Tanzania Black Friday ya nini?

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,244
113,628
Jana tarehe 23, Novemba 2023 ilikuwa ni sikukuu ya Thanksgiving nchini Marekani.

Kama hujui sikukuu hiyo ina maana gani huko Marekani, zama Google au YouTube [zote hizo ni kampuni za Kimarekani 😉 🇺🇸] ufute ujinga.

Thanksgiving huwa ni siku ya Alhamisi ya mwisho ya mwezi Novemba kila mwaka.

Siku ifuatayo, yaani Ijumaa, huwa inajulikana kama Black Friday.

Black Friday ni siku ambayo madukani kunakuwepo na mapunguzo makubwa ya bei za vitu/ bidhaa.

Zamani kabla ya masoko ya mtandaoni hayajaenea na kuzoeleka, watu walikuwa wanaenda kupiga kambi kabisa nje ya maduka kama Best Buy ili kuwahi kuwa wa kwanza kuingia madukani humo pindi milango inapofunguliwa.

Ilikuwa ni vurugu sana. Watu walikuwa wanapigana. Wengine walikuwa wanakanyagana hadi kuuana kabisa.

Siku hizi hakuna sana hizo vurugu maana manunuzi watu wanafanyia kwenye mitandao.

Sasa cha kushangaza, eti hata Tanzania leo ni Black Friday!

IMG_5548.jpeg


Ina maana Tanzania nako wanasherehekea Thanksgiving siku hizi?

Wameanza lini kusherehekea sikukuu za Marekani? Na July 4th nayo wanaisherehekea?

Kubalini, kataeni, chukieni, oneni wivu, jibamizeni ukutani, mwisho wa siku Marekani ndo taifa bora kabisa kuwahi kutokea katika historia ya uhai!

Kama mnaiga hata black Friday, basi Marekani imewakamata panapo vizuri sana.

🇺🇸🇺🇸🇺🇸🇺🇸🇺🇸🇺🇸
 
Jana tarehe 23, Novemba 2023 ilikuwa ni sikukuu ya Thanksgiving nchini Marekani.

Kama hujui sikukuu hiyo ina maana gani huko Marekani, zama Google au YouTube [zote hizo ni kampuni za Kimarekani 😉 🇺🇸] ufute ujinga.

Thanksgiving huwa ni siku ya Alhamisi ya mwisho ya mwezi Novemba kila mwaka.

Siku ifuatayo, yaani Ijumaa, huwa inajulikana kama Black Friday.

Black Friday ni siku ambayo madukani kunakuwepo na mapunguzo makubwa ya bei za vitu/ bidhaa.

Zamani kabla ya masoko ya mtandaoni hayajaenea na kuzoeleka, watu walikuwa wanaenda kupiga kambi kabisa nje ya maduka kama Best Buy ili kuwahi kuwa wa kwanza kuingia madukani humo pindi milango inapofunguliwa.

Ilikuwa ni vurugu sana. Watu walikuwa wanapigana. Wengine walikuwa wanakanyagana hadi kuuana kabisa.

Siku hizi hakuna sana hizo vurugu maana manunuzi watu wanafanyia kwenye mitandao.

Sasa cha kushangaza, eti hata Tanzania leo ni Black Friday!

View attachment 2823288

Ina maana Tanzania nako wanasherehekea Thanksgiving siku hizi?

Wameanza lini kusherehekea sikukuu za Marekani? Na July 4th nayo wanaisherehekea?

Kubalini, kataeni, chukieni, oneni wivu, jibamizeni ukutani, mwisho wa siku Marekani ndo taifa bora kabisa kuwahi kutokea katika historia ya uhai!

Kama mnaiga hata black Friday, basi Marekani imewakamata panapo vizuri sana.

🇺🇸🇺🇸🇺🇸🇺🇸🇺🇸🇺🇸
Piga box mkuu achana na wabongo hatuna dogo sisi.
 
Back
Top Bottom