Speaker
JF-Expert Member
- Aug 12, 2010
- 6,324
- 2,238
Miaka mitatu mijayo tutakuwa na crisis ya upungufu mkubwa wa ajira na
ongezeko kubwa la graduates mitaani kuliko kipindi chochote kile katika historia ya nchi yetu!
Ni changamoto nzuri kiuchumi lakini itatumaliza kisiasa.
Serikali iweke mkakati wa kuwajengea uwezo wa kujiajiri hii critical mass mapema kabla bomu hili halijailipua CCM 2015!
" says kigwangala."
Nionavyo mimi pia ni kweli kwamba hili ni janga jipya,...ni zuri kwa wapinzani
kwani litachangia kuiondoa ccm madarakani,lakini halita wasaidia wapinzani sana baada ya hapo
maana tatizo hilo hilo laweza kuwaondoa madarakani pia.
Ni vyema sasa serikali ikaangalia jinsi ya kuwawezesha wasomi ili wajiajiri wao wenyewe.
Kwa mfano:-
UDSM,DIT,ARIDHI etc wana hitimu ma-injinia kila mwaka,lakini wote huenda kutafuta ajira kwenye makampuni makubwa
na huko huwa watumishi wa kawaida tu,na possibly wengi husahau hata profession zao.
Serikali ingetoa fungu kwa Mainjinia kama hawa,then waka kabidhiwa bara bara kwa mfano ili waisimamie,
kwanza wangepata experience na tungetengeneza wataalamu kweli kweli sio wataalamu wa nadharia tu