Naomba CHADEMA kwanza kuomba maelezo na msimamo wa chama CCM kuhusu kauli hiyo ya Nape na viongonzi wengine wa CCM kuhusu tamko hilo la uchagga,ukabila udini au kijinsia n.k.Baada ya hapo ichukue hatua za kisheria,Kufungua mashitaka kwa Chama cha CCM au vyama vingine vyovyote na mtu au kikundi chochote kinachotoa matamko hayo bila uthibitisho kwa kufungua mashitaka.Jambo hili likiendelea kuishia kutoa majibu ya majukwaani na malumbano linaendelea kupotosha umma na jamii mzima na jamii itashindwa kuzitofautisha kauli za CCM na CHADEMA kwa ujumla itatupeleka pabaya MUNGU IBARIKI TANZANIA.Hakika umenikuna mwanakijiji. Naomba chadema wafanye yafuatayo;
1. Kumstaki nape na ccm mahakamani ili wathibishe kuwa chadema ni chama cha wachaga.
2. Naomba chadema wakomalie hiki kipengele cha uzushi ili kiingie kwenye katiba mpya
Again, Uishi milele mkuuu.
Sijutii kutolisoma hilo gazeti leo. Hili gazeti sasa hivi ni sehemu ya Habari Corporation. Hivi leo kweli mtu unaweza kuzungumzia Tanzania Daima wakati Raia Mwema iko mtaani? labda kama unataka kusoma mawazo ya mafisadi, ndo utapata Tanzania Daima.
Mkuu kwani ulikuwa ujui? si unawaona wanavyotoa maneno, mimi gazeti likishaanza kusifia mafisadi sitaki ata kuliona
M. M. Mwanakijiji
Matokeo yake tunalazimishwa kuiangalia CHADEMA aidha ni kama chama cha Wakristu au chama cha Wachagga kwa sababu mantiki inayopendekezwa mbele zetu haitupi uchaguzi mwingine wowote. Na tukifuata mlolongo huo huo wa mantiki tunajikuta tunaangalia CCM vile vile kama chama cha Waislamu na ukishaliona hili utaelewa ni kwanini baadhi ya Waislamu ambao walikuwa na tatizo na CCM miaka kadhaa huko nyuma leo hawana tatizo nayo kwa sababu wanaona kuwa kinaongozwa na Waislamu. Na matokeo yake utaona kundi la Waislamu hawa hawawezi kuona kosa au tatizo lolote lile la serikali kwani kwa kufanya hivyo itabidi wakubali matatizo ya Muislamu mwenzao au Waislamu wenzao.
mawakili wa chadema, mh. Lisu na marando tafadhali fungueni kesi mapema iwezekanavyo dhidi ya nape na washirika wake. Ni hatari nape wa ccm kuendelea kuligawa taifa kwa msingi ya ukabila na udini kinyume ne katiba ya nchi yetu tuliachiwa na mwalimu. Amani ya nchi ni muhimu kuliko ccm
Topical,
Kinachonishangaza unapotoa hoja zako mara nyingi naona kama uko pekee
yako na siku zote hoja hujadiliwa na watu wakachangia na kuonekana upande
mmoja umeshinda,Lakini wewe mara zote nikiangalia hoja unazopinga naona
wazi umeegemea upande mmoja kama vile unafaidi zaidi matunda ya uhuru wa
Tanzania bila kuona huruma ya watanzania walio wengi.
Labda nikufahamishe kuwa CCM ni chama cha mapinduzi ya amani kati ya
vyama vya TANU(TAA) na ASP
CCM ni sehemu ya maisha ya watanzania,
ccm ni msingi wa siasa za Tanzania,kila mtanzania unayemuona leo ktk Siasa
ukiondoa wachache sana wametokea CCM,
Mimi ni mwanachama wa ccm kwa miaka 25 (Believe it NOT)
Tofauti iliyopo kati ya CHADEMA na CCM ni kuwa CHADEMA kwa miaka michache
sana tangu kuanza siasa za vyama vingi imeweza kuwa mshindani wa karibu sana
na CCM.Hizi ni jitihada za hali ya juu sana kwenye ulingo wa siasa za ushindani.
Kwa mantiki hii utaona wazi kuwa CCM imeshazeeka na inahitaji damu changa ili kiende na wakati
Sasa bahati hiyo tayari imeshapotea na badala yake imeshikwa na CHADEMA na kwa taarifa yako
CCM inaelekea UPINZANI.Huu ndio ukweli na wenyewe wameshakiri wamepoteza umaarufu na mvuto.
sasa ccm wameshaanza siasa za majitaka...oh chadema ni wachaga,mara ...oh chadema ni wakristo..
.oh chadema wanapoka demokrasia
Watanzania wameshajua nani mtetezi wa kweli hapa...ccm au chadema....niambie mwenyewe Topical.
Naomba uniambie sababu mbili (2) tu za kushindwa kwa ccm.
Sbabu (2) za CHADEMA kupanda chati.
Hapa JF of course hoja kama zangu lazima nitakuwa tofauti kwakuwa nina akili niko huru sifuati bendera fuata upepo
Pili Mwanakijiji ni katika mtandao huo huo wa kanisa katoliki (jumuia za kanisa zimejaa mitaani kupandikiza ubaguzi)
Proof namba moja kama mwandishi siku zote atamsifu mkristo mtawala, na chama ambacho ni kinaratibiwa na kanisa kikristo kama chadema na si vinginevyo umeshawahi kuona akiandika kuhusu CUF pamoja na kwamba ni chama kikubwa sana cha upinzani kwanini (hidden agenda), atafanyeje hayo wakati chama hicho hakifuati matakwa kutoka kwa jumuia?
Chadema haipendwi na watu, vyombo vya habari vinatuhadaa..what is 26% mkuu? pamoja na support kubwa ya fedha haramu za kanisa na mtandao mkubwa wa jumuia mitaani kuwashawashi watu wakipigie lakini wameambulia nini?
Wabadilike au watazimika kwa dhambi ya ubaguzi na kufanya usanii kuchagua waislam weak kwa maslahi fulani fulani?
Mnapojibu moto huu ni muhimu mkakumbuka kuwa mnachochea moto uliowashwa na mtu ambaye yeye na familia yake hawapo Tanzania.......
Ni hayo tu
Principles of valid inferences bado ni tatizo kubwa.Sizani kama Mwanakijiji anataka kutete udini wala ukabila.
Kimsingi amejaribu kuchambua SYLLOGISM iliyotumika kufikia hitimisho kwamba CHADEMA ni wachaga na ameonesha kwamba kama tukitumia hiyohiyo SYLLOGISM lazima tufikie hitimisho kwamba CCM ni cha WAISLAMU.
Hata hivyo ameonesha pia kwamba SYLLOGISM iliyotumika inapelekea kwenye FALLACY.
Mmmh!......mkuu mwanakijiji unatisha! Big up kakaTatizo ni kuwa wako tayari kukubali mwelekeo wa mantiki kwenda upande mmoja lakini kwa kutumia vigezo vile vile hawataki mwelekeo uende upande ule mwingine.
Mtu anasema "Binadamu wote ni sawa (kwa utu na hadhi yao)" vigezo kavitumia ni utu na hadhi
Halafu anasema "Hawa ni binadamu"
Kwa hiyo anataka tuamini kuwa "hawa" binadamu wote wako sawa kwa vigezo hivyo hivyo.
Tatizo ni kuwa atakuja na kusema "Huyu ni binadamu mndengereko"
na kusema "siyo sawa kwa utu na hadhi na binadamu mmakua yule".
Lakini ukimuonesha kujipinga kutokana na kanuni aliyoiweka mwenyewe anaanza kutafuta maelezo kwanini Mndengereko na Mmakua si sawa in light of "binadamu wote ni sawa kwa hadhi na utu". Wanasema Chadema ni chama cha Kichagga kwa uanzilishi wake, uongozi wake, na eneo lake la jiografia kilipokubaliwa awali. Hawajali kama kuna watu wa makabila mengine humo au Waislamu na wasioamini - hilo wakilikubali linavunja hoja yao kuwa CHadem ni chama cha Wakristu na Wachagga. Sasa tukitumia mtiindo huo huo - kwamba tusijali kama kuna Wakristu au Wachagga ndani ya CCM nasi tukafuata mtiririko huo huo wa mawazo tunaweza kusema tu bila shaka CCM ni chama cha Waislamu. Wao watakataa hilo na watajaribu kueleza kwanini CCM SIYO ya Waislamu lakini CHADEMA ni cha Wakristu! It baffles my mind. Na hawa ndio wanaitwa WASOMI.