Tafadhali nifafanulie hiyo tofauti iliyopo kati ya UGs na PGs wa UDSM.
Ze marcopolo na Shy Mngekuwa ndio watu wa Daraja la chini haya maneno ya Machibya mngeyaaelewa lakini kwakuwa mambo yenu yapo shwari lazima mumuone kama Mzushi tu kwani kwenu hakuna Effect na inawezekana nyi e ndio mliosoma bure Wasaliti wakubwa na wanene, nadhani mnashindwa kusoma alama za nyakati !!!!!!
Machibya aache sera potofu, ni majuzi tu Waziri wa Elimu ameeleza wazi kabisa kuwa ambaye atashindwa kabisa kulipia akate rufaa kwake. Angetakiwa awahamasishe watoto wa maskini kukata rufaa kwa waziri
- Kwanza kabisa PG's wanadhaminiwa mostly na waajiri wao wachache sana wanaojilipia wenyewe, hawa ni wenye makampuni, biashara, makanisa etc. Hivyo basi wakati focus ya UG's ni serikali kupitia bodi ya mikopo ktk PG's 50 kunaweza kuwa na wadhamini 40 tofauti tofauti (responsible sponsors).
- PG's wengi wanaishi manyumbani kwao na wachache waliobaki wana mabweni special na kila mtu na kitanda chake. UG's sasa karibu asilimia 99% pale chuo wanalala mzungu wa nne maarufu kama kubebana.
- Wakati UG's wanakaa kenye lecture theters zingine mpaka 1000, PG's wengi wanakuwa ni less than 100.
- PG's karibu wote wanamudu maisha ya chuo, UG's kibao wamepinda na wengine hela hiyo hiyo ya boom wanalipia ada wadogo zao.
- PG's wengi wana familia na a life to lead (kibongo bongo mtu wa namna hii lazima anakuwa na kauga fulani hivi), wkt UG's ndio kwaanza wanakuwa wanatafuta ujuzi wakaanze maisha.
Nadhani tht gives u the highlight!!!!!!
- Kwanza kabisa PG's wanadhaminiwa mostly na waajiri wao wachache sana wanaojilipia wenyewe, hawa ni wenye makampuni, biashara, makanisa etc. Hivyo basi wakati focus ya UG's ni serikali kupitia bodi ya mikopo ktk PG's 50 kunaweza kuwa na wadhamini 40 tofauti tofauti (responsible sponsors).
- Wakati UG's wanakaa kenye lecture theters zingine mpaka 1000, PG's wengi wanakuwa ni less than 100.
- PG's karibu wote wanamudu maisha ya chuo, UG's kibao wamepinda na wengine hela hiyo hiyo ya boom wanalipia ada wadogo zao.- PG's wengi wana familia na a life to lead (kibongo bongo mtu wa namna hii lazima anakuwa na kauoga fulani hivi lol!!!!!), wkt UG's ndio kwaanza wanakuwa wanatafuta ujuzi wakaanze maisha.
Nadhani tht gives u the highlight!!!!!!
Nyambala sijui unazungumzia PGs wa karne gani ila hiyo unayozungumzia ya kuwa na sponsor siyo kweli. Wanafunze wote wa postgraduate ambao mimi ninawafanahamu na wanatoka kwenye family hawana sponsor yoyote wala mwajiri. Hii sababu ni weak sana, haielezei sababu za PGs kutokugoma. Hivi kweli unaamini kuwa postgraduate students hawahitaji kusaidiwa gharama za masomo???tafadhali fanya utafiti zaidi juu ya
hili.
Nyambala sijui unazungumzia PGs wa karne gani ila hiyo unayozungumzia ya kuwa na sponsor siyo kweli. Wanafunze wote wa postgraduate ambao mimi ninawafanahamu na wanatoka kwenye family hawana sponsor yoyote wala mwajiri. Hii sababu ni weak sana, haielezei sababu za PGs kutokugoma. Hivi kweli unaamini kuwa postgraduate students hawahitaji kusaidiwa gharama za masomo???tafadhali fanya utafiti zaidi juu ya hili.
Swala la kusaidia ndugu sio la UGs peke yao, karibu kila mtanzania aliye na kipato rasmi kuna watu wanamtegemea awasaidie. hii point pia ni weak, haiwezi kusubstanciate tabia ya UGs kugoma wakati PGs wanaendelea na masomo bila migomo.
Ingemake sense iwapo DARUSO wangeomba fungu la kuwawezesha kutafuta report za hali za uchumi wa wanafunzi na kuanalyse uwezo wao wa kujilipia kuliko jinsi wanavyoact irresponsibly!!!
Kilicho wazi hapa ni kuwa kuna wenyenacho wanaruhusiwa kusoma na wasionacho hawatakiwi sasa kuna usalama hapo?Tuangalie mambo kwa undani tunapotoa maoni kwani usawa wa binadamu ni katika mahitaji na Elimu ni hitaji muhimu.
Swala la kusaidia ndugu sio la UGs peke yao, karibu kila mtanzania aliye na kipato rasmi kuna watu wanamtegemea awasaidie. hii point pia ni weak, haiwezi kusubstanciate tabia ya UGs kugoma wakati PGs wanaendelea na masomo bila migomo.
Kama kuna mwenye nacho, je ni kwanini wanafunzi wote waligoma wakidai kila mwanafunzi apewe mkopo 100%??? Je hao waliolipa sasa hivi wametoka wapi iwapo madai ya wanafunzi hawa kuwa watanzania wote hawawezi kujilipia ada chuo kikuu yana uzito?
Hawa wanafunzi wa UDSM wataka kuwa mzigo kwa taifa. Hatuwezi kuacha kusimamia maendeleo tukaanza kubaby sit watu wazima. enough is enough.
Tuelewavyo sisi huku shamba ni kuwa DARUSO hawapingi sera ila wanapinga utekelezaji. Zemakopolo una pinga nini? Kauli ya Machibya? sera ya serikali? au bodi ya utekelezaji?
Naelewa kuwa kauli na vitendo vya akina Machibya ni katika kupinga utekelezaji but ukiangalia dhana nzima hata ya kamati ya bunge wamekubali kuhusu utekelezaji kuwa na walakini.
Jiulize
Hivi nini maana ya MKURABITA/MKUKUTA?
Nini mafanikio ya mkurabita na application yake kwenye hii sera ya uchangiaji wa elimu ya juu? Mimi baba yangu alikataa kunipa hati ya nyumba yake ila alinipa hati ya hisa zake za tanga cement pamoja na salary slip. Hiki nikichekesho ijapokuwa haikuwa hivyo na pia mwenyekiti wa mtaa wangu (CCM) aliidhinisha kuwa hajadanganya.
- Kuna sehemu pa kuanzia lakini sio wale waliofaulu. Tumezoea kuburuzwa na kesho ataburuzwa mwanao kama sio wewe
Kichwangumu unaongea theory nyngi lakini practice iko tofauti na hizo theory. Ukimleta mwanafunzi aliyepeleka hati ya nyumba bodi ya mikopo mlete hapa. Hakuna mtu anayelazimishwa kupeleka hati ya nyumba ili apewe mkopo. wala hakuna collateral yoyote inayohitajika ili kuidhinisha mkopo.
Wanafunzi hawa hawapingi utekelezaji, wanapinga sera. wao wanataka flat rate 100% kwa wanafunzi wote na sera haisemi hivyo.
You sound crazy!!! hawa ni nwanafunzi wa watanzania wa kawaida kipato kidogo. Kwa taarifa yako wazazi wa hawa watoto wanakipato cha chni ya dola 1 kwa siku, ukitaka wajilipie haiwezekani, tuache kujenga matabaka sababu ya umasikini...bila mkopo binafsi nisingekuwa hapa nilipo maana hata secondary nilisoma kwa kufutiwa ada, nachukia unaposhindwa elewa logic ndogo kabisa ya wanafunzi wa UGs kugoma.....
Inasikitisha sana kuona watu mnaweka siasa kwenye mambo ya kitaifa. Yaani wanafunzi wa Chuo Kikuu kudai haki zao linafanywa kwamba ni jambo la kisiasa!
Malipo ni hapa hapa duniani.....!!!! Ipo siku!
Hujui unachoongea pole sana, tafuta mwanafunzi yeyote anayesoma elimu ya juu akueleweshe ....