Miaka 26 baada ya ujamaa kuzikwa hapa nchini bado kuna tuna fikra tegemezi sana, bado wananchi ata wale waliobahati kupata elimu nzuri wanategemea eti serikali iwalishe chakula mdomoni, fikra potofu sana hizi.
Serikali imefanya wajibu wake kwa kuhakikisha hao "unaowaita wasomi" wamepata elimu yao, . Tunatarajia kuwa mtu mwenye elimu ya "chuo kikuu" awe na uwezo wa kuyasoma vizuri mazingira yake, kuangalia matatizo yaliyopo, na kuyatafutia ufumbuzi kwa faida yake binafsi na taifa kwa ujumla. hivyo ni wajibu wa hao wasomi wenyewe, kupitia elimu zao ambazo zinapaswa ziambatane na ujuzi, maarifa na fikra sahihi kuweza kuanzisha shughuli za uzalishaji mali na kuwaajiri wengine ambao hawakupata fursa za "elimu".
Naamini kama wameelimika vizuri, kama elimu imewawezesha kuyajua mazingira yaliyopo vizuri, basi watakuwa na uwezo wa kuzitumia fursa zilizopo kujikomboa kiuchumi, la kama hawawezi basi tatizo lao kubwa "lipo kwenye fikra zao" wenyewe na hivyo ata kama serikali ingewapa mitaji, mitaji hiyo haitawasidia lolote na mwisho wa siku itakuwa ni matumizi mabovu ya fedha za walipa kodi wengine.
Naamini msaada wa serikali katika hili unaweza ukawa tu kwenye kuwaunga mkono wale "walioweza kufikiri na kuanzisha "shughuli zao" kwa kutoa upendeleo maalumu kwa kampuni za ndani kwenye baadhi ya kazi/huduma full-stop.
Jamani muda wa kuisubiri serikali ikuletee chakula mezani umepita, ebu tutambue kuwa "Ujamaa Umekufa Na Hautarudi Tena", ebu tubadilike kifikra na tuitumie elimu tuliyoipata kujikomboa wenyewe, nchii hii bado ni "bikira" kwa kiwango kikubwa na hii ni fursa kwa "msomi aliyeelimika", unachopaswa kufanya ni kufungua tu macho yako na kufikiri kwa bidii sana.
Sawa mkuu,hatuongelei ujamaa lakini tunaongelea sera mbovu za elimu
ambazo zinatengeneza watu ambao wanasiasa wana waita "wasomi" lakini kiukweli
ni bomu ambalo litakuja kuwasumbua au kuisumbua serikali kwa mda mrefu.
Bajeti nyingi za serikali ni za kisiasa,kila kitu wanacho fanya ni siasa tu.
Hakuna mipango ya mda mrefu zaidi ya miaka mitano (5) wakimaanisha wana focus
uchaguzi hadi uchaguzi.
Nimemaliza form6 mwaka 2009 na kujiunga chuo mwaka huo.
Tuliokua tunasoma sayansi tuliahidiwa "mkopo 100%" na tukapewa kweli.
Kwa nini? kwa sababu walikua wana focus kwenye uchaguzi wa 2010.
Unajua mwaka huu (2011) wametoa vipi mkopo baada ya uchaguzi kuisha?
Hakuna cha 100% tena,wanao soma course kama yangu wapo waliopata 80% wengine 70%,..
kwanini?
Ni ubabaishaji mwanzo mwisho.
Hakuna anae taka kulishwa siku zote,kwanza ni kujidhalilisha kulishwa milele kwa hiyo hatulilii kulishwa.
Tunataka kuwezeshwa kwa sababu hatuna msingi financially kwa kujiinua na kufanya kile tunacho weza.
Hebu nambie,nimemaliza civil engineering kwa mfano,...unategemea nipate wapi mtaji wa kufanya kazi
zinazo husiana na taaluma yangu ili hata baadae niajiri wengine?
Nadhani umetoa mfano ukidhani kila anae soma chuo ni mtoto wa fisadi,wengine hata mkopo
kidogo tunaopata tunasomesha wadogo zetu shule za kata,...