Tanzania ina uhaba wa skills. Je, kuna tatizo katika Mfumo wa Elimu?

Masokotz

JF-Expert Member
Nov 26, 2018
3,495
5,532
Habari za wakati huu,

Katika suala la ujenzi wa uchumi na maendeleo moja kati ya vitu muhimu sana katika labour force ni skills.Mfumo wa elimu unalenga kuwapatia watu skills and knowledge.

Skills ni uwezo wa kufanya jambo kikamilifu na Knowledge ni uwezo wa kuelewa jambo kikamilifu. So ninaposema kama taifa tuna uhaba wa skills namaanisha kwamba tuna idadi kubwa ya watu ambao hawana uwezo wa kufanya jambo lolote kikamilifu/hawajua wanaweza kufanya jambo gani kikamilifu.

Ninaposema kwamba watu wengi hawana skills simaanishi kwamba watu wote ila asilimia kubwa.Kwa mtazamo wangu kuna aina mbili za skills (Transferable skills na Non-Transferable skills) Sasa kwa taifa letu wengi wamepawaya katika aina zote mbili za skills na mbaya zaidi mfumo wetu wa elimu haujaaangalia namna sahihi ya kuhakikisha kwamba labour force inakuwa na skills zote muhimu ili waweze kujiajiri au kuajiriwa.

Katika semina moja tuliwahi kuambiwa kwamba. Kama kazi ambayo unatafuta huwezi kuifanya mwenyewe bila kuajiriwa basi huna competency ya kutosha. Mfano kama wewe ni mwalimu unatafuta kazi ya ualimu na hujaweza hata kufungua tution centre basi kuna walakini juu ya uwezo wako wa kufundisha.Kwa lugha nyepesi kama huwezi kujiajiri katika fani yako basi hufai hata kuajiriwa.

Leo niwakaribishe tujadili iwapo mfumo wetu wa elimu na malezi una muaandaa mtu kikamilifu kuweza kuajiriwa au kujiajri katika fani yake.

Karibuni
 
'Mfano kama wewe ni mwalimu unatafuta kazi ya ualimu na hujaweza hata kufungua tution centre basi kuna walakini juu ya uwezo wako wa kufundisha.'

Haya kama mtu ni Pilot na hajapata kazi na yeye anatakiwa afanye nini?
 
'Mfano kama wewe ni mwalimu unatafuta kazi ya ualimu na hujaweza hata kufungua tution centre basi kuna walakini juu ya uwezo wako wa kufundisha.'

Haya kama mtu ni Pilot na hajapata kazi na yeye anatakiwa afanye nini?
Kuna pilot ambae Hana kazi Tanzania?

Mwaka Jana kule mbugani Serengeti kulikuwa na uhaba wa pilots wa kuembesha zile parachutes Hadi wakaenda kutafutwa kenya.
 
Kuna pilot ambae Hana kazi Tanzania ?


Mwaka Jana kule mbugani Serengeti kulikuwa na uhaba wa pilots wa kuembesha zile parachutes Hadi wakaenda kutafutwa kenya.
'Kuna pilot ambae Hana kazi Tanzania?'

Tembelea pale Civil Aviation Training college (CATC) watakupa majibu mujarabu khs suala hilo ila usije kushangaa.
 
'Mfano kama wewe ni mwalimu unatafuta kazi ya ualimu na hujaweza hata kufungua tution centre basi kuna walakini juu ya uwezo wako wa kufundisha.'

Haya kama mtu ni Pilot na hajapata kazi na yeye anatakiwa afanye nini?
Mkuu,hata Pilot kuna maeneo yake ya kujimwamba na kuonesha uwezo wake wakati anasubiri ajira.Anaweza kufanya kitu.
 
Tatizo kuna nyakati unaweza pewa maarifa hayo na mtu ambaye hata yeye pia hana competency na hicho alichokupa.
 
Mkuu wewe ni PILOT.Unajua PILOT akiwa shule anasoma nini?
Mkuu tu-assume mimi sio Pilot na sijui chochote kile khs hayo mambo ya Aviation i.e Aviation Security,Aeronatical info. Management,AirTraffic Management,Communication Nav&Surveillance etc,then unaweza kunisaidia labda wanasoma nini wakiwa huko mkuu?
 
1. Tunamfumo wa elimu unaowajaza wanafunzi mambo mengi ambayo hayana applications katika real life problems za hapa Tanzania. Ukiwapa maswali ya matatizo ya jamii ya uhalisia wanaanza search majibu kutoka katika point walizokuwa wanasoma class kule chuo.

2. Maofisi ya taasisi za serikali na binafsi hayana utamaduni wa kuwasaidia vijana kuweza kujipa mazoezi na kujua utofauti wa vitu wanavyoclamishwa class na uhalisia wa mambo huku duniani. Hili si tatizo kwa mataifa ya wenzetu huko ulaya na Asia. Walishashtuka mapema sana.

Sisi vijana wakimaliza chuo wanapotafuta nafasi ya kuweza kujinoa wanakutana na ujumbe kuwa inahitajika experience ya miaka 5 au 10. Sasa kijana anatoa wapi hiyo experience na amemaliza chuo?!

3. Elimu yetu ni 90% impractical yaani ni notes mwanzo mwisho. Hii sio nzuri katika kujenga uwezo wa kiutendaji.
 
Ila nikichogundua madogo wa sasa mnaanza kuwa active akili zenu zinaanza kuwaza positive of which is good for the nation..... Mnaweza kutumia vichwa kuwaza positive na kuhoji mswali ya msingi.
 
Mkuu tu-assume mimi sio Pilot na sijui chochote kile khs hayo mambo ya Aviation i.e Aviation Security,Aeronatical info. Management,AirTraffic Management,Communication Nav&Surveillance etc,then unaweza kunisaidia labda wanasoma nini wakiwa huko mkuu?
Mkuu,hizo zote ulizotaja ni maeneo ambayo PILOT anaweza kufanya kazi kama Independent Consultant,Researcher,Advisor etc wakati akisubiri fursa za kuruka.Hio itamwezesha kujenga Network yake na kujiongezea fursa.SO NAFIKIRI nimekupa JIBU.
 
Mkuu,hizo zote ulizotaja ni maeneo ambayo PILOT anaweza kufanya kazi kama Independent Consultant,Researcher,Advisor etc wakati akisubiri fursa za kuruka.Hio itamwezesha kujenga Network yake na kujiongezea fursa.SO NAFIKIRI nimekupa JIBU.
Acha kukariri maisha hayapo hivyo.
 
Mkuu,hizo zote ulizotaja ni maeneo ambayo PILOT anaweza kufanya kazi kama Independent Consultant,Researcher,Advisor etc wakati akisubiri fursa za kuruka.Hio itamwezesha kujenga Network yake na kujiongezea fursa.SO NAFIKIRI nimekupa JIBU.
Hapo hakuna jibu umetoa mkuu,yaani hayo maneno uliyoniambia hapa ni kama yale ya motivational speaker mkuu.
 
Hapo hakuna jibu umetoa mkuu,yaani hayo maneno uliyoniambia hapa ni kama yale ya motivational speaker mkuu.
Kwa hio maneno ya motivational speaker kwako hayana maana?Basi utakuwa na matatizo mengine zaidi na kwa sababu hutaki kukubali unaishia kuwalaumu Motivationa Speaker kumbe wewe tayari una matatizo tofauti kabisa.Binafsi nafikiri kama kweli unataka kufanya kitu kati ya hivyo Fanya kutafuta mtu anayeelewa jinsi ya kufanya akuongoze.Mimi binafsi sina uwezo wa kukusaidia.

Ila nakutakia kila heri pamoja ba subra
 
Kwa hio maneno ya motivational speaker kwako hayana maana?Basi utakuwa na matatizo mengine zaidi na kwa sababu hutaki kukubali unaishia kuwalaumu Motivationa Speaker kumbe wewe tayari una matatizo tofauti kabisa.Binafsi nafikiri kama kweli unataka kufanya kitu kati ya hivyo Fanya kutafuta mtu anayeelewa jinsi ya kufanya akuongoze.Mimi binafsi sina uwezo wa kukusaidia.

Ila nakutakia kila heri pamoja ba subra
Asante sana mkuu,ila next time mkiwa mnajadiliana na wenzako khs practicality ya elimu yetu muwe pia mnajaribu kuja na relevant solutions za matatizo hayo na sio mnakuja na maneno matupu yasiyo saidia jamii inayotuzunguka mkuu.
 
Asante sana mkuu,ila next time mkiwa mnajadiliana na wenzako khs practicality ya elimu yetu muwe pia mnajaribu kuja na relevant solutions za matatizo hayo na sio mnakuja na maneno matupu yasiyo saidia jamii inayotuzunguka mkuu.
Utupu wa maneno yangu ni upi?Ninchoona ni utupu wa fikra zako.Mimi nimeleta mjadala hapa ili wewe uwe mwenzangu tuujadili.Wewe ukashindwa kujadili kwa sababu ambazo tayari unazijua.Nilipjaribu kukurudisha kwenye mada bado ukazidi kuonesha utupu wako kwa kutoka zaidi kwenye mada kwa hili jibu lako.

Maelezo yako ni uthibitisho kwamba hukupewa skills au hukupewa uwezo wa kutumia skills zako either katika mfumo wako wa malezi au wa elimu.Hivyo siwezi kukulaumu wewe bali naweza kukutumia kama uthibitisho kwamba kweli kuna tatizo katika mfumo wetu wa elimu.Naamini kwamba mfano wako utawasaidia wachnagiaje wengine kuelewa kwamba hapa tunajadili tatizo liko wapi na suluhu ni nini.Mifano niliyotoa isaidie kuhamasisha mjadala na sio watu kuleta frustration zao.
 
Back
Top Bottom