Tanzania Labour Law (Sheria ya Kazi Tanzania)

Buswelu

JF-Expert Member
Aug 16, 2007
1,998
352
Mkataba wa ajira, kama ilivyo desturi kwa mikataba mingine kwa mujibu wa sheria, huzaliwa, huishi na kufa; kama ilivyo kwa binadamu na viumbe hai vingine.

Unazaliwa mara baada ya mwajiriwa na mwajiri kutia saini zao. Hapo ndipo wanapouanzisha, utekelezaji wake unapoanza kuchukua hatua na kifo ni pale tu yanapoanza kujitokeza baadhi ya mambo au masuala yanayoainishwa na sheria.

Aidha, zipo taratibu maalum za kumaliza au kuua mkataba wa ajira na hii ni katika mazingira yote, iwe kwa hiari na yale ya kumaliza kwa kulazimika kulingana na sababu mbalimbali.
Kumalizika au kukoma mkataba wa ajira kwa hiari au kufikia ukomo wa kazi kulingana na wepesi wa kutekeleza majukumu ya kazi yenyewe.

Kanuni ya 4 (1)-(7) na ya 5 (1)-(5), zote ni Kanuni za Ajira na Mahusiano Kazini, Kanuni za Utendaji Bora za Mwaka 2007, zinaeleza hakuna shida kama ilivyo kumaliza, kukoma mkataba wa ajira kwa kulazimika kutokana na sababu mbalimbali za kinidhamu.

Katika uhusiano kazini, jambo mojawapo linalomfukuza mtu kazi au kusababisha kukoma mkataba wa ajira, ni utovu wa nidhamu. Hiyo ni mojawapo, kati ya sababu za msingi zinazoweza kumfanya mwajiriwa au mfanyakazi kupoteza ajira yake.

Kimsingi, kanuni hizo zinaelekeza kuwa ni sahihi kumfukuza mfanyakazi kwa sababu za kinidhamu, lakini haimaanishi kuwa mwajiri amtafutie mwajiriwa kisa cha kuzusha au kupika, ili kumwondoa kazini.
Kinachosisitizwa hapa, ni lazima sababu hizo ziwe zimejitokeza na kuthibitika kweli na ziweze kuthibitishwa pale itakapotakiwa kufanyika hivyo.

Ujenzi wa hoja kwa kushikilia mkazo kuwa nilisikia au nahisi, zitasababisha tuhuma hizo kukosa mashiko mbele ya msuluhishi, hakimu au jaji kutegemeana na shauri lilikofika.

Kanuni ya 8 (1)(d) na 12 (1)-(5), zote za Ajira na Uhusiano Kazini na Kanuni za Utendaji Bora za mwaka 2007, sanjari na Kifungu cha 37 (2), Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini, 2004 Sura ya 366, zote zinasisitiza ukweli na uthibitisho wa madai yanayotolewa.

Angalizo ni kwamba, sheria inaelekeza kuwa mwajiriwa au mfanyakazi, atafukuzwa kazi mara moja, bila ya hata kupatiwa barua ya onyo kwa kosa la mara ya kwanza au “summary dismissal”.

Kwa utaratibu huo, imafanya mwajiriwa, au mfanyakazi kupoteza haki zake zote za msingi kama kiinua mgongo. Kifungu cha 42 (1)-(4) cha Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini ya mwaka 2004 Sura ya 366 inalifafanua hilo.

Hivyo basi, ni kosa kwa mwajiri kumfukuza mfanyakazi kwa utaratibu wa mara moja, yaani ‘summary dismissal, isipokuwa kama hilo litafanyika katika mazingira ambayo sheria inaruhusu wazi kufanya hivyo na siyo kinyume chake.
Kifungu cha 41 (1)-(7) cha Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini ya 2004 sura ya 366 ina ufafanuzi.

Haki ya Kusikilizwa
Kila mtu ana haki ya kusikilizwa, kabla hatua ya kisheria kuchukuliwa. Ni haki ya asili, ambayo haiwezi kuondolewa na mtu au mamlaka yoyote ile. Kwa maana hiyo, pasipo kujali ukubwa wa kosa, hata kama kosa la mwajiriwa, mhusika anapaswa kupewa nafasi ya kutoa utetezi wake.

Atajitetea na kutakiwa kuwasilisha utetezi wake, dhidi ya: “Kwanini asichukuliwe hatua za kinidhamu?” Kanuni ya 13 (1)-(13) Kanuni za Ajira na Uhusiano Kazini, 2007 inaeleza.

Ni kosa kwa mwajiri au mkuu wa kazi kumfukuza mfanyakazi, bila ya kumpatia nafasi ya kumsikiliza au kujitetea. Hii siyo hiari ya mwajiri kuamua kumpatia mwajiriwa haki husika, bali ni haki ya msingi. Hiyo ni kwa sababu, haki yenyewe ipo kwa mujibu wa sheria, hivyo utekelezaji wake ni lazima.

Haki ya Malipo Stahiki

Kifungu cha 44 (1)(a) cha Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini ya mwaka 2004, Sura ya 366, kinaelekeza haki za msingi alizo nazo mwajiriwa atakayefukuzwa kazi, kutokana na sababu za kinidhamu. Hiyo ni pamoja na kulipwa mshahara au ujira wake.

Mshahara utalipwa kwa kuzingatia tarehe ya mshahara wa mwisho mpaka siku ambayo mwajiriwa amefukuzwa, mathalan kama tarehe ya mwisho ya kupokea mshahara itakuwa Juni 30, 2019, kisha mhusika atafukuzwa Julai 17, 2019; pesa itakayotolewa ni kwa kuzingatia siku ambazo mhusika amefanyakazi. Yaani jumla ya siku 17 kuanzia tarehe 1 hadi 17 Julai. Inatajwa kuwa haki ya msingi, wala isipuuzwe kulinda maslahi ya pande zote mbili.

Ingia hapa ujisomee sheria ya ajira na mahusiano kazini

Sheria ya ajira na mahusiano kazini

==============

Michango ya wadau

----
----
----
 
Mkuu Buswelu,

Thanks very much for this.....! one of the very interesting sections is 34(1)(a)-(b) on Paternity Leave! I have just copied this;

During any leave cycle, an employee shall be entitled to-

(a) at least 3 days paid paternity leave if-
(i) the leave is taken within 7 days of the birth of a child;
and
(ii) the employee is the father of the child;

I think the law is not fair by giving just 3 days for the father to be with the new baby and its mother. The father needs enough time to stay together with the new family, help through the wife who needs to rejuvenate after many weeks of pregnancy and tough delivery job. At least the father should have been given 7 clear working days for this reason.

Mkuu Buswelu;

Nilisikia kitu kama mwaka jana kuna regulations mpya kuhusu malipo ya likizo kwa wafanyakazi wa sekta mbalimbali....vipi utakuwa na copy ya hii kitu?
 
Hii ni kati ya documents anazopaswa kupewa mfanyakazi anapoajiriwa. Sasa sijui kama ndivyo hivyo.

Mkuu,

Labda developed world....bongo sijui.....! Mimi nimeshabadilisha ajira kama mara tatu hivi tangia ni graduate, lakini hakuna hapa Employer mmoja aliye nikabidhi msahafu huu....nafikiri kwa sababu waajiri wengi hawapendi kufuata hizi sheria za kazi so sitashangaa kuona hawawapi copy waajiriwa wao!
 
wanajamii naomba kuuliza hivyi ikitokea mwajiri kakulipa msharaha kimakosa (yani kazidisha amount fulani katika mshahara wako kwa mda wa zaidi ya miezi 2) je ni sahihi mshahara wako kushushwa tena kama hilo kosa lilikuwa la mwajiri. je sheria ya kazi inasemaje kuhusu hilo wanasheria tunaomba mtutafsirie.
 
Pengine nifafanue kuwa sheria ime-provide minimun standards. na ndicho kilichoandikkwa hapo juu " at least 3 dayspaid paternity leave..."

Nini maana yake. Sheria imejaribu kutoa standards ambazo kila mwajiri atweza kuzimudu na kuzitekeleza kwa urahisi hat sisi ambao tuwa wadsaidizi wa ndani mna siku zote uwa tujajisahau ama kufikiri siyo waajiri kama makampuni.

Kwa mantiki ya sheria ni kuwa wafanyakazi kupitia vyama vyao (trade unions) au mabaraza ya mashauriano wanaweza kuongea na mwajiri wao na hiyo paternity leave kuwa siku 10 au 15 au 20 au vyovyote vile ambapo pande mbili kati ya mwajiri na wafanyakazi wataweza kuridhia.

Tatizo ninaloliona na ni la uzoefu ni kuwa wafanyazi wanachua tafsiri kuwa sheria imetoa siku 3 bila kujali ama kuangalia kuwa iko ni kiwango cha chini ambacho mwajiri endapo hatakiuka basi anaweza kuchukuliwa hatua kwa kushindwa kutekeleza mahitaji ya kisheria (minimum standard). kwa upande wa pili ni kma nilivyodokeza hapo juu, endapo sheria ingetoa siku 10, au 20 then ingekuwa tatizo kubwa kwetu sisi waajiri wa majumbani kwa mzigo wa utekelezaji wake ungekuwa mgumu hasa ukizingatia ukweli kuwa hat mimi mwenye kipato cha laki moja nikiwa na hoseboy ni mwajiri ya tayari, sasa ikiwa nimpatie 20 days paid paternity leave sidhani kam nitaweza au wote wenye kipata cha aina hiyo tutaweza kutekeleza sheria husika.
 

Hapa swali lako limekaa kimtego kidogo. Lakini kama nimekuelewa vizuri, unazungumzia makosa ya payroll tu. Na sio kwamba mwajiri amekupa kabisa barua ya increment then anataka kushusha mshahara after two months. Kama ni overpayments due to payroll errors, mwajiri anaruhusiwa kukukata hiyo overpaid amount provided that the total deductions does not exceed one quarter of your salary.

Section 28(5) of the ELRA 2004 states that; An employer shall not require or permit an employee to (a) repay any remuneration except for overpayments previously made by the employer resulting from an error in calculating the employee's remuneration.

So, deductions zinaruhusiwa kisheria kama kweli kuna kosa la overpayments.
 
Hii inabidi kuwa nayo kwenye hali tete kama kule North Mara kwa sasa wanavyo punguza wafanyakazi kwa kisingizio cha GFC, huwezi jua wanatumia kigezo gani..wakati wanaacha expart 12 kwenye kitengo kimoja.

Wa nini..kwa kawaida Expart moja anatakiwa kuwa na watu wa chini yake 6 mpaka nane, sasa department ina wafanyakazi 30 Expart 12 wa nini?Harafu unataka punguza nationals..
 
Asante sana Mkuu Buswelu. Ni leo asubuhi tu, nilikuwa natafuta hii Labour Law bila mafanikio.

Shukrani sana Mkuu.

JF forever.

wandugu, msihangaike kutafuta sheria. sheria zote za tz kuanzia mpya hadi za zamani, zipo kwenye website ya parliament of tz. nenda kule utaipata kwenye pdf. nashangaa wengine wanasema walikuwa wanatafuta sheria hizi, wakati ziko wazi sana, tena mno.
 

kukabidhiwa is one thing....na kuusoma je?

nani hata huwa anjisumbua kusema nikatafuta sheria ya kazi ili nijue haki na wajibu wangu kama mwaajiriwa??
Of coz hata wewe ungekuwa mwajiri ungetumia viudhaifu vya dizaini hiyo kuwabania watu
ukweli ni kwamba wengi wetu hatupendi kujishughulisha hata kwa mambo ambayo ni ya manufaa kwetu...
after all mwajiri hana obligation ya kukupa huu msaafu anapokuajri, unabaki kuwa wajibu binafsi tu.......
 

Lakini iko haja ya kuijua sheria ya kazi
hapa nilipo Contract ya job na msaafu unakabidhiwa ..
 
Lakini iko haja ya kuijua sheria ya kazi
hapa nilipo Contract ya job na msaafu unakabidhiwa ..

haja ipo my dear tena bila kupingwa

duh hiyo ya kukabidhiwa msaafu ofisi chache zinafanya......safi sana
 

Just wanted you to know that the law you menitioned (see my highlight) says that you are entilteld to at least 3 days. This is the minimum number of days. Each organisation is entitled to increase the number. I know of organisation here in TZ who have seven days partenity leave and other who have 14 and even some embassies which have 28 days.

Ni vizuri sana wakati wafanyakazi wananegotiate voluntary agreements to argue for more inclusion of the days.
 

In actual sense you are supposed to demand it. Hawewezi tu kukupa unless wanafollow employment best practices.
 
Jamani nisaidieni kupata "Public service Regulations 2003 nimeangalia website ya bunge haipo.
Natanguliza shukurani
 
Nimesikia kuna labour law(mpya) inasema kuwa mwanamke anaruhusiwa kwenda martenity leave ya miezi mitatu hata kama hajamaliza miaka mitatu toka martenity leave iliyopita. Mwenye kujua naomba aniambie ni kipengele namba ngapi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…