Tanzania said nothing about Trump election!

Tanzania said nothing about Trump election!

Wanaochukua madini ya kongo unawajua?
Kwa hiyo majeshi yetu yako Kongo kwa ajili ya Kulinda wezi toka Marekani ?
.....Kama tatizo ni hao wezi tena wazungu wa Magharibi ,kwa nini Majeshi yetu yasiwachakaze hao wezi mchezo ukaisha?
Acheni utani bhana.
.....Vita za Afrika zinatokana na viongozi waroho wa madaraka wanaotumia majeshi kuua watu na kutesa watu kwa sababu ya kupenda kufia madarakani na rafiki na ndugu zao.
Demokrasia ya kweli na haki sawa itaondoa vita dunia. Mana kila MTU ataipenda nchi yake kwa moyo wote.

Jiongeze acha siasa za kujenga chuki dhidi ya binadamu wenzako.

Dunia ilishaondoka huko kwenye hizo siasa ndio maana Ufaransa inageuka kuwa Tawi la Bara la Afrika.
Watu wanaishi popote alimradi kuna Uhuru na kujali haki na utu wa wanadamu.

Hii mambo ya kuona kuwa wazungu ni wezi tu ni ujinga na Propaganda za kijinga za kuhalalisha uhalifu dhidi ya binadamu.

Watu wanatuonya kuwa hayo tunayoyafanya yatapoteza amani ya nchi yetu na kuruhusu wezi kuvamia nchi yetu badala yake tunakua wakali badala ya kurekwbisha makosa ili tuwe na amani zaidi.

Ukweli ni kwamba Watanzania tukipendana na kuungana bila kubaguana hakuna Muzungu wala Muchina atakayeivamia nchi yatu na kuiba rasilimali zetu milele. Lakini tukichukiana na kulazimisha watu wanaovaa nguo za rangi Fulani tu ndio wafaidi mema ya nchi sidhani kama tutafikia kuzuri.
Sioni sababu ya kutisha ,kuteka ,kutesa ,kujeruhi na kuua ndugu wa jamaa moja kwa sababu tu ya madaraka ya kulazimisha mtu mmoja kushinda uchaguzi kwenye Kata au jimbo.


Mchawi wa Afrika ni Waafrika wenyewe wala sio nchi za Magharibi.
 
Basi acheni kuvipokea maana naona kune eneo fulani vinatumika kufunika vifaranga wachanga
Mkuu umenena ngoja nikuwekee bango la usia wa baba wa taifa.
downloadfile-6.jpg
 
Kwa hiyo majeshi yetu yako Kongo kwa ajili ya Kulinda wezi toka Marekani ?
.....Kama tatizo ni hao wezi tena wazungu wa Magharibi ,kwa nini Majeshi yetu yasiwachakaze hao wezi mchezo ukaisha?
Acheni utani bhana.
.....Vita za Afrika zinatokana na viongozi waroho wa madaraka wanaotumia majeshi kuua watu na kutesa watu kwa sababu ya kupenda kufia madarakani na rafiki na ndugu zao.
Demokrasia ya kweli na haki sawa itaondoa vita dunia. Mana kila MTU ataipenda nchi yake kwa moyo wote.

Jiongeze acha siasa za kujenga chuki dhidi ya binadamu wenzako.

Dunia ilishaondoka huko kwenye hizo siasa ndio maana Ufaransa inageuka kuwa Tawi la Bara la Afrika.
Watu wanaishi popote alimradi kuna Uhuru na kujali haki na utu wa wanadamu.

Hii mambo ya kuona kuwa wazungu ni wezi tu ni ujinga na Propaganda za kijinga za kuhalalisha uhalifu dhidi ya binadamu.

Watu wanatuonya kuwa hayo tunayoyafanya yatapoteza amani ya nchi yetu na kuruhusu wezi kuvamia nchi yetu badala yake tunakua wakali badala ya kurekwbisha makosa ili tuwe na amani zaidi.

Ukweli ni kwamba Watanzania tukipendana na kuungana bila kubaguana hakuna Muzungu wala Muchina atakayeivamia nchi yatu na kuiba rasilimali zetu milele. Lakini tukichukiana na kulazimisha watu wanaovaa nguo za rangi Fulani tu ndio wafaidi mema ya nchi sidhani kama tutafikia kuzuri.
Sioni sababu ya kutisha ,kuteka ,kutesa ,kujeruhi na kuua ndugu wa jamaa moja kwa sababu tu ya madaraka ya kulazimisha mtu mmoja kushinda uchaguzi kwenye Kata au jimbo.


Mchawi wa Afrika ni Waafrika wenyewe wala sio nchi za Magharibi.
Wakati wa Mkapa CUF na NCCR ililalamika eti hakuna demokrasia...
Wakati wa Kikwete Chadema ikaendelea kulialia eti hamna demokrasia na Rais ni dhaifu...wakati huu mnalalamika eti mnanyimwa haki...
Acheni utoto wa kujificha kwenye kichaka cha neno "demokrasia"
eleweni kuwa hata hao mnawatumia video clips na picha ili watoe matamko hawana hiyo demokrasia mnayoitaka.
 
Vita za Afrika zinatokana na viongozi waroho wa madaraka wanaotumia majeshi kuua watu
Cia imemuua Lumumba,Mondlane,Kwame,Abdelnaser,Machel,Sankara, hawa ni baadhi tu ya wazee wetu.

Hizo data za kupikwa sijui umezitoa wapi.
 
Siku zote mwenye mbwa ndio anaongea.

Usisahau USA ndio wanatulisha, kutupatia hela za misaada na mikopo. Ufadhili wa madawa, na mambo kama hayo.

Tanzania haijawahi kuisaidia USA msaada wowote hata wa unga wa muhogo debe moja.

Siyo hayo tu yako mengi. Wahega waliposema USITUKANE MAMBA KABLA YA KUVUKA MTO hawakuwa wajinga ....Kuna hili la kuweka order ya kutengenezewa Dreamliner....Mmarekani ndiyo anayetutengezea kuonyesha tu kwamba nyie kama Tanzania tunawategemea Wamerekani kwa kiiiila kitu...!! Hivi Marekani wakiammua waweke intelligence devices za kuwa zinapeleka siri zote za Tanzania mna ubavu wa kudhibiti hiyo hali..?
 
Siyo hayo tu yako mengi. Wahega waliposema USITUKANE MAMBA KABLA YA KUVUKA MTO hawakuwa wajinga ....Kuna hili la kuweka order ya kutengenezewa Dreamliner....Mmarekani ndiyo anayetutengezea kuonyesha tu kwamba nyie kama Tanzania tunawategemea Wamerekani kwa kiiiila kitu...!! Hivi Marekani wakiammua waweke intelligence devices za kuwa zinapeleka siri zote za Tanzania mna ubavu wa kudhibiti hiyo hali..?
Sio tunatengenezewa bure...tunanunua tena kwa cash....na wakiweka hivyo vifaa ni breach ya privacy ya abiria popote itakapoenda usiishi ki-utopia
 
Marekani ndio taifa la kwanza kwa kuua ndugu zetu waarabu.
 
Wameingilia Mambo ya ndani vipi?
Kuna mahali FBI wamemkamata kada wa CCM / Msimamizi wa Uchaguzi aliyevuruga Uchaguzi ?
Kuna mahali wameleta askari wa marekani kusimamia Uchaguzi wetu?
Nyie vipi?
Tuwapende na kuwatetea watanzania wenzetu wanaodhulumiwa kwa sababu ya baadhi ya wenzetu wenye uroho wa kupata sifa na madaraka?

Huo ndio ujinga unaofanyika Kongo. Wanashindwa kukaa pamoja na kuaminiana kwa ajili ya kuijenga Kongo nchi yenye rasilimali nyingi duniani badala yake kila siku ni kuvuruga Uchaguzi na kuuana kwa ubinafsi na uroho wa Madaraka.

Huyo unayemueleza haya ni mfaidika wa hii awamu. Hivyo anatumia muda wake wote kutetea hadi maovu kwani anajua utawala huu ukiondoka madarakani naye ni mwisho wake wa ulaji. Kumezuka mtindo wa kupotosha ukweli na kutengeneza uzuri wa maisha ya Watanzania kupitia vyombo vya habari, na inapotokea wananchi wakataka kuonyesha hisia zao hasa kwenye box la kura ndio unakuta unafanyika ukatili wa wazi kulazimisha kukubalika.
 
Basi kuna haja mpaka kwenye uchaguzi wa serekali za mitaa wawatume waangalizi wa kimataifa.
 
Serikali hii inatakiwa ijitafakari kama bado imebakiwa hata na 'Residue' ya Mandate ya wananchi wa nchi hii.

Make sasa hakuna tena sababu ya mtu /watu wenye akili zao kupoteza muda kwa kuungua juani eti kusubiri kupiga "Kura", kwani hii nchi hakuna tena uchaguzi kwani yanayofanyika sasa ni utaahira mtupu kama sio uhuni.
 
Cia imemuua Lumumba,Mondlane,Kwame,Abdelnaser,Machel,Sankara, hawa ni baadhi tu ya wazee wetu.

imhotep,

Usitake kupotosha historia kama hujui nyamaza kimya kuliko kubwabwaja uharo wako hapa!!
Kina Lumumba, Mondlane, Machel,Nkrumah waliuawa na Makaburu na Wareno waliokuwa wanazitawala nchi zao kikolone. Abdel Gamal Nasser aliuawa na Waisrael kutokana na vita vya Mwarabu na Mwisrael. Thomas Sankara aliuawa na Waburkinabe wenyewe ambao ni maadu zake.
Je, kwa Tanzania .nani kawaua hawa: Edward Moringe Sokoine, Amani Karume,Imran Kombe, Horace Kolimba,Ben Saanane,n.k.

Hivi unaweza kuelezea mazingira ya kifo cha Baba wa Taifa baada ya kukatishwa uhai wake na baadhi ya vigogo wa CCM baada ya kutofautiana wakti alipong'atuka? Kabla Mwalimu hajaaga dunia aliwahi kusema CCM SIYO MAMA YAKE na alikuwa na msimamo mkali kuhusu KUZIKWA KWA AZIMIO LA ARUSHA pamoja na hata SERA ZA BEN MKAPA ZA UGENISHAJI na alizipinga kwa nguvu zote.....jamaa wakaona isiwe noma wakamaliza mchezo....!
 
Lumumba you have to put sanctions against USA, they have to commense immediately. all the Best Lumumbas
 
Ndio maana tunataka tuondokane na huo mtego maana wanabwata kwa kutusaidia pedi za wake zetu!
Sio kwa namna hiyo ya kutofuata Katiba na sheria tuliojiwekea wenyewe.
Watakuja wengine miongoni mwetu na kutawala halafu watafukua makaburi ya watu waliendesha nchi bila kufauata sheria .

Lowassa anapata tabu sana kwa sababu tu alikiuka sheria za kuingilia mchakato wa Kumpata mzabuni.
Hilo tu lilisababisha wapinzani wake kisiasa kuamua kumshughulikia wakaiongozwa na Mzee wa kunyoa watu kwa chupa.
Leo hii hayo bado yanafanyika tena kwa zabuni kubwa za matrioni ya fedha achana na ile ya Lowasa ya kajenereta ka vijisenti. Watu wanakiuka taratibu na sheria za. Zabuni na manununzi tulioziwekea wenyewe.

Sasa wanachofanya ni kuufuta upinzani ambao ndio wanaoibua udhaifu ,ufisadi na upigaji mkubwa unaofanywa na watendaji wakuu wa Serikali kupitia zabuni za mabilioni.
Hayo pia anayafanya Mbowe kwa kuwashughulikia wapinzani wake ndani ya chama wanaohoji matumizi,manunuzi na zabuni ndani ya chama.
Sasa hapo ubaya ni wa nchi za magharibi au watendaji wetu ambao wengi wao sio waaminifu ndio maana hawataki watu wa kuwakosoa kwa wazi?
 
Sio tunatengenezewa bure...tunanunua tena kwa cash....na wakiweka hivyo vifaa ni breach ya privacy ya abiria popote itakapoenda usiishi ki-utopia

Wewe utaendelea kuwa jingalao tu!!
Sijasema unatengenezewa bure wala kununua kwa cash kama Tanzania haikusaidii or to add any value. Kama wewe huna huna teknolojia hata ungekuwa na hela za madafu kwa mabilioni haikusaidii lolote bado utampigia magoti Mmarekeni akutengezee Bombadier kwa hela yoyote atakayoamua? The technology is so advanced nowdays, hivo usishangae kama USA akikuwekea vifaa ambavyo vitashughulika na wewe tu kama Mbongo bila kugusa abiria wa Mataifa mengine....Try to think out of the box!
 
Huyo unayemueleza haya ni mfaidika wa hii awamu. Hivyo anatumia muda wake wote kutetea hadi maovu kwani anajua utawala huu ukiondoka madarakani naye ni mwisho wake wa ulaji. Kumezuka mtindo wa kupotosha ukweli na kutengeneza uzuri wa maisha ya Watanzania kupitia vyombo vya habari, na inapotokea wananchi wakataka kuonyesha hisia zao hasa kwenye box la kura ndio unakuta unafanyika ukatili wa wazi kulazimisha kukubalika.
Hivi umeingia lini JF?Wanaopotosha ukweli wanajulikana ...na walikuwa wakifanya hivyo in past 10 years toka enzi za JK mlifanya upotoshaji kwa manufaa ya kujenga chama chenu.
 
The plot against Lumumba is a classic example of American policy out of control - an assassination attempt launched by the C.I.A.
Mzalendo feki soma New york times la Marekani.
 

Vitabu vya dini vinasema siku za mwisho WATADANGANYA NA KUDANGANYIKA......!!!Wewe endelea kudanganya wajinga wenzako na kujidanganya mwenyewe lakini huwezi kudanganya watu wote kwa wakati wote hasa tunaojitambua.
Marekani haijawahi kuwa na koloni lolote hapa Afrika...!Nchi zilizokuwa na makoloni Afrika zinajulikana na kama hujui uliza.
 
Vitabu vya dini vinasema siku za mwisho WATADANGANYA NA KUDANGANYIKA......!!!Wewe endelea kudanganya wajinga wenzako na kujidanganya mwenyewe lakini huwezi kudanganya watu wote kwa wakati wote hasa tunaojitambua.
Marekani haijawahi kuwa na koloni lolote hapa Afrika...!Nchi zilizokuwa na makoloni Afrika zinajulikana na kama hujui uliza.
Soma #118 nikipe Link.
 
Back
Top Bottom