Zawadi Ngoda
JF-Expert Member
- Aug 13, 2009
- 3,804
- 1,871
Kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sio lelemama, ni lazima uwe umekamilika katika nyanja zote. Ninaelewa kuwa kila mmoja wa watanzania takriban 40 mil, angependa kuwa raisi wa Tanzania japo kwa siku moja katika maisha yake. Lakikini hali halisi sio hiyo.
Mheshimiwa Slaa ni mbunge ninayemheshimu sana, lakini kugombea kiti cha urais ni utani uliokithiri. Mapungufu aliyekuwanayo ni makubwa, kama nikiyaorodhesha yote basi mtachoka hata kusoma, na bado sijaeleza mapungufu ya chama CHADEMA. Mapungufu mawili ya Slaa ni kuwa na elimu ya jicho moja, nikimaanisha kuwa ana elimu isiyo na upeo wa kuwaelewa na kuwakubali watanzania wote(usiponielewa mpaka hapo niulize nitakufafanulia). Pungufu la pili ni mtu asiyeelewa au kuwa na vision ya uchumi, kitu ambacho ni changamoto kubwa ktk nchi yetu sasa hivi. Na pungufu la tatu si la Slaa bali ni la chama chake, ambalo ni kushindwa kuwa na wabunge wa kutosha kumuunga mkono puindi atapokuwa Raisi. Ni dikteta peke yake anaweza kuongoza nchi akiwa na chini ya 20% ya wabunge wa nchi nzima, kitu ambacho CHADEMA haiwezi kuzidi namba hiyo.
Hatutaki vurugu tunataka muendelezo wa demokrasia, madhara ya kujaribu kuwa Rais bila uwezo ni makubwa sana, tunaona yanayotokea huko Madagaskari 'Demokrasia bila Amani'
Ushauri wangu kwa Slaa: Jitoe ktk kugombea urais na badala yake saidia kupiga kampeni ya wabunge katika majimbo mbali mbali. Urais hutauweza kamwe na ni hatari kwa nchi yenye martaumaini kama TZ. Hatuhitaji Revolution bali tunahitaji Evolution kutokana na matatizo yaliyopo Tanzania.
Mheshimiwa Slaa ni mbunge ninayemheshimu sana, lakini kugombea kiti cha urais ni utani uliokithiri. Mapungufu aliyekuwanayo ni makubwa, kama nikiyaorodhesha yote basi mtachoka hata kusoma, na bado sijaeleza mapungufu ya chama CHADEMA. Mapungufu mawili ya Slaa ni kuwa na elimu ya jicho moja, nikimaanisha kuwa ana elimu isiyo na upeo wa kuwaelewa na kuwakubali watanzania wote(usiponielewa mpaka hapo niulize nitakufafanulia). Pungufu la pili ni mtu asiyeelewa au kuwa na vision ya uchumi, kitu ambacho ni changamoto kubwa ktk nchi yetu sasa hivi. Na pungufu la tatu si la Slaa bali ni la chama chake, ambalo ni kushindwa kuwa na wabunge wa kutosha kumuunga mkono puindi atapokuwa Raisi. Ni dikteta peke yake anaweza kuongoza nchi akiwa na chini ya 20% ya wabunge wa nchi nzima, kitu ambacho CHADEMA haiwezi kuzidi namba hiyo.
Hatutaki vurugu tunataka muendelezo wa demokrasia, madhara ya kujaribu kuwa Rais bila uwezo ni makubwa sana, tunaona yanayotokea huko Madagaskari 'Demokrasia bila Amani'
Ushauri wangu kwa Slaa: Jitoe ktk kugombea urais na badala yake saidia kupiga kampeni ya wabunge katika majimbo mbali mbali. Urais hutauweza kamwe na ni hatari kwa nchi yenye martaumaini kama TZ. Hatuhitaji Revolution bali tunahitaji Evolution kutokana na matatizo yaliyopo Tanzania.