Ndugu zet wa Zanzibar ni watu wa ajabu kidogo.
Walibadili katiba yao na kuifanya kukiuka katiba mama ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Waziri Mkuumstaafu Pinda alijaribu kuwaonya juu ya hatari hii ya kikatiba.
Wao wakaishia kumnanga kuwa hatambuliki Zanzibar na asiingilia mambo muhimu ya Wazanzibari.
Pinda akaufyata, na sijui kama aliwahi kutembelea huko Zanzibar.
Leo kwa kiburi kile kile cha Uzanzibari Mwenyekiti wa ZEC, Tume ya Uchaguzi Zanzibar ameufutilia mbali uchaguzi huko Zanzibar.
Hakuna wa kumuingilia
Zanzibar ni Nchi ati.
Leo tunamuona Maalim Seif akitoa povu ati na uchaguzi wa Tanzania Bara nao usimamishwe!
Tume ya Lubuva ilimkanusha haraka sana, na ni kama ilisema hilo ni suala la Zanzibar kwa mujibu wa katiba yenu.
Nami nasema Wazanzibari huu uozo wa ki katiba mliutengeneza wenyewe, mlinywe.
Mwalimu alisema, tena prophetically, hawa wazanzibari wakiamua kujitenga na kuwabagua watanzania bara, watapata matatizo , na leo tunayaona live.