Yapo mengi yanayoweka matumaini ya Tanzania bora baada ya hawa ndugu kuondolewa madarakani.
Hawa ndugu wameshindwa kujifunza wala kubadilika pamoja na kupigiwa kelele mno. Kwamba ni lipi hawakuambiwa?
1. Ni hii misafara mirefu yenye kutuweka barabarani bila ukomo kuwapa wao nafasi ya kupita kwa starehe zao?
2. Ni hii misafara ya magari kibao, madege juu au wapambe kusimama nyuma yao wanapohotubu? Mbona kwa beberu au yule mwamba wa M23 siyo hivyo?
3. Nini uhalali wa gharama kubwa za matibabu au mortuary kwenye hospitali za umma?
4. Kulikoni familia zile zile kuwa wao ndiyo wenye haki na keki ya taifa hili?
5. Vipi ajira serikalini kutokuwa za mkataba usiokuwa wa kudumu usiozidi angalau miaka 8 ili kuwapa nafasi na wengine?
6. Vipi wananchi wote katika nchi kutokushirikishwa kikamilifu serikalini kwenye ujenzi wa nchi hii?
7. Kwanini raslimali zetu kutokuwepo kikamilifu kwenye kuchangia katika ustawi wa maisha ya watu?
8. Kwanini watu kupotea, kuuwawa, kuteswa au kukamatwa pasipokuwa na uhalali?
9. Kwanini dhuluma na vyombo vya Dola?
10. Kwanini vilio vya maisha magumu ya watu kuangukia kwenye masikio viziwi?
11. Nk, nk.
Upinzani ni muhimu kujitenga na ya namna hiyo mapema, ambayo ni kero kubwa kwa wananchi.
Viongozi wa wananchi hawawezi kujitenga kiasi cha kujidhania wao ni miungu na watu ni watuhumiwa ama eti ni wahalifu sugu.
Sheria za nchi haziwezi kuelekezwa kwenye kuwapora watu mali zao.
Upinzani mjitafakari kujitofautisha kabisa na hawa watu kwani biashara ni asubuhi.
Hawa ndugu wameshindwa kujifunza wala kubadilika pamoja na kupigiwa kelele mno. Kwamba ni lipi hawakuambiwa?
1. Ni hii misafara mirefu yenye kutuweka barabarani bila ukomo kuwapa wao nafasi ya kupita kwa starehe zao?
2. Ni hii misafara ya magari kibao, madege juu au wapambe kusimama nyuma yao wanapohotubu? Mbona kwa beberu au yule mwamba wa M23 siyo hivyo?
3. Nini uhalali wa gharama kubwa za matibabu au mortuary kwenye hospitali za umma?
4. Kulikoni familia zile zile kuwa wao ndiyo wenye haki na keki ya taifa hili?
5. Vipi ajira serikalini kutokuwa za mkataba usiokuwa wa kudumu usiozidi angalau miaka 8 ili kuwapa nafasi na wengine?
6. Vipi wananchi wote katika nchi kutokushirikishwa kikamilifu serikalini kwenye ujenzi wa nchi hii?
7. Kwanini raslimali zetu kutokuwepo kikamilifu kwenye kuchangia katika ustawi wa maisha ya watu?
8. Kwanini watu kupotea, kuuwawa, kuteswa au kukamatwa pasipokuwa na uhalali?
9. Kwanini dhuluma na vyombo vya Dola?
10. Kwanini vilio vya maisha magumu ya watu kuangukia kwenye masikio viziwi?
11. Nk, nk.
Upinzani ni muhimu kujitenga na ya namna hiyo mapema, ambayo ni kero kubwa kwa wananchi.
Viongozi wa wananchi hawawezi kujitenga kiasi cha kujidhania wao ni miungu na watu ni watuhumiwa ama eti ni wahalifu sugu.
Sheria za nchi haziwezi kuelekezwa kwenye kuwapora watu mali zao.
Upinzani mjitafakari kujitofautisha kabisa na hawa watu kwani biashara ni asubuhi.