ya suala kuwa mtandaoni wameitishwa kikao,,kumbuka kapost tar ngapi hii na kikao kimeitishwa wakati gani,,,ila msingi mkubwa upo kwenye ufafanuzi anaojaribu kuutoa Malya nami nikitoa yangu/ukweli wa procedures karibia ntakuwa narudia. Twende tu taratibu mkuu usihamaki
 
Kumbe ulikuwa hujajua siri ya TZ kukubali mfumo wa vyama vingi? Ilikuwa mbinyo mkali sana toka nchi wafadhili. Hizi propaganda wanazotoa magamba kuwa wao waliridhia mfumo wa vyama vingi, ni uongo wa hali ya juu, na ndiyo maana ingawa kwa mujibu wa sheria za nchi yetu, vyombo vyote vya usalama vinatakiwa visijiingize kwenye siasa, lakini hali halisi inajidhihirisha bila shaka yoyote kuwa Jeshi la Polisi na Usalama wa Taifa, vyombo hivyo viwili vinatekeleza kwa asilimia 100, maelekezo ya kuminya vyama vya upinzani vinavyoonekana ni tishio kwa CCM, wanayopewa na watawala. Sasa na huyo Tendwa naye yumo kwenye huo mkumbo, na ndiyo maana hilo tukio haliwezi kushangaza sana, maana ni majuzi tu Tendwa alinukuliwa akisema kama Chadema wamesusa kufanya kazi na mimi, si wasuse na kuja kupokea ruzuku!!

NA UDHAIFU WA KATIBA PIA UTAWAWEZESHA MASHETANI WAKIJANI KUENDELEA KUSHIKA DOLA TENA, MAMBO YATABAKIA HAYAHAYA.I am not sure if ccm goverment would confer the execution of the new constitution before 2015
 
aaah! kumbe hela mnapata sasa mbona mnatuchangisha na sisi wananchi wakat hatujui hzo mnazopata mnazifanyia nini...wizi mtupu

Du! Ndo nimesikia leo, msajili wa vyama anachangisha fedha kwa wananchi? Au sijakuelewa. Ni vyema kujipatia maarifa na taarifa (kujielimisha) kabla ya kuchangia. Msome mshikaji, tehn argue against or for accordingly.
 
CCM 1.2billion
CHADEMA 233million
CUF 98million

Hata hivyo utaratibu wa kutoa hizi hela ofisi ya Msajili inahusika kwa sehemu ndogo sana kwa kuandika Voucher kwenda hazina ambapo hazina inahamishia fedha hizo kwenye account za vyama kwa njia ya kielectroniki wala hakuna utaratibu wa Cheque kama mtoa habari alivyosema. Pia ile Voucher huwezi kuandika chama kimoja na kuacha vyama vingine kwa SABABU YOYOTE ILE.
Pengine ingeelezwa kuwa serikali haina fedha kwa sasa ningeelewa kwakuwa ni ukweli kuwa vyama vyote havijapata ruzuku hadi jana.

Deus F Mallya, uwe tayari kusahihishwa katika hili ulilotamka.
Utaratibu wa Msajili wa vyama vya siasa ni kupeleka voucher za madai ya ruzuku hazina. Hazina ikishaandika
hundi zinarudishwa kwa Msajili wa vyama vya siasa. Yeye ndiye mwenye kutia sahihi
hundi hizo kabla ya kuwakabidhi wahusika. Bila sahihi ya msajili wa vyama vya siasa hundi hizi zikipelekwa hazina kuchota kilicho chao vyama vya siasa haitakubalika.

Kwamba Tendwa amekalia
hundi hizo za vyama vya upinzani si jambo la kupinga, ila inawezekana ni mchezo wa rafu za Tendwa kuitishia nyau Chadema.

Deus F Mallya
hundi zinazotoka serikalini zina utaratibu huo si vyama vya siasa tu, labda hujawahi kupata hundi za malipo toka hazina zisizohusu mishahara. Check za malipo toka Hazina hata ukiishaishika mkononi haina nguvu ya kuchukua pesa mpaka ofisa mwandamizi mwidhinishaji umpelekee amwage wino. Nakubaliana na mleta hoja. Mimi mwenyewe mwaka huu nilishikishwa adabu nilipopata hundi yangu toka hazina nikafiri pesa ninayo tayari, lakini nipoenda pale bank nikaambiwa kazi bado niende kule kwa ofisa fulani mwidhinishaji amwage wino ndipo niirudishe bank kupata kilicho changu. Nilipofuata utaratibu wao mambo yalienda shwari.

Wanajamii forums tusijenge ubishi wa kutumia akili bila kujua taratibu za mhimili wa serikali unavyofanya kazi katika idara ya pesa kuhakikisha malipo yanamfikia mhusika.
 
Huyu jamaa anapenda kubishana bila evidence. Hata kudhani kuwa Msajili siyo Mhasibu ameshindwa. Hata kukumbuka kuwa kasma ya kuendeshea nchi ambako ndiko fungu la kuendeshea Ofisi ya Msajili ni Tofauti na kasma inayotumika kulipa ruzuku zote nchini. Anajaribu kuwashawishi watu waelewe anavyotaka yeye. John Tendwa si Mhasibu na kazi yake ni kutoa Voucher ambazo zilishaandaliwa zina list ya vyama vyote.

Tusikazane kujenga hoja kwa kutumia akili zetu, tujenge hoja kwa kufuata taratibu za malipo ya hundi zitolewazo na serikali. Nakubaliana kwamba hundi ziko kwa msajili wa vyama, lakini ulichosema wewe si sahihi kwa vile hundi ikishatoka hazina lazima ofisa mwandamizi katika idara inayohusika na malipo amwage winu. Hii ni kwa sababu ya serikali kuthibiti malipo sahihi yafikishwa kwa mhusika. Hazina huandika hundi tu kutokana na hati za malipo, kwamba anayelipwa ndiye au la ni ofisa mwandamizi katika idara yake ndiye atakayejua ndipo amwage wino wake.

Utaratibu huo si kila mmoja toka chama cha siasa ataweza kwenda kuchukua hundi kwa msajili wa vyama, kuna offisa mmoja au kwa utaratibu uliowekwa ndiye mwenye kuweza kuchukua hizo hundi kwani kuna mambo ya kuhakiki uhalali wa mchukua hundi kwa kuonyesha vitambulisho husika.
 
Deus F Mallya, uwe tayari kusahihishwa katika hili ulilotamka.
Utaratibu wa Msajili wa vyama vya siasa ni kupeleka voucher za madai ya ruzuku hazina. Hazina ikishaandika
hundi zinarudishwa kwa Msajili wa vyama vya siasa. Yeye ndiye mwenye kutia sahihi
hundi hizo kabla ya kuwakabidhi wahusika. Bila sahihi ya msajili wa vyama vya siasa hundi hizi zikipelekwa hazina kuchota kilicho chao vyama vya siasa haitakubalika.

Kwamba Tendwa amekalia
hundi hizo za vyama vya upinzani si jambo la kupinga, ila inawezekana ni mchezo wa rafu za Tendwa kuitishia nyau Chadema.

Deus F Mallya
hundi zinazotoka serikalini zina utaratibu huo si vyama vya siasa tu, labda hujawahi kupata hundi za malipo toka hazina zisizohusu mishahara. Check za malipo toka Hazina hata ukiishaishika mkononi haina nguvu ya kuchukua pesa mpaka ofisa mwandamizi mwidhinishaji umpelekee amwage wino. Nakubaliana na mleta hoja. Mimi mwenyewe mwaka huu nilishikishwa adabu nilipopata hundi yangu toka hazina nikafiri pesa ninayo tayari, lakini nipoenda pale bank nikaambiwa kazi bado niende kule kwa ofisa fulani mwidhinishaji amwage wino ndipo niirudishe bank kupata kilicho changu. Nilipofuata utaratibu wao mambo yalienda shwari.

Wanajamii forums tusijenge ubishi wa kutumia akili bila kujua taratibu za mhimili wa serikali unavyofanya kazi katika idara ya pesa kuhakikisha malipo yanamfikia mhusika.

Utaratibu wako ni tofauti na utaratibu wa Vyama vya Siasa. Pengine wewe ulikuwa unalipwa kiasi kidogo ambacho kinabebeka kwa pamoja kirahisi sana. Ukiunganisha malipo ya ruzuku zote na ili vyama visipate usumbufu wa Go& Return kufuatilia Cheque zao ndipo ulipowekwa utaratibu wa kielektroniki. Nakuhakikishia (Kwa Evidence ya Mkurugenzi wa Fedha wa Chadema na Mweka hazina wa CCM) kuwa hakuna utaratibu wa cheki kwa vyama vya siasa kutoka OFISI YA TENDWA. Hazina wanapokea Voucher kama maombi ya fungu kwenda kwenye Acount za vyama vya siasa na hakuna huo mlolongo wa Hazina kutoa Cheque zirudi tena na kuhitaji huruma ya msajili. Nakubali kukosolewa lakini kwa facts.
 
Ninavyowajua Chadema wangeyimwa cheki ya ruzuku lazima wangetoa tamko au kuitisha maandamano nchi nzima.

Mapema mno, huenda hundi hizo zilipishana kufika ofisini kwa msajili wa vyama, ya CCM pengine ilitangulia. Tamko hutolewa baada ya kujiridhisha kuona msajili wa vyama vya siasa amedinda kutoa hundi kwa hoja zisizoeleweka au kukubalika.
 
Back
Top Bottom