Manyerere Jackton
JF-Expert Member
- Dec 11, 2012
- 2,438
- 4,461
Kiukweli ni kwamba Watanzania tuna nafasi kubwa mno ya kuwa super power kiuchumi na kijeshi katika ukanda huu. Ukiaacha Afrika Kusini, sisi ndo tulipaswa kuwa wa pili. Lakini kwa sababu ya udhaifu wa viongozi wetu, Tanzania imebaki kuwa nchi isiyojiamini na ndio maana wachangiaji hapa wanaonyesha kutokuwa na hakika kama kweli Tanzania inaweza kuisaidia Comoro usafiri wa ndege. Juzi tu tulikuwa Comoro pamoja na wafanyabiashara 200 kutoka Tanzania. Kuna fursa nyingi za kiuchumi ndani ya Comoro. Ni suala la sisi kuamsha akili tu na kuacha woga.