Tanzania kuipa Comoro Msaada wa Ndege

Tanzania kuipa Comoro Msaada wa Ndege

Tz na wa tz kwa kupenda kujitutumua et nanyie mnatakakutoa msaada wa usafili wa anga mbavu znaniuma kwa kicheko kilichojaa kebei/ nyie wakomoro mnamacho lakini hamuon kweli tz inaweza kuwasaidia ktk hili? duuuuuuu
 
Tz na wa tz kwa kupenda kujitutumua et nanyie mnatakakutoa msaada wa usafili wa anga mbavu znaniuma kwa kicheko kilichojaa kebei/ nyie wakomoro mnamacho lakini hamuon kweli tz inaweza kuwasaidia ktk hili? duuuuuuu

wa comoro huenda walikuwa wanafanya "Jokes" za kiutu uzima
 



SERIKALI ya Comoro imeiomba Serikali ya Tanzania iisaidie kutatua changamoto ya uhaba wa ndege zinazotua nchini humo hali iliyosababishwa na kusitishwa kwa huduma za safari za shirika la ndege la Yemen.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Waziri wa Uchukuzi wa Comoro, Bahia Masoundi, alisema Shirika la Ndege la Yemen lilisitisha huduma zake kufuatia machafuko yanayoendelea nchini Yemen.

“Mchafuko ya nchini Yemen yalipelekea shirika lao la ndege kusitisha huduma zake na kutokana na kwamba ndilo shirika tulilokuwa tukilitegemea kwa kiasi kikubwa ndio maana uhaba umejitokeza baada ya kufunga huduma zao,” alisema Massoundi.

Alisema kwa sasa kuna mashirika manne tu yanayofanya kazi nchini humo na ndege zinazotua ni chache na kwamba serikali ya nchi hiyo haimiliki shirika hata moja hivyo kulazimika kuomba msaada nchini Tanzania.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Anga Tanzania (TCAA), Charles Chacha alisema waziri huyo amefanya mazungumzo na waziri wa Uchukuzi nchini, Samweli Sitta ambaye ametoa maagizo kwa TCAA ili ifanye utaratibu wa kuisaidia nchi hiyo.

“Tayari tumepokea maagizo ya Waziri mwenye dhamana na sisi kama mamlaka inayosimamia safari za anga tunaanza mara moja kuangalia namna ya kuisaidia Comoro kwasababu ni nchi ambayo ina makubaliano ya kusaidiana na Tanzania,” alisema Chacha.

Alisema kwa sasa ndege za Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) hufanya safari zake mara nne kwa wiki nchini Comoro lakini bado kuna tatizo la mrundikano wa abiria wanaotaka kusafiri kwenda au kuja nchini kwa shughuli za biashara, utalii au kufuata huduma.

Aliongeza kutokana na uwezo mdogo wa ATCL atakutana na uongozi wa mashirika yenye uwezo yanayofanya kazi nchini yaweze kufanya safari nchini Comoro pamoja na kutoa kibali maalumu kwa shirika la ndege la Ethiopia ili ndege zake ziende nchini humo baada ya kutua Tanzania.

Chanzo: Mpekuzi blog
mhhh hivi sisi tuna ndege? au tumekodisha ndege?
 
hahahaha.

Tulipowasaidia kijeshi wakajua hawa jamaa si bure,na madege watakuwa nayo.

Nchi yangu ikawaambia 'ah hilo tu?mskonde'.

The reason to why Orijino komedi hawana ladha tena.
 



SERIKALI ya Comoro imeiomba Serikali ya Tanzania iisaidie kutatua changamoto ya uhaba wa ndege zinazotua nchini humo hali iliyosababishwa na kusitishwa kwa huduma za safari za shirika la ndege la Yemen.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Waziri wa Uchukuzi wa Comoro, Bahia Masoundi, alisema Shirika la Ndege la Yemen lilisitisha huduma zake kufuatia machafuko yanayoendelea nchini Yemen.

"Mchafuko ya nchini Yemen yalipelekea shirika lao la ndege kusitisha huduma zake na kutokana na kwamba ndilo shirika tulilokuwa tukilitegemea kwa kiasi kikubwa ndio maana uhaba umejitokeza baada ya kufunga huduma zao," alisema Massoundi.

Alisema kwa sasa kuna mashirika manne tu yanayofanya kazi nchini humo na ndege zinazotua ni chache na kwamba serikali ya nchi hiyo haimiliki shirika hata moja hivyo kulazimika kuomba msaada nchini Tanzania.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Anga Tanzania (TCAA), Charles Chacha alisema waziri huyo amefanya mazungumzo na waziri wa Uchukuzi nchini, Samweli Sitta ambaye ametoa maagizo kwa TCAA ili ifanye utaratibu wa kuisaidia nchi hiyo.

"Tayari tumepokea maagizo ya Waziri mwenye dhamana na sisi kama mamlaka inayosimamia safari za anga tunaanza mara moja kuangalia namna ya kuisaidia Comoro kwasababu ni nchi ambayo ina makubaliano ya kusaidiana na Tanzania," alisema Chacha.

Alisema kwa sasa ndege za Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) hufanya safari zake mara nne kwa wiki nchini Comoro lakini bado kuna tatizo la mrundikano wa abiria wanaotaka kusafiri kwenda au kuja nchini kwa shughuli za biashara, utalii au kufuata huduma.

Aliongeza kutokana na uwezo mdogo wa ATCL atakutana na uongozi wa mashirika yenye uwezo yanayofanya kazi nchini yaweze kufanya safari nchini Comoro pamoja na kutoa kibali maalumu kwa shirika la ndege la Ethiopia ili ndege zake ziende nchini humo baada ya kutua Tanzania.

Chanzo: Mpekuzi blog

hii habari imekaa kama wakwenda kuomba majamvi msibani
yaani kweli siasa ni kitu kibaya sana
 
inafedhehesha sana unakuwa na mdogo wako anajua utamsaidia na anakutegemea kumbe na wewe hujiwezi. mbaya zaidi hujiwezi sababu ya uzembe.
 
Kabla sijafungua huu uzi nilikuwa najiuliza wanataka ndege wale wanyama (birds) au ndege kifaa cha usafiri (aeroplane), maana haiingii akilini mtu kuiomba Tanzania (nchi yangu) ndege (aeroplane), hata sasa napata mashaka na habari hii.
 
Maskini comoro rafiki yetu,tunashukuru umetupa heshima kuubwa sana kuliko uwezo wetu.Habari imeniumiza sana kichwa changu leo.
 
Kwikwiiiii......mwe....kwel hawa yamewazid.....wanaiyomba sanda maiti....hiv comoro amekosa kwel marafiki...had amekuja tz
 
Kweli jamani tusiwe wachoyo wa ndege tuwape tu wacomoro ni jirani zetu. Yaani ndege wamejaa maporini halafu wengine Hadi wanaharibu mazao mashambani! Tena naishauri serikali yetu sikivu ianze na kunguru wa zanzibar!
 
Shirika la ndege la Tanzania limeanza safari za kila siku mwenda Moroni Comoro kuanzia jumatatu ya tarehe 18/05/2015, safari hizo zitaanzia Dar es Salaam, Moroni, Mtwara, Dar es Saaam. Kwa sasa ATC inayo ndege moja tu itakayokuwa ikitoa huduma ya usafiri kwa njia hiyo.




 
Hahaha duuh hii ni kweli???

Nakumbuka juzi mh mkosamali alisema serikali imezidiwa akili na wakurugenzi wa makampuni binafsi kama presicion na fastjet so serikali ikayaaombe haya makampuni binafsi kupeleka ndege zao comoro
 
Ki ukweli hii ni aibu inapotokea fursa kama hii kwa taifa kama hili Lililopata uhuru zaidi ya miaka 50iliyopita,lenye idadi ya watu zaidi ya 40 milioni inashindwa kuwa hata na shirika la ndege lenye ndege zinazoruka?
Kenya na Rwanda mbona wao wameweza wana nini? Nasisi tunashindwa kwa nini?
kweli tuna haja ya kujitafakari upya kama taifa na kujua mwelekeo wetu ni upi.
Nikiangalia mbele naona giza totoro,
 
Back
Top Bottom