Tanzania kushirikiana kijeshi na Iran

Inasemekena Tz kuna Uranium na Iran anahitaji sana hiyo resource

Inaoenkana kila anayetaka kuwa Rais Tz ni muhimu kuwa karibu na Iran

......of all the countries!!!.....Iran!!.......give me a break!!......damn

Naamini Tanzania ni nchi isiyofungamana na nchi yoyote na tuna uhuru wa kuangalia lenye faida nasi, kama hiyo uranium mnunuzi atakuwa Iran basi tutamuuzia kwani ipo tofauti gani kati ya Iran na Marekani haizidi Marekani ameshauwa sana kuliko hao Wairani.
 
Ukishangaa ya Musa utayaona ya firauni...kwa mtazamo wangu hili suala la kuanza uhusiano wa kijeshi na Iran ni lakuangalia kwa makini. Tusijiingize kwenye games ambazo hatutakuja kuziweza mana hawa jamaa wa Iran policy zao haziko compatible na siasa yetu ya kutofungamana na upande wowote.
 
YNIM,

..USA na Iran ni maadui wakubwa na kuna vita baridi inaendelea kati yao.

..sasa kabla hawa wakubwa[usa & iran] hawajapatana, au kumaliza tofauti zao, kama mwandishi anavyoshauri, ni bora wa-Tanzania tukaepukana nao.

..ni hatari kwa Tanzania kujitia kimbelembele cha kumkumbatia mmoja kati ya wababe hawa waziwazi.

..hawa wababe hawa common border kwa hiyo vita watakayopigana ni proxy war.

..tuwe makini na tuinusuru nchi yetu isije kuwa Angola, Zaire, Vietnam, au Afghanistan, ambazo zilikuwa uwanja wa mapambano kati ya USA and former Soviet Union.

NB:

..tena kama tunaambiwa kuna Uranium ndiyo inabidi tuwe makini zaidi na mashirikiano yetu kama Iran.

..Congo/Zaire walikuwa na wakati mgumu sana wakati wa cold war kutokana na uwepo wa uranium ktk ardhi yao.
 
Mie yangu macho...

MamaWenajilipuamwenyewe.gif
 
dogo weekend hii...badala ya kuwa sehemu sehemu unakula maisha wewe unashinda JF.....ngoja mwenzio niingizane Luckie Lounge....
 
Tatizo sio Ubungoubungo tu, tatizo ni Mods, CEO wa hii JF, MKJJ na genge lake la wadini akina PM, Maxshimba, na yule mpemba hayawani mwenye sura kama fenesi (Mtindiowaubongo). Genge hili linadhani udini utawaletea manufaa ktk agenda zao mufilisi!! Uzuri wenyewe tutabanana nao hapa hapa na wataelewa tu!! Inshallah...

Ahh. .. Ustadha Tausi..i mean Baunsa..

Nilikuwa sijapitia huku..kumbe hata huku unaendeleza pumba zako ..LOL..Unasema unabanana..unabanana na nani? Mimi sina kawaida ya kubanana na watu wenye mtindio. Hiyo ndo filosofia yangu. Nakupa ukweli wako halafu nakuacha..

Hivi, unadhani kuna mtu ana ufagio na pumba zako zaidi ya hao mapakacha wenzako wenye akili butu..? Nilikuacha kule kwenye ile thread utukane matusi yooote uliyofundwa na wazazi wako na ufungiwe peke yako lakini mamods( haswa huyu kimbelembele Silencer) wakakuogopa na kunifungia na mimi ili kukufurahisha ..

Haya sasa, nakupa bonus ofa, kamwambie baba yako Silencer na kingereza chake cha dictionary anifungie tena ili ufurahi na kukenua..

Bua ha ha ha..
 
Last edited by a moderator:
Wewe ni chizi, tena alokuroga kesha kufa....lol! Kama ni karata basi wewe galasa...

Naona hili la mafungamano na Wairani lisikupe tatizo moyoni kwani mara nyingi hii mikataba inayofanywa na wakubwa wetu haitufungi na wala hatuna bidii ya kuifatilia. Naona mtaumiza vichwa kwa kukosa usingizi wakati hii si mikataba bali ni mbinu za kupata kufutiwa madeni na mwahala mwa pesa ya haraka kwani hao mabwana wetu tunaowaona wao ndio awliostaarabika na wasafi misaada yao na pesa zao zina njia ndefu kuzipata.

Cha kushangaza ni kuwa Wabongo ubongo wetu umelemazwa na uzungu na kutiwa chuki na uarabu lakini hao wazungu pesa wanayotambia inatoka huko kwa Waarabu na viongozi wetu wanalijuwa hilo na ndio maana wanajisogeza nao kwa Waarabu. MSIPOTEZE USINGIZI hakuna Muirani atakaekuja hapa bali ni SIASAtu.
 
YNIM said:
Mkuu Joka,
Mbona unapindisha mchana kweupeee ninachosema mimi ni kuwa, tunaweza kuwa marafiki wa Iran kama ambavyo tulivyo marafiki wa USA bila kuegemea upande wowote ktk bifu lao....so far ndipo tulipo sasa hivi Tzania kama nchi!!

Hizi story za kusema tusiwe rafiki wa yeyote mpaka wa sort out tofauti zao umezitoa wapi? Hivi Bush alikuwa anafanya nini bongo mwaka jana!? Unachosema wewe kimsingi ni kuwa, tuwe rafiki wa USA na sio Iran (kitu ambacho nadhani si sahihi), na huko ndiko kuchukua sides kwenye/kujiingiza ktk bifu lao.

Hizo habari za proxy war kupigwana Tzania umeziokota wapi mkuu!? Vita ya Iran na US inapiganwa huko huko middle east hasa Palestine, Lebanon na sasa Iraq...hizo scare tactics zako zitafanya kazi hapa hapa JF kwa watu dizaini ya Ubungoubungo, lakini wajanja tunaelewa kuwa hizo ni story tu!. Moja wapo ya hizo proxy war za Iran na USA ni hiyo onslaught ya Gaza iloisha juzi, ambayo "kimsing" ni another loss kwa Israel.

NB: Bongo inaweza kuwa rafiki wa Iran bila kutengeneza uadui na USA, vile vile inaweza (kama ambavyo ilivyo sasa) kuwa rafiki wa USA bila kutegeneza uadui na Iran......longolongo zaidi ya hapo ni majungu, udini, fitina, uzushi na uzandiki uso kipimo!

Wkend Njema!

YNIM,

..uhusiano na urafiki tunaozungumzia hapa ni ktk masuala ya KIJESHI.

..kama Iran wanataka kutusaidia kulima mbirimbi,mboga-mboga etc i am cool with that. kuna mradi wa kilimo maeneo ya Rufiji uko funded na wa-Iran.

..Marekani nao kama wanataka kutusaidia kupambana na malaria i am also cool with that.

..mahusiano ninayoyapinga mimi ni mahusiano ya KIJESHI na mataifa hayo mawili.

..hakuna suala la udini hapa. Tanzania ina mahusiano ya kijeshi na Egypt na Algeria, nchi za Kiislamu, na sina matatizo nayo. mwenendo wa serikali za mataifa hayo ni tofauti na ule wa Iran.

..mwisho, article uliyoileta kuhusu Iran inatisha, lakini ndiyo ukweli wenyewe kuhusu Iran. hakuna haja ya kunisakama kwamba natisha wana-JF, wakati wewe mwenyewe umeshindwa kuleta taarifa zinazowa-humanize wa-Iran.
 
Inasemekena Tz kuna Uranium na Iran anahitaji sana hiyo resource

Inaoenkana kila anayetaka kuwa Rais Tz ni muhimu kuwa karibu na Iran

......of all the countries!!!.....Iran!!.......give me a break!!......damn


Labda upo sahihi!!

Iran needs Uranium

'Iran running short of uranium supply'

Link:
'Iran running short of uranium supply' | Iran news | Jerusalem Post


Iran in scramble for fresh uranium supplies
Link:
Iran in scramble for fresh uranium supplies - Times Online


Report: Iran's uranium supply could run out within months
Link:
Report: Iran's uranium supply could run out within months - Haaretz - Israel News

Does Tanzania have it?

Tanzania Prepares Policies For Uranium Mining
Link:
Tanzania Prepares Policies For Uranium Mining

UK firm buys Tanzania uranium licences
Link:
UK firm buys Tanzania uranium licences
 
Mwinyi on Iran ties

DAILY NEWS Reporter
Daily News; Friday,January 30, 2009 @21:15

The Minister for Defence and National Service, Dr Hussein Mwinyi, has explained that Tanzania's cooperation with Iran is in the area of the transfer of technology and experiences to the national service and does not involve military affairs.

Clarifying recent reports implying that Tanzania was developing military cooperation with Iran, the minister said mutual cooperation in defence was not an agenda in his visit to Iran last year.

He said the cooperation with Iran will be in agriculture – farming and livestock development in the national service and not otherwise. "The coperation will be in those areas and the technology being referred to is in agriculture and livestock husbandry in the national service. He said Tanzania could benefit from Iran's experience in these fields.

Ushirikiano wetu na Iran ni kwa kilimo - Waziri

Mwandishi Wetu
Habari Leo; Friday,January 30, 2009 @21:15

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Dk. Hussein Mwinyi amefafanua kwamba ushirikiano unaokusudiwa kuendelezwa kati ya Tanzania na Iran, utakuwa kwenye maendeleo ya kilimo na ufugaji ndani ya JKT.

Akifafanua taarifa zinazotoa picha kwamba Tanzania inaendeleza uhusiano wa kijeshi na Iran, Dk. Mwinyi alisema uhusiano uliozungumziwa wakati wa ziara yake Iran mwishoni mwa mwaka jana, ulikuwa wa kubadilishana ujuzi na teknolojia katika kilimo na ufugaji kwa JKT.

Hakuna kilichozungumzwa kuhusu uhusiano wa kijeshi, alisema. Waziri alisema Tanzania inaangalia uwezo ambao Iran inao katika teknolojia ya kilimo na ufugaji ili kujenga ushirikiano na nchi hiyo katika maeneo hayo.

Msaada wa kilimo jeshini. Msaada wa kilimo jeshini. Okay! Msaada wa kilimo jeshini.

Wanaweza kutuonyesha hiyo Memorandum of Understanding iliyoripotiwa kusainiwa?

Hakuna kitu nakisubiri kwa hamu kama muswada wa Freedom of Information Act unao languish wizara ya Mkuchika toka 2007. Lakini unaweza kupitishwa na waandishi wakashindwa kuutumia. Press ya vilaza.

Hawasemi ilikuwaje mpaka akatoa ufafanuzi leo kwa habari ya wiki mbili zilizopita, alibanwa na mwandishi au alikuwa na routine press conference, alikuwa kwenye kilabu cha pombe akaulizwa na some curious friend, what was the occasion? Masharti ya huu mkataba ni nini? Hizo reports alizokuwa ana clarify ni zipi hizo? So far nimeona ni magazeti ya Iran na ya Uchina yamenukuliwa na Mwanakijiji yakisema uhusiano ni wa kijeshi. Sasa Waziri sijui anasema Wairani waongo? Hakuna wakutuhabarisha hivi vitu.

Yani kuna mtandao wa Wachina ndio umeripoti lile dili siku liliposainiwa, na some Iranian outlet. Sisi aaaah, hatuna presha na maisha. Tumenukuu Wachina na Wairani wanaandika kuhusu dili letu la kijeshi. Sijui kilimo, sijui kijeshi. Sijui JKT. Who knows. Na JKT hivi ni nini hasa, zamani nikikuwa nafikiri ilifutwa pamoja na utaratibu wa JKT ya lazima wa wanafunzi. Sasa hii JKT hii, nani anaenda JKT siku hizi, kazi yake nini hasa, kutulisha? Kwa mujibu wa sheria gani?
 
Kati ya Waziri wa Tanzania au wa Iran mmoja wao amelidanganya taifa lake:

Hivi ndivyo imeripotiwa:

Mwandishi Wetu
Daily News; Friday,January 30, 2009 @21:15

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Dk. Hussein Mwinyi amefafanua kwamba ushirikiano unaokusudiwa kuendelezwa kati ya Tanzania na Iran, utakuwa kwenye maendeleo ya kilimo na ufugaji ndani ya JKT.

Akifafanua taarifa zinazotoa picha kwamba Tanzania inaendeleza uhusiano wa kijeshi na Iran, Dk. Mwinyi alisema uhusiano uliozungumziwa wakati wa ziara yake Iran mwishoni mwa mwaka jana, ulikuwa wa kubadilishana ujuzi na teknolojia katika kilimo na ufugaji kwa JKT.

Hakuna kilichozungumzwa kuhusu uhusiano wa kijeshi, alisema. Waziri alisema Tanzania inaangalia uwezo ambao Iran inao katika teknolojia ya kilimo na ufugaji ili kujenga ushirikiano na nchi hiyo katika maeneo hayo.

Lakini vyombo vya Iran na vingine vya kimataifa viliripoti hivi:

ISNA - Tehran
Service: Foreign Policy


TEHRAN, Jan. 21 (ISNA)-Iran and Tanzania signed a Memorandum of Understanding (MoU) on Wednesday to boost defense cooperation.

The MoU was signed as Iran's Defense Minister Mostafa Mohammad Najjar and Tanzania's Minister for Defense and National Service Hussein Mwiny held their second round of talks in Tehran for expansion of defense cooperation.

The two sides also stressed strengthening international peace, security and stability and expansion of defense ties.

The Memorandum of Understanding involves sharing defense and military experiences and dispatching delegations on service, technical and training fields.


Mwiny heading a defense delegation stepped in Iran on Monday for talks with Iranian officials on defense section. He has been officially invited by Najjar.

Hussein Mwiny is the first Tanzanian Defense Minister who has tripped to Iran after Islamic revolution in 1979.

more News:
Iran-Tanzania defense ties to be expanded



TEHRAN (IRNA) – Iran’s Defense Minister stressed the need to expand ties with Tanzania in all fields, given its strategic location in east Africa.


In a meeting with his Tanzanian counterpart, Hussein Ali Mwinyi, Major General Mostafa Mohammad Najjar expressed Iran’s readiness to broaden its ties with the country in all fields.

Referring to his ministry’s capabilities in defense industries, he further noted that it is ready to convey its experience to the country.


Pointing to Zionist regime’s brutalities in Gaza, Najjar said Gazans’ resistance once again defeated the forged regime as it was trounced by Hezbollah in 33-day war.

He called on the Muslim nations to help end Zionist regime’s crimes and said that using forbidden bombs such as phosphorous bombs by Israelis to kill Palestinians is a war crime and they should be prosecuted in an international court.

Mwinyi, for his part, expressed pleasure over his visit to Iran and stressed the need to broaden defense ties between Iran and Tanzania.


He(Mwinyi) also announced his country’s interest in developing relations with Iran in all fields and said that Iran has valuable experience and advanced equipment which can be useful for Tanzanian armed forces.

So:

Yawezekana:

a. Waziri wa Iran alikuwa anadanganya
b. Waziri wa Tanzania alikuwa anadanganya
c. Hawa wote hawajui walichokubaliana
d. Hawa hawakukutana kabisa na hawaakuzungumza lolote!

Vyovyote vile ilivyo; Kama Mwinyi kadanganya basi na yeye ajiandae kuomba msamaha tumsamehe.
 
Issue ya Iran ina angle mingi sana.....kitu ambacho bongo inafanya na Iran so far ni pouwa tu, ila unataka kubebea bango kwa sababu zako binausi! carry on and yes you can... goodluck.

Kuwa na uhusiano sio tatizo, ila hao tunaoweka nao uhusiano wanataka nini au wana nia gani na huo uhusiano?
 
Mwanakijiji,'
Let me be biased. Nadhani aliyedanganya ni waziri wa Tanzania. Tuna utamaduni huo.
 
Back
Top Bottom