OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,191
- 103,715
Nitatumia lugha kali lakini ndio ukweli mchungu. Tanzania haiwezi kuendelea zaidi ya hapa pamoja na kuwa na rasilimali za maana. Nimefikiria kwa haraka haraka kwa kuitazama Tz katika miaka 40 ya uhuru,ikaja miaka 50 ya uhuru na sasa miaka 60 ya uhuru. Hakuna hatua kubwa ya maana tuliyopiga ukilinganisha na umri ya nchi ikiwa huru.
Sababu kubwa nayoona ni watu wake kuwa wavivu kimwili na kufikiria. Akili za watanzania wengi ni nzito sana,inaishia kwenye kufikiria mambo madogo madogo na jinsi ya kujikimu tu. Ukitaka kuipeleka kwenye vitu vikubwa vya maendelea makubwa ya mtu mmoja mmoja na taifa inagoma.
Bahati mbaya zaidi kwa sababu hawafikirii kiasi kikubwa wamebaki wameacha mustakabali wa maisha yao kwa wanasiasa. Yaani wanasiasa wafikirie kwa niaba ya wao walio wengi.
Sababu kubwa nyingine ni viongozi wa siasa na taasisi za umma na binafsi. Wengi wana uwezo mdogo sana wa kufikiria. Kwa sababu watu hawa wanatoka kwenye jamii ile ile ya Watanzania.
Nini kifanyike?
Kwa kizazi kilichopo hakuna namna. Lakini kidogo kidogo tunaweza kusogea kama tutafumua mfumo wote wa elimu,uwafanye watu waanze kutumia akili ipasavyo. Wakianza kufikiria ipasavyo itapelekea kuondoa wanasiasa na viongozi wavivu wa kutumia akili na kujenga taifa lenye uelekeo
Sababu kubwa nayoona ni watu wake kuwa wavivu kimwili na kufikiria. Akili za watanzania wengi ni nzito sana,inaishia kwenye kufikiria mambo madogo madogo na jinsi ya kujikimu tu. Ukitaka kuipeleka kwenye vitu vikubwa vya maendelea makubwa ya mtu mmoja mmoja na taifa inagoma.
Bahati mbaya zaidi kwa sababu hawafikirii kiasi kikubwa wamebaki wameacha mustakabali wa maisha yao kwa wanasiasa. Yaani wanasiasa wafikirie kwa niaba ya wao walio wengi.
Sababu kubwa nyingine ni viongozi wa siasa na taasisi za umma na binafsi. Wengi wana uwezo mdogo sana wa kufikiria. Kwa sababu watu hawa wanatoka kwenye jamii ile ile ya Watanzania.
Nini kifanyike?
Kwa kizazi kilichopo hakuna namna. Lakini kidogo kidogo tunaweza kusogea kama tutafumua mfumo wote wa elimu,uwafanye watu waanze kutumia akili ipasavyo. Wakianza kufikiria ipasavyo itapelekea kuondoa wanasiasa na viongozi wavivu wa kutumia akili na kujenga taifa lenye uelekeo
Sisi n hatupendi kufanya kazi lakini tunataka tuwe napesa mfukoni je tutazipata vipi bila kufanya kazi tena sio kufanya kazi tuu bali n kwa kujituma sana je hyo spirit tunayo?
N watu wa kulaumu kila kitu serikali ifanye Ila tunasahau kuwa serikali n watu na watu ndo sisi yaan tunapenda kufanyiwa sasa Kama hukufanya wewe unahisi utapata kile unachostahili ndo mana mtu mvivu na mzembe kulalamika hakutamuisha kamwe eti unategemea Chama Cha siasa ndo kikuletee urahisi wa Mambo yako thubutu hilo haliwezekani, urahisi wa Mambo yako unafanyanywa na pesa na ili uwe na pesa lazima ufanye kazi na ujitume.
Unakuta kijana au hata mtu mzima kapata kazi analipwa vizuri tuu badala ya kusave pesa yeye ndo kwanza anawaza kunywa pombe na pizi Kali, kununua Gari la kustarehe, hujaoa unapanga nyumba nzima eti uishi ki single boy unaacha kuishi kibachela matokeo yake baadae tunaanza kulalamika hoo Kodi nyingi mshahara hautoshi Yan full kulalamika tunasahau kuwa pesa uletwa na pesa Kama huna pesa tumia akili kupata pesa pia tambua akili huishiwa maarifa hvyo n muhimu ukiwa na pesa tumia pesa kupata pesa nasio kutumia pesa kupata vitu.
Uwezo wa kufikiria
Hii kiukweli sisi Ma-slowlearn yan tunachelewa kujua vitu na hatuwezi kujenga hoja kabisa mfano Tanzania insvyuo vikuu zaidi ya 15 na kila chuo kinatoa wahitimu zaidi ya 200 kila mwaka Sasa jiulize kweli wataalamu wetu wameshindwa kutoa elimu jamii kuhusu KATIBA au CHANJO YA KORONA na kuwaacha wanasiasa watoe hyo elimu.
Mpaka Leo kijana anajitimu chuo kikuu hajui anaenda mtaani kuwa Nani kweli?
Mwanao anatakiwa kwenda chuo kikuu na hawezi kujaza fomu za elimu ya juu wazazi mnashinikiza au mnalipa watu wasasaidie watoto wenu jinsi ya kujaza fomu kweli?
Angalia elimu ya muhindi anasomea kweli na kazi anafanya kweli Sasa wewe mtanzania mwenzangu umesoma lakini hujaelimika bado unajua kesho n siku ya kazi unaenda kulewa mpaka saa sita usiku asubuh unafika kaxin sas nne na misamaha kibao unafikiri muhindi au boss wako atakulipa vizuri? Kwanini usiseme anakunyanyasa?
TUJIFUNZE JINSI YA KUJIANDAA NA KUPANGILIA MAMBO YETU.
- Wewe n kijana unasoma basi jiulize au ulizia kwa wanaojua hicho unachosoma kina faida gani kwenye jamii na je unakiweza au unasoma kutimiza wajibu?
- Umepata kazi jifunze jinsi yakuwa mbunifu kazini tena ikibidi siku ya holiday omba jitolee kufanya kazi ofisini kwako bila malipo pia ukipata pesa punguza matumizi ya kijinga iga wahindi au watanzania wenzio WACHAGA mana hawa pia wameiga au wamefundishwa kuishi Kama WAHINDI.
usitegemee mwanasiasa akuletee urahisi wa maisha yako kila kibiashara Ina mtaji na mtaji wa mwanasiasa Ni mtu ambae hajielewi.
Tengeneza pesa, omba MUNGU akupe afya njema, heshimu watu hayo mengine yakatiba, korona, chadema, CCM yote utaona yanakupotezea muda tuu.