Tanzania tumejiandaaje kwa Ebola?

Tanzania tumejiandaaje kwa Ebola?

Siielewi hii post yako!! Kwani serikali ndiyo imeleta ebola kutoka uganda? Sio watu waoingia uganda pamoja na serikali kukataza halafu wanuleta ugonjwa na kuua watu wasiokuwa na hatia??/ Hili ni tatizo la waliokwenda uganda na kurudi tanzania wakati serikali imetahadharisha sana kuhusu huu ugonjwa.
Ugonjwa huo unasadikiwa kuingia katika kijiji kilichotajwa kwa jina la Mlongo wilayani Karagwe. Wananchi wamekuwa na hofu na wanailaum serikali kwa kutochukua taadhari kuzui ugonjwa huo toka uganda. Wanadai kuwa uzembe huo ndio ulipelekea UKIMWI kuingia toka Uganda.
 
Dr hakusema kuwa ni ebola amesema mgonjwa ana dalili za huo ugonjwa hivyo wanachukua tahadhari. Amesema tutaarifiwa ni ugonjwa upi baada ya majibu ya vipimo kupatikana.
Kwanini wasiseme ni anthrax/kimeta na waseme ni ebola?!, maana hizi pia ni clinical signs za antharx. Differential diagnosis ni muhimu.
 
Siielewi hii post yako!! Kwani serikali ndiyo imeleta ebola kutoka uganda? Sio watu waoingia uganda pamoja na serikali kukataza halafu wanuleta ugonjwa na kuua watu wasiokuwa na hatia??/ Hili ni tatizo la waliokwenda uganda na kurudi tanzania wakati serikali imetahadharisha sana kuhusu huu ugonjwa.

Mkuu hapo huhitaji kunielewa mimi hayo ni malalamiko yaliyotolewa na wananchi na yakaripotiwa hivyo kwa hiyo nimeyaleta kama nilivyosikia katika 'breaking news' si mawazo yangu binafsi!
 
Dr hakusema kuwa ni ebola amesema mgonjwa ana dalili za huo ugonjwa hivyo wanachukua tahadhari. Amesema tutaarifiwa ni ugonjwa upi baada ya majibu ya vipimo kupatikana.

Ni kweli Dr Andrew aliyehojiwa hakusema ni Ebola bali mgonjwa anaonesha dalili za ugonjwa wa Ebola kwa hiyo basi amewekwa chini ya uangalizi maalum pamoja na mamaye na muuguzi wake. Wanasubiri wataalamu wa wizara ya afya wampime na watatoa taarifa.
 
Serikali inathamini kununua magari yenye thamani kubwa wakati haina hata maabara ya kupimia ugonjwa wa Ebola. Fuatilia sakata hili kutoka gazetii la mwananchi:

[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading, width: 100%"]

‘Serikali haina maabara ya kupima Ebola’
[/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"] Send to a friend [/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: createdate"]
Thursday, 16 August 2012 21:29
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]

Geofrey Nyang'oro na Zaina Malongo

SERIKALI imeweka wazi kuwa hadi sasa hakuna majibu sahihi yanayoweza kuthibitisha kuwapo kwa ugonjwa wa
Ebola kwa kuwa hakuna maabara ya kupima ugonjwa huo.

Aidha hali hiyo imesababisha vimelea vya mtu aliyedaiwa kuwa na dalili za ugonjwa huo kupelekwa Uganda ambako kuna mabara zinazofanya kazi ya uchunguzi na kutambua ugonjwa huo.

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk Hussein Mwinyi alisema hayo jijini Dar es Salaam jana alipokuwa akijibu maswali ya waandishi wa habari waliotaka kujua hatua ilipofikia kuhusu ugonjwa wa Ebola.

Agost 5 mwaka huu maofisa wa afya walifika Hosptali Teule ya Wilaya ya Karagwe ya Nyakahanga na kumuona mgonjwa akiwa na baadhi ya dalili zinazofanana na ugonjwa wa Ebola na kuzipeleka Dar es Salaam kwa uchunguzi zaidi.

Akifafanua hilo Dk Mwinyi alisema hadi sasa hakuna majibu ya vipimo hivyo kwa kuwa vilipelekwa Uganda ambao wana maabara zinazothibitisha tatizo hilo.

Alifafanua kuwa hadi sasa bado majibu ya vipimo hivyo vya ugonjwa huo wa mlipuko havijarejea nchini lakini akawatoa hofu watanzania akisema hadi sasa hakuna kesi nyingine iliyoripotiwa.
“Nikweli hatujapata majibu ya vipimo vile,lakini hakuna sababu kwa watanzania kuwa na hofu kwani hakuna kesi nyingine ya mgonjwa iliyopatikana hadi sasa”alisema Dk Mwinyi.

Mwinyi alifafanua kuwa serikali kupitia wizara hiyo ya Afya inaendelea na mchakato wa kuelimisha jamii juu ya namna ya kukabiliana na ugonjwa huo ambao hauna dawa.

“Ugonjwa huu unaambukizwa na kirusi aina ya fangasi, vimelea hivyo vipo vingi na vinatofuatiana na ndio sababu tumepeleka Uganda kupima, lakini kwa kuwa tatizo hilo limekuwa likijirudia nchini tunaona haja ya sisi kuwa na kipimo hicho”alisema Mwinyi.

Wakati mtu mmoja akigundulika kuwa na dalili za ugonjwa huo wa Ebola, nchi jirani ya Uganda ulishatokea na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 100.Mwinyi alisisitiza kuwa serikali bado inafuatilia majibu hayo na kwamba pindi yatakapopatikana itayatoa kwa umma.
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
hii ni aibu kwa taifa,kuna hatari huyo mgonjwa akapandikiziwa ebola hata kama alienda na ugonjwa wa kawaida.
 
Usishangae kukosekana kwa Maabara peke yake. Jiulize tuna CT Scan ngapi Tanzania!
 
Kipi cha kushangaza hapo?? Hiyo ndio nchi yenu isiyojua vipaumbele muhimu wa wananchi wake!!wakati Dr's tunagoma tupate vifaa tiba mahospitalini tulionekana wauaji..shiit!
 
Mimi nina hakika vifaa vya kupimia viko (PCR machines) na wataalamu wako nchini hata hapo SUA and NIMR. Kinachohitajika ni primers za kupimia huo ugonjwa ambao fedha zake sio nyingi sana. Ni kujipanga tu.

Au nimekosea molecular biologists? Hatuna maabara ya category 4 hapa Tz?
 
Huu ugonjwa unatisha. Kwa hii kasi yake ya kusambaa sijui kama serikali imejiandaa au ndio inazidi tu kupunguza bajeti ya wizara ya afya. Hizi viwanja vya ndege na mipaka je vinatumika vizuri kuthibiti? Ugonjwa upo jirani sana. Bahati mbaya hatujatenganishwa na bahari. Tusisubiri mpaka ufike Rwanda, Burundi, DRC, au Kenya, ndiposa tuchukue hatua.
Mganga mkuu wa serikali Dk. Donald Mbando amesema tahadhari hiyo inafuatia kuwepo kwa mlipuko wa ugonjwa huo katika nchi za afrika magharibi na hivyo serikali imeshatuma timu ya wataalam wake katika maeneo ya mipakani kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi ya namna ya kumgundua mtu mwenye virusi vya ugonjwa huo.

Dk. Mbando amesema kupitia wataalam wa afya waliopo katika mipaka ya nchi serikali itakuwa ikitoa taarifa za mara kwa mara ya namna uzuiaji wa ugonjwa huo kwa wananchi na wanapata elimu ya kutosha ya kujikinga na virusi vya Ebola.

Wakati huo huo, uchunguzi wa East Africa Radio umebaini kuwepo kwa matumizi makubwa ya mashine zinazodaiwa kupima na kutambua magonjwa mbali mbali ya binadamu za Guantamo Analyzer, mashine ambazo sifa na uwezo wake katika kubaini magonjwa inayopima ni wa kutiliwa shaka.
Mashine hizo zimekuwa zikitumiwa kwa wingi na watu wanaodai kutoa tiba mbadala ambapo mbali ya kupima na kutambua orodha kubwa ya homa na magonjwa yanayowasumbua wanadamu, mashine hizo pia zinadaiwa kuwa na uwezo wa kuondoa sumu mwilini.

Hata hivyo, alipoulizwa kwa njia ya simu kuhusu mashine hizo, msajili wa bodi ya maabara binafsi Bi. Zainab Mfaume amekana kuzifahamu na kwamba hazipo katika orodha ya vifaa vya uchunguzi wa magonjwa vinavyotambuliwa na bodi hiyo.

Chanzo:EATV
 
Wadau huu ugonjwa unazidi kuenea na kusambaa kwa kasi sana. Nigeria, ethiopia na nchi nyingine zimechukua hatua kali za tahadhari kuzuia tishio la ugonjwa huu. Ukizingatia urahisi wa kuambukizwa,ugumu wa kutofautisha dalili zake na magonjwa mengine, na ukweli kwamba congo si mbali na 90% wanaoambukizwa wanafariki wakiwemo madaktari bingwa. Kwa tishio hili nilitarajia sirikali ingechukua hatua za tahadhari mapema na kuwaelimisha wananchi juu ya tishio hilo. Serikali imekomaa na IMTU na mafuvu badala ya kuhangaikia wale walio hai. Em sirikali kuweni siliasi basi hii ngoma ikiingia bongo mpaka ije kuisha tushaumia sana..
 
Liberia wameamua kufunga mipaka yao mingi na michache ambayo imeachwa wazi wameweka Wataalam wa kuhakikisha wote watakaoingia nchini humo wako salama. Ugonjwa huu unaua kwa kasi ya kutisha na 60% to 90% ya walioupata wanafariki. Serikali lazima ianze kuchukua hatua madhubuti za tahadhari mapema badala ya kusubiri ugonjwa huu uingie nchini.

Ebola outbreak: Liberia closes its borders - CNN.com
 
Duh aisee, huu ugonjwa tuombe Mola usiingie hapa nchini!! Amen
 
shaka ondoa BAK na Gefu idara husika wamejipanga. ishu kubwa hapa kwetu kuna wale wenzetu wanao pita njia za panya hao ndio watakao tuletea.

umeskia madereva wa malori wamepewa angalizo sasa sijui wangapi watakao chukua hatua
 
Last edited by a moderator:
Wadau huu ugonjwa unazidi kuenea na kusambaa kwa kasi sana. Nigeria, ethiopia na nchi nyingine zimechukua hatua kali za tahadhari kuzuia tishio la ugonjwa huu. Ukizingatia urahisi wa kuambukizwa,ugumu wa kutofautisha dalili zake na magonjwa mengine, na ukweli kwamba congo si mbali na 90% wanaoambukizwa wanafariki wakiwemo madaktari bingwa. Kwa tishio hili nilitarajia sirikali ingechukua hatua za tahadhari mapema na kuwaelimisha wananchi juu ya tishio hilo. Serikali imekomaa na IMTU na mafuvu badala ya kuhangaikia wale walio hai. Em sirikali kuweni siliasi basi hii ngoma ikiingia bongo mpaka ije kuisha tushaumia sana..

Wako makini usiwe na wasiwasi
 
Back
Top Bottom