Tanzania Daima lamshambulia Zitto?

leo uk wa mbele kuna Picha ya Mh Jk akifurahi na Zitto.
Katika picha hiyo tzdaima lajidai "Marafiki wa kufa na kufaana"

Kwanini tzdaima haichapishi picha ya Mh mbowe na JK wakicheka pamoja?
Jee kwa zitto kuchapisha na kuandika maneno hayo , Viongozi wa CDM hawatazidi kumuona ZItto ni msaliti?


mods bado wamelala.
 
kunawatu hawalali wanawaza namna gani cdm itatenganishwa, na kama njia wanaptia vitu avifanyavyo zito kutengeneza hlo. Binafsi nadhani kungalkuwa na shda kihivyo mtangazavyo uongozi cdm usingekaa kmya. Na kunaubaya gani mtu kucheka na binadam mwenzie? siasa ni vita [kwa tafsiri kamili ya vita]??
 
Unajua toka Zito atangaze kugombea urais kupitia CDM amekua adui wa Mbowe na magazeti yake pamoja na watu wote wa Kaskazini ambao wao mbowe ndiye mgombea sahihi kwa sababu anatoka Moshi.Zito komaa nao tu mpaka waache fitina zao.
 
Unajua toka Zito atangaze kugombea urais kupitia CDM amekua adui wa Mbowe na magazeti yake pamoja na watu wote wa Kaskazini ambao wao mbowe ndiye mgombea sahihi kwa sababu anatoka Moshi.Zito komaa nao tu mpaka waache fitina zao.

like like like like like.
 
leo uk wa mbele kuna Picha ya Mh Jk akifurahi na Zitto.
Katika picha hiyo tzdaima lajidai "Marafiki wa kufa na kufaana"

Kwanini tzdaima haichapishi picha ya Mh mbowe na JK wakicheka pamoja?
Jee kwa zitto kuchapisha na kuandika maneno hayo , Viongozi wa CDM hawatazidi kumuona ZItto ni msaliti?
Naona mwandishi wewe ndo unataka tuamini kuwa Tanzania Daima linamshambulia Zitto, au unajenda ya siri kututengenezea ugomvi kwa wana CDM na Zitto. Binafsi siamini kama tofauti za kichama zinamaanisha uadui! Unataka tuamini kuwa Zitto SI RAFIKI wa JK. Kama kweli ni marafiki, TanzaniaDaima imekosea wapi? Namsubiri Zitto aje atuambie yeye si refiki wa kikwete na gazeti limempakazia.
 
Sizani kama kulikuwa na tatizo kwenye picha na ujumbe.Tafsiri yake ukiamua kusukumwa na ushabiki utatafsiri vibaya.Halafu tuache ujuha wa kuamini/kutaka Tanzania Daima liwe linaandika ama kutoa habari kama tutakavy sisi.
 
statizo sio kwa mtoa mada ila liko kwa mwandishi wa gazeti alitaka kutoa picha gani kwa watu hasa kipindi hiki cha siasa za kuviziana?Zitto si tishio tu kwa ccm bali hata kwa baadh ya viongoz wa cdm,watu wanahangaika kuzima nyota yake kila siku.sisi tunajua hakuna ubaya wwt kuwa marafiki hatuna siasa za chuki.Jk atamaliza muda wake then ataiaji km raia sasa uadui wa nn?mwandishi ana ajenda yake
Zitto ana kila dalili ya unafiki inayofahamika hapa duniani. Aliibua hoja nzuri sana ya kumtoa Mh Pinda na imepandisha umaarufu wake na wa CDM, lakini anabakia kuwa mtu wa kuangaliwa kwa makini sana. Aendelee kujifunza kutoka kwa wengine ndani ya CDM na atakapopevuka atakuwa mwanasiasa na pengine rais mzuri sana. Kwa sasa Zitto hana uwezo na ujasiri wa kumfikisha Kikwete mahakamani na kumfilisi mali alizojilimbikizia na mafisadi wengine hapo 2016. Aje rais kutoka CDM atakayekata mizizi ya ufisadi kwa kuwafunga jela mafisadi then baada ya kusafisha nchi ndio Zitto aje apewe urais na atatuongoza vizuri tu, lakini kuwafunga mafisadi Zitto hataweza. Rostam, Lowassa, Riziwani, Serukamba wote ni rafiki zake.
 
Tuliona karibu viongozi wote wa CDM walipoenda pale magogoni na kupewa chai wote walionesha tabasabu/kufurahi tu.
..

Mkuu,
This is so poor.Kwa hio wewe unaona CDM walitabasamu kwa sababu ya chai? Hua hawanywi chai huko makwao.Acheni Poor thinking hizi bana.
 
Wanachama wa CHADEMA wanaoanzisha choko choko ndani ya chama ndio marafiki wa ccm na serikali yake na ndio wanaonekana wazuri na mabingwa wa demokrasia. Mwanahalisi Tar 02/05/2012
 
Naona Mod wa JF anapenda aone wanaJF wote wako upande wa CDM maana kila tunapost kitu tofauti na mtazamo wake na CDM anaziondoa.CCM OYEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEE
 
Zito komaaa nao mpaka waache siasa za ukanda.tulimsikia mzee ndesamburo alivyo mponda zito pindi alipotangaza nia ya kugombea urais.cdm lazima kisambaratike tu kwani zito ana kundi kubwa sana la watu hivyo waomshambulia watakwama tu.
 
Mmh sijaliona gazeti,ila nadhani iyo picha imewekwa purposely,anajua mhariri,hivi tanzania daima si gazeti la mbowe??? Au ni uzushi??
 
kuna kipindi alisema anaenda kulalamika gazet hilo kwa mmiliki. alienda?

wanalalamika kwa mharir siyo mmiliki. kuhusu picha, mi sion tatizo maana picha yenyewe inaongea yenyewe, mi nilivyoiona sikuhitaj kusoma caption, nilipata picha ya kile picha hiyo inaeleza,... jaman waachen waandish wafanye kazi yao. tungejuaje hayo kama isingetolewa!
 
Zito komaaa nao mpaka waache siasa za ukanda.tulimsikia mzee ndesamburo alivyo mponda zito pindi alipotangaza nia ya kugombea urais.cdm lazima kisambaratike tu kwani zito ana kundi kubwa sana la watu hivyo waomshambulia watakwama tu.

do u have any primafacie evidence ya kundi ilo??? Au maneno tu ya mtaani?
 
Hapo kuna hoja hamtaki kuijadili kwa sababu ya uoga wa kuijadili au mapenzi yenu kwa wahusika. Kama kweli Gazeti limeandika chini ya Picha Husika kwamba zito na Kikwete ni "marafiki wa kufa kufaana" kuna jambo la kujadili hapo. Labda wengi wetu si wajuvi wa lugha yetu aadhimu ya Kiswahili.

Kwa Waswahili ukisema huyu ni rafiki yangu wa kufa na kuzikana na siyo kufaana kama mleta mada alivyoandika. Ina maana kwa kila hali urafiki huo hauta kufa wala kutenganishwa kwa jambo lolote lile. Kama wana CDM wanaona kwamba Kikwete ndiye tatizo lao na Zitto anatengenezwa na Gazeti la Tanzania Daima kama ni "rafiki" wa Kikwete basi kwa Zitto kuonekana Kibaraka wa Kikwete ni rahisi sana!!

Mleta mada nadhani lengo lake ni kuwagutua (alert) wana CDM kwamba Gazetil la Tanzania Daima linataka kuwachonganisha!!
 
Huwa napata shida sana na wana JF humu ndani ukizungumza udhaifu wa CDM utashambuliw alkini ukiweka post ya mazuri kila mtu atakusifu safi kamanda hakika wewe ni mapambanaji, ktk siasa za sasa ni lazima wana CDM wakubali kuw Zitto, ni tishio ndani ya CDM na nje ya CDM, na hata Picha yake kutumiw aktk ukurasa wa mbele kwenye Gazeti la Tanzania Daima tunajua klichojificha nyuma yake.

Ni nani asijua Zitto, alipokwenda katika sherehe za kutangazwa uhuru wa Sudani Kusini, Gazeti hili hili lilitoka na picha kubwa ya Zitto na JK sambamba na habari kubwa iliyosema 'JK ambeba Zitto', amuandaa kugombe urais hali ya kuwa siku zote Zitto anajijenga mwenyewe kutokana na hoja zake mahili kwa Taifa letu.

Hakika huu ni mkakati wa baadi ya viongozi wa CDM katika kufifisha nyota yake lakini daima haiwezekani kwa Tanzania ya sasa.
 
Back
Top Bottom