Aidha, wametamka wazi kwamba, wana haki ya kutumia bendera ya JMT kwakuwa ZNZ nayo ni sehemu ya muungano. Lakini pamoja na kuwa na mamlaka hayo, wao wametamka wazi kwamba hakuna meli yoyote ya Iran ambayo ama wameisajili wao moja kwa moja au kupitia kwa wakala wake aliyepo Dubai.
Na hata ukiisoma vizuri hiyo barua ya Berman, wala hawajasema kwamba hiyo meli imesajiliwa Tanzania bali inapeperusha bendera ya Tanzania. Hapo kinachoonekana ni speculation tu toka USA kwamba provided meli hizo zinapeperusha bendera za TZ basi kuna uwezekano kwamba zimepata baraka kutoka TZ ama kusajiliwa TZ!!
Kinyume chake, haigharimu chochote kwa meli yoyote kupeperusha bendera ya nchi yoyote!!! Zile bendera ni vitambaa tu na sizani kama zina security mark yoyote ambayo mtu anaweza kuhoji ilikuwaje hadi wahusika wakapata bendera yenye security mark.
NasDaz,
..Zanzibar hawana haki ya kupeperusha bendera ya Tanzania kwenye masuala yasiyo ya muungano.
..kama suala hili la usajili wa meli halina mahusiano na muungano basi Zanzibar walipaswa kupeperusha bendera yao.
..Siku zote Zanzibar wanalilia kuwa huru na kujiamulia mambo yao wenyewe. Sasa ktk hili la kusajili meli za wa-Iran wameshindwa nini kuji-assert na kupeperusha bendera yao??
Umeona, eeh? Sasa unaelewa ni kwa nini Bush alikuja na ataendelea kuja Tanzania. Siyo kwamba anatutakia mema.
Amewekeza mirija yake huko.
Ni kweli Barrick ilianza kuchimba wakati wa Mkapa. Lakini mikataba ilisainiwa wakati wa Mwinyi. And guess what? Nani alikuwa waziri wa madini na nishati wakati wa Mwinyi?
Kwavile USA inafahamu kwamba TZ ni nchi huru yenye haki ya kujiamulia mabo yake;
By the way, bado nasisitiza kwamba kupeperusha bendera ya nchi yoyote sio issue; hata dala dala zetu za Tandika ndani unakuta bendera za nchi mbalimbali including US.
ndumila kazini! Nyerere alikuwa aidha baridi au moto lakini siyo vuguvugu!
Haya ndio matunda ya kuwa Omba Omba.... Lazima tuwe na mtazamo tofauti na taifa letu. Check tunavyodharauliwa, Ranking officer writing to the President of United Republic of Tanzania? I was expecting President Barack Obama and not otherwise... :shetani:
Kwenye suala la bendera nimekuelewa.....na ofcoz, suala la usajili wa meli sio la kimuungano kwahiyo kama upo right, then isn't right kwa znz kupeperusha bendera za JMT kwa meli ambazo imezasajili kupitia SMZ. Lakini hoja ya msingi hapa ni kwamba, ZNZ wamekanusha kusajili meli yoyote ya Iran.....labda kama unataka kuniambia SMZ imedanganya!!! Na ndio maana hoja yangu ipo pale pale kwamba, hata kama meli hizo hazijasajiliwa na mamlaka halali ya JMT/SMZ, bado haiwezi kuwa shida kwao kupeperusha bendera ya JMT.
Sana sana ninachokiona kwenye barua hiyo ni silika waliyonayo baadhi ya watu. Kuna baadhi ya watu wana silika ya ajabu sana...watu wa aina hii endapo wanahitilafiana na baadhi baadhi ya watu, basi wanataka wale wote wanaoshirikiana nao nao wawe wahitilafiane na hao watu!!! Yaani, ikwa JokaKuu, FJM na Jasusi ni maswahiba, na mara JokaKuu akaingia kwenye mgogoro na NasDaz, basi hapo JokaKuu atatamani FJM na Jasusi nae wamnunie NasDaz!!!!! Lakini JokaKuu akiona JFM na Jasusi wanacheka na kunywa pamoja, JokaKuu atachukia....!!! Sasa kama sio wehu tuite nini?! Hapa kinachoonekana ni kwamba, pamoja na kwamba USA inaisaidia sana TZ na kumpa JK heshima ya kwenda kwao mara kwa mara; lakini bado TZ haitaki kununua kesi ya USA na Iran...!! Kwavile USA inafahamu kwamba TZ ni nchi huru yenye haki ya kujiamulia mabo yake; ikakosa sababu ya kuitaka TZ ivunje uhusiano na Iran. Hivyo, ilipotokea issue ya bendera, ndipo ikaona "hapa hapa" waeleze hisia zao za kutofurahishwa na kitendo cha TZ kuendelea kuwa na uhusiano na Iran Bila shaka furaha ya USA ni kuona nchi zote zenye uhusiano mzuri na wao(USA) basi zinunue kesi za USA zote na kuzifanya zao!!
Sana sana ninachoweza ku-conclude hapa ni kwamba, hawa USA waache upuuzi wao unless wa-prove beyond reasonable doubt kwamba meli hizo zimepata baraka halali toka URT/SMZ na kwamba URT/SMZ wamevunja vipengele HALALI vya UN, otherwise waache kutishia watu hapa. By the way, bado nasisitiza kwamba kupeperusha bendera ya nchi yoyote sio issue; hata dala dala zetu za Tandika ndani unakuta bendera za nchi mbalimbali including US.
Oh, Kikwete
Yasije tukuta jamani,marekani ndio kilakitu kataa kubali,kama neti tu mpaka marekani,tangazo dogo tu kwa hisani ya marekani,ukichukiwa na marekani hakuna atakae kupenda,kubali kataa marekani ndio boss
Kumbe hawezi chomoka maana akisema mikataba haijasainiwa kwenye awamu yake kam Rais tutamwambia ilisainiwa kipindi ni waziri utawala wa Mwinyi