Tanzanized S
New Member
- May 3, 2024
- 3
- 3
Tanzania iko katika wakati muhimu sana katika safari yake ya maendeleo. Kama Taifa ni muhimu kuandaa ramani ambayo itakuwa muongozo wetu kwa miaka 20 ijayo, ramani ambayo itagusa sekta zote muhimu katika ustawi wa nchi. Katika makala hii nimeelezea mpango wa maendeleo tunaoweza kuutumia;
Ramani ya Ukanda wa Afrika Mashariki ikionesha uelekeo wa Kimbunga Hidaya katika pwani ya Tanzania. Source: Zoom Earth
Afya: Katika sekta ya afya serikali ilenge kuwapatia raia wote bima ya afya ya msingi kabla ya mwaka 2044.
Ihakikishe kwamba huduma bora za afya zinawafikia wananchi wote, mijini na vijijini. Hili litafanikishwa kwa kuimarisha miundombinu ya afya, kutoa mafunzo hitajika kwa wahudumu wa afya na kupeleka wataalamu zaidi katika maeneo ya vijijini.
Aidha, hatua za kinga ya afya zipewe kipaumbele kwa kutekeleza kampeni za chanjo kwa magonjwa yanayozuilika kwa chanjo, bila kusahau kipaumbele kwenye afya ya uzazi na watoto kwa ustawi wa vizazi vijavyo.
JP Magufuli akikagua mashine ya kupiga picha za viungo ndani ya mwili (MRI Scan). Source: MNH Mloganzila
Elimu: Kufikia mwaka 2044, Tanzania iwe na mfumo imara wa elimu utakaohakikisha upatikanaji wa elimu kwa raia wote bila kujali tofauti zao za kiuchumi.
Pamoja na suala la elimu bure kwa shule za msingi mpaka sekondari, serikali ifanye uwekezaji katika miundombinu ya elimu kwa kujenga shule za kisasa na vituo vya elimu ya ufundi katika maeneo yenye uhitaji.
Aidha, Mtaala wa elimu ufanyiwe marekebisho yatakayosaidia kukuza uwezo wa kufikiri kwa kina na kutatua matatizo bila kusahau kuwajengea wanafunzi ujuzi wa kidijitali ili kuwaandaa kwa changamoto za soko la ajira la karne ya 21.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Pamba wakijisomea wenyewe kwenye chumba maalum cha kompyuta. Source: pambasec.blogspot.com
Mazingira: Udhibiti wa mazingira upewe kipaumbele katika ajenda ya maendeleo ya Tanzania.
Ili taifa letu liweze kuhifadhi urithi wake wa asili na kuurithisha kwa vizazi vijavyo tunapaswa kudhibiti uwiano kati ya shughuli za kiuchumi na uhifadhi wa mazingira.
Pamoja na juhudi za kupanda miti, serikali ihamasishe matumizi ya nishati jadidifu ili kupunguza uzalishaji wa hewa ya ukaa.
Matumizi ya Nishati safi ya gesi kupikia
Teknolojia: Katika kipindi cha miaka 20 ijayo, inawezekana kabisa kwa Tanzania kuwa kitovu cha Afrika Mashariki na kati katika suala zima la teknolojia na uvumbuzi.
Hilo litatimia kama tu serikali itaamua kwa nia ya dhati kabisa kuwekeza katika kuboresha miundombinu ya mawasiliano ili kurahisisha upatikanaji wa intaneti katika maeneo yote nchini.
Serikali iongeze uwekezaji katika tafiti na kuboresha sera za uwekezaji katika teknolojia ili kuchochea uanzishwaji wa kampuni za kidijitali.
Matumizi ya teknolojia yataimarisha utoaji wa huduma katika sekta mbalimbali kama vile kilimo, fedha, na utawala hivyo kurahisisha maisha.
Kiwanda cha kutengeneza magari aina ya Toyota. Source: Bloomberg
Uchumi: Ili kukuza uchumi wa taifa na mtu mmoja mmoja serikali ihamasishe wafanyabiashara kuwekeza katika Viwanda vidogo vidogo na vya kati kwa kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji.
Kufanya hivyo kutasaidia kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira jambo litakalosaidia kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja na kuondoa utegemezi wa bidhaa kutoka nje huku mauzo ya bidhaa zilizoongezewa thamani nje ya nchi yakiliongezea taifa mapato na fedha za kigeni.
Pamoja na sekta ya uzalishaji viwandani, serikali ihakikishe sekta nyingine zinazoliingizia taifa fedha za kigeni zinafanyiwa uwekezaji utakaochochea ukuaji wake zaidi.
Katika Utalii kwa mfano; pamoja na ujenzi wa barabara za lami, serikali ijenge viwanja vya ndege katika maeneo yote ya kitalii nchini ili yaweze kufikika kwa urahisi.
Mkia wa ndege ya ATC aina ya Boeing 737 mwaka 1995. Source: Wikipedia
Miundombinu mingine ya utalii kama ujenzi wa hoteli ichangamkiwe na wawekezaji wa ndani ili pesa wanazotumia watalii katika hoteli hizo zibaki hapa nchini.
Sekta nyingine ya muhimu kwa uchumi wetu ni Kilimo. Katika kilimo serikali ihakikishe upatikanaji wa pembejeo ni wa uhakika katika maeneo yote nchini.
Ikibidi, gharama inayotumika kuweka ruzuku kwenye mbolea ielekezwe katika ujenzi wa viwanda vya kuzalisha mbolea hapa nchini ili kuokoa fedha zetu.
Sekta ya kilimo ikisimamiwa vizuri, si tu kwamba tutakuwa na uhakika wa chakula nchini lakini pia tutakidhi mahitaji ya malighafi katika viwanda vyetu.
Usalama: Kwa kutambua umuhimu wa amani na usalama katika maendeleo ya nchi, ndani ya miaka 20 ijayo Tanzania iimarishe mfumo wake wa ulinzi ili kuwa tayari kudhibiti matishio ya amani yanayoweza kujitokeza. Mfano; Ugaidi, Uvamizi wa kimataifa, na mashambulizi ya kimtandao.
Wanajeshi wa Tanzania wakiwa kwenye mafunzo maalum kwa ajili ya mission ya MONUSCO chini ya UN. Source: Wikipedia
Hii ijumuishe kuimarisha uwezo wa kutekeleza sheria ili kudhibiti matukio ya uhalifu yanayotokea mara kwa mara nchini.
Pia serikali iwekeze katika ukusanyaji na uchambuzi wa taarifa za kijasusi, na kuimarisha zaidi sera yetu ya mambo ya nje kwa kukuza ushirikiano wa kikanda katika kushughulikia changamoto za kiusalama katika nchi jirani zinazoweza kuvuka mipaka.
Kwa kuhitimisha, Dira ya maendeleo kwa miaka 20 ijayo ilenge kuwa na taifa lenye maendeleo kiuchumi na jamii yenye ustawi inayoishi kwa amani bila hofu za kiusalama.
Kwa kuweka kipaumbele katika sekta hizo na nyingine ambazo sijazigusa kama Madini, Uchumi wa Blue n.k, Tanzania inaweza kupiga hatua kubwa mno kimaendeleo na kuwa miongoni mwa mataifa 5 tajiri zaidi barani Afrika.
Ili yote hayo yatimie tunahitaji Uongozi thabiti utakaoweza kusimamia utekelezaji wake bila kuyumbishwa.
MWISHO!
Ramani ya Ukanda wa Afrika Mashariki ikionesha uelekeo wa Kimbunga Hidaya katika pwani ya Tanzania. Source: Zoom Earth
Afya: Katika sekta ya afya serikali ilenge kuwapatia raia wote bima ya afya ya msingi kabla ya mwaka 2044.
Ihakikishe kwamba huduma bora za afya zinawafikia wananchi wote, mijini na vijijini. Hili litafanikishwa kwa kuimarisha miundombinu ya afya, kutoa mafunzo hitajika kwa wahudumu wa afya na kupeleka wataalamu zaidi katika maeneo ya vijijini.
Aidha, hatua za kinga ya afya zipewe kipaumbele kwa kutekeleza kampeni za chanjo kwa magonjwa yanayozuilika kwa chanjo, bila kusahau kipaumbele kwenye afya ya uzazi na watoto kwa ustawi wa vizazi vijavyo.
JP Magufuli akikagua mashine ya kupiga picha za viungo ndani ya mwili (MRI Scan). Source: MNH Mloganzila
Elimu: Kufikia mwaka 2044, Tanzania iwe na mfumo imara wa elimu utakaohakikisha upatikanaji wa elimu kwa raia wote bila kujali tofauti zao za kiuchumi.
Pamoja na suala la elimu bure kwa shule za msingi mpaka sekondari, serikali ifanye uwekezaji katika miundombinu ya elimu kwa kujenga shule za kisasa na vituo vya elimu ya ufundi katika maeneo yenye uhitaji.
Aidha, Mtaala wa elimu ufanyiwe marekebisho yatakayosaidia kukuza uwezo wa kufikiri kwa kina na kutatua matatizo bila kusahau kuwajengea wanafunzi ujuzi wa kidijitali ili kuwaandaa kwa changamoto za soko la ajira la karne ya 21.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Pamba wakijisomea wenyewe kwenye chumba maalum cha kompyuta. Source: pambasec.blogspot.com
Mazingira: Udhibiti wa mazingira upewe kipaumbele katika ajenda ya maendeleo ya Tanzania.
Ili taifa letu liweze kuhifadhi urithi wake wa asili na kuurithisha kwa vizazi vijavyo tunapaswa kudhibiti uwiano kati ya shughuli za kiuchumi na uhifadhi wa mazingira.
Pamoja na juhudi za kupanda miti, serikali ihamasishe matumizi ya nishati jadidifu ili kupunguza uzalishaji wa hewa ya ukaa.
Matumizi ya Nishati safi ya gesi kupikia
Teknolojia: Katika kipindi cha miaka 20 ijayo, inawezekana kabisa kwa Tanzania kuwa kitovu cha Afrika Mashariki na kati katika suala zima la teknolojia na uvumbuzi.
Hilo litatimia kama tu serikali itaamua kwa nia ya dhati kabisa kuwekeza katika kuboresha miundombinu ya mawasiliano ili kurahisisha upatikanaji wa intaneti katika maeneo yote nchini.
Serikali iongeze uwekezaji katika tafiti na kuboresha sera za uwekezaji katika teknolojia ili kuchochea uanzishwaji wa kampuni za kidijitali.
Matumizi ya teknolojia yataimarisha utoaji wa huduma katika sekta mbalimbali kama vile kilimo, fedha, na utawala hivyo kurahisisha maisha.
Kiwanda cha kutengeneza magari aina ya Toyota. Source: Bloomberg
Uchumi: Ili kukuza uchumi wa taifa na mtu mmoja mmoja serikali ihamasishe wafanyabiashara kuwekeza katika Viwanda vidogo vidogo na vya kati kwa kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji.
Kufanya hivyo kutasaidia kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira jambo litakalosaidia kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja na kuondoa utegemezi wa bidhaa kutoka nje huku mauzo ya bidhaa zilizoongezewa thamani nje ya nchi yakiliongezea taifa mapato na fedha za kigeni.
Pamoja na sekta ya uzalishaji viwandani, serikali ihakikishe sekta nyingine zinazoliingizia taifa fedha za kigeni zinafanyiwa uwekezaji utakaochochea ukuaji wake zaidi.
Katika Utalii kwa mfano; pamoja na ujenzi wa barabara za lami, serikali ijenge viwanja vya ndege katika maeneo yote ya kitalii nchini ili yaweze kufikika kwa urahisi.
Miundombinu mingine ya utalii kama ujenzi wa hoteli ichangamkiwe na wawekezaji wa ndani ili pesa wanazotumia watalii katika hoteli hizo zibaki hapa nchini.
Sekta nyingine ya muhimu kwa uchumi wetu ni Kilimo. Katika kilimo serikali ihakikishe upatikanaji wa pembejeo ni wa uhakika katika maeneo yote nchini.
Ikibidi, gharama inayotumika kuweka ruzuku kwenye mbolea ielekezwe katika ujenzi wa viwanda vya kuzalisha mbolea hapa nchini ili kuokoa fedha zetu.
Sekta ya kilimo ikisimamiwa vizuri, si tu kwamba tutakuwa na uhakika wa chakula nchini lakini pia tutakidhi mahitaji ya malighafi katika viwanda vyetu.
Usalama: Kwa kutambua umuhimu wa amani na usalama katika maendeleo ya nchi, ndani ya miaka 20 ijayo Tanzania iimarishe mfumo wake wa ulinzi ili kuwa tayari kudhibiti matishio ya amani yanayoweza kujitokeza. Mfano; Ugaidi, Uvamizi wa kimataifa, na mashambulizi ya kimtandao.
Wanajeshi wa Tanzania wakiwa kwenye mafunzo maalum kwa ajili ya mission ya MONUSCO chini ya UN. Source: Wikipedia
Hii ijumuishe kuimarisha uwezo wa kutekeleza sheria ili kudhibiti matukio ya uhalifu yanayotokea mara kwa mara nchini.
Pia serikali iwekeze katika ukusanyaji na uchambuzi wa taarifa za kijasusi, na kuimarisha zaidi sera yetu ya mambo ya nje kwa kukuza ushirikiano wa kikanda katika kushughulikia changamoto za kiusalama katika nchi jirani zinazoweza kuvuka mipaka.
Kwa kuhitimisha, Dira ya maendeleo kwa miaka 20 ijayo ilenge kuwa na taifa lenye maendeleo kiuchumi na jamii yenye ustawi inayoishi kwa amani bila hofu za kiusalama.
Kwa kuweka kipaumbele katika sekta hizo na nyingine ambazo sijazigusa kama Madini, Uchumi wa Blue n.k, Tanzania inaweza kupiga hatua kubwa mno kimaendeleo na kuwa miongoni mwa mataifa 5 tajiri zaidi barani Afrika.
Ili yote hayo yatimie tunahitaji Uongozi thabiti utakaoweza kusimamia utekelezaji wake bila kuyumbishwa.
MWISHO!