TANROADS: Serikali imetoa zaidi ya Tsh. Bilioni 567 kuboresha barabara za Kigoma

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049
Meneja wa TANROADS Kigoma, Mhandisi Narcis Choma amesema Serikali imetoa fedha zaidi ya Tsh. Bilioni 567 kwa ajili ya ujenzi wa miradi mbalimbali ya barabara yenye jumla ya urefu wa Kilometa 420 zinazojengwa kwa kiwango cha lami kwa wakati mmoja mkoani hapo.
IMG-20230422-WA0024.jpg

Amesema: “Hiki kinachofanywa na Serikali ya Rais Samia Suluhu hakijawahi kutokea, kuna Barabara 9 zinazojengwa Mkoa wa Kigoma, hilo ni jambo kubwa.”

Ameongeza kwa kusema “Tunawashauri Wananchi kutoka mikoa tofautitofauti waje kuwekeza Kigoma kwa kuwa mji unafunguka na kumekucha, fursa zipo nyingi na wanakaribishwa kwa ajili ya kufanya uwekezaji.”

Amesema wakati miradi hiyo ya barabara ikiendelea, pia itaambatana na miradi mingine ya ziada, jumla ya Tsh. Bilioni 23 itatumika kukamilisha kazi hiyo.

Ameeleza “Baadhi ya maeneo yatafaidika na vituo vya afya, visima, ukarabati wa hospitali, shule na stendi. Baadhi ya maeneo yatakayofaidika ni Kasulu, Makele na Kibondo.

Aidha, ameongeza kuwa kuna mchato wa uboreshaji wa Uwanja wa Ndege wa Kigoma ikiwa ni sehemu ya miradi sanifu ambayo inatarajiwa kufanyika mkoani hapo.

“Kutajengwa jengo jipya ya abiria, sehemu ya kuegesha ndege, barabara za kuingia uwanja wa ndege, sehemu ya kuegesha magari, control tower mpya, ofisi ya Fire, kituo kidogo cha kupoozea umeme na uzio, pia kutawekwa taa sehemu ya ndege kutua ambayo itawezesha ndege kutua hadi usiku,” amesema Mhandisi Narcis Choma

Akielezea kuhusu mradi wote anaeleza umegawanyika katika hatua nne, kwanza ni Manyovu - Kasulu (Kilometa 68.25), pili ni Kidyama-Mvugwe (Kilometa 70.5), tatu ni Mvugwe – Nduta (Kilometa 59) na nne ni Nduta-Kabingo (Kilometa 62.25).

Hatua ya Kwanza (Lot 1)
IMG-20230422-WA0053.jpg
IMG-20230422-WA0052.jpg
IMG-20230422-WA0055.jpg
IMG-20230422-WA0054.jpg

Mhandisi Laurent Gervance Mtayangurwa ambaye ni Mhandisi wa Mshauri wa Mradi, amesema wanaongeza nguvu ya ujenzi licha ya kuwa kumekuwa na mazingira ya mvua.

Lot 1 inahusisha Barabara ya Manyovu-Kasulu (Kilometa 68.25) na kuna madaraja makubwa matatu na madaraja ya boksi karavati 8, kati ya hayo 6 yamekamilika ujenzi wake.

Ameweka wazi kuwa katika kipande hicho kuna madaraja mengine yanayofahamika kwa jina la caravan pipes yapo 68 na kati ya hayo 56 yameshakamilika.

Amesema maendeleo ya mradi huo unatarajia kuchukua miezi 36 ni mazuri na gharama ya mradi katika kipande hicho ni Tsh. Bilioni 76.1.

Kuhusu ajira, amesema jumla wapo Wafanyakazi 192 ambao wote ni Watanzania na pia kuna raia wa kigeni 12.

Hatua ya maendeleo iliyofikiwa ni 47.12%.


Hatua ya Pili (Lot 2)
IMG-20230422-WA0045.jpg
IMG-20230422-WA0041.jpg

IMG-20230422-WA0044(1).jpg
IMG-20230422-WA0054.jpg

Mhandisi Narcis Choma anasema kipande cha mradi huo ni unaoanzia makutano ya Kanyani na kuishia Mvugwe (Kilometa 70.5) una gharama ya Tsh. Bilioni 83.7.

Ameeleza kuwa hatua ya mradi ilipofikia ni 56.14%, ukiwa nyuma kidogo kwa kiwango cha 0.5 ya mipango ambayo iliwekwa awali kuhusu matarajio.

“Tungempa mkandarasi mmoja barabara yote kwa maana hawamu zote nne, isingekuwa na ufanisi na kasi kama ilivyo sasa ndio maana tumegawa katika vipande vinne, hivyo kasi ni nzuri na tunategemea utaisha ndani ya muda tuliopanga.

“Mradi huu una faida kubwa kwa kuwa Wakazi wa Kigoma wamekuwa na changamoto ya kutokuwa na barabara za lami kwa muda mrefu, hivyo barabara hii itarahisisha shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii,” anasema Mhandisi Narcis Choma.

Naye, Reginald Kaganga ambaye ni Mhandisi Mshauri wa sehemu ya pili anasema mradi huo unatarajiwa kukamilika Oktoba 23, 2023.

Amesema “Natoa wito kwa Mkandarasi aongeze vifaa ili aendane na mpango kazi ambao aliuwasilisha kwetu wakati anaomba tenda.”

Hatua ya Tatu (Lot 3)

Mhandisi Narcis Choma anasema mradi huo wa Mvugwe – Nduta una barabara yenye urefu wa Kilometa 59.3 na gharama ya mradi ni Tsh. Bilioni 84.7, ujenzi wake ukiwa umefikia katika kiwango cha 86%.

Kuhusu masuala ya kiufundi zaidi kuhusu mradi huo, Mhandisi Sebastian Kisandu anasema ulianza Oktoba 26, 2020 na unatarajia kukamilika Oktoba 26, 2026 ambapo tayari wamekamilisha kiwango cha lami kwa urefu wa Kilometa 20.
IMG-20230422-WA0042.jpg
IMG-20230422-WA0046.jpg
IMG-20230422-WA0050.jpg

Kutoka Kibondo hadi Nyakanazi lami imeshakamilika
 
Ccm ilituchelewesha sana kigoma tunataka na soko la kimataifa sasa ili congo na burundi tuwakamate vizuri na bandari ya kisasa
 
Ndani ya Miaka Miwili ya rais Samia, Tanroads imepewa Bilioni 567 za Kujenga Kilometa 420 kwa Mkoa wa Kigoma tu. Hadi sasa km 100 zimejengwa.

Hii hapa ni miradi ya barabara ambayo inaendelea hadi sasa hivi Mkoani Kigoma yote.

1. Mradi wa ujenzi wa Barabara ya kazilambwa (Tabora) Chagu (Kigoma) 36km kwa kiwango cha lami. Hadi sasa 82% imejengwa. - Kuanza kwa mradi ni tarehe 03/08/2020

2. Mradi wa ujenzi wa Barabara sehemeu ya Malagarasi – ilunde uvinza 51.1Km kiwango cha lami. Hadi sasa 31% imejengwa. - Kuanza kwa mradi tarehe 07/10/2021

3. Mradi wa ujenzi wa Barabara ya Manyovu Kasulu – Kibondo – Kabingo kwa kiwango cha lami 260.6Km. Imegawanyika katika LOTS 4.

LOT: I. – Kasulu – Manyovu naviunganishi vyake 68.25Km kwa kiwango cha lami (Super pave). Hadi sasa 47.12% imejengwa.
- Kuanza kwa mradi tarehe 14/09/2020.

LOT: II. – Kanyani – Mvugwe (70.5Km). Hadi sasa 54.00% imejengwa. - Kuanza kwa mradi tarehe 23/10/2022

LOT: III. –Mvugwe – Njiapanda (59.35Km). Hadi sasa 66.3% imejengwa. - Kuanza kwa mradi tarehe 26/10/2020

LOT: IV. –Nduta - Kabingo (62.5Km). Hadi sasa 78.5% zimejengwa. - Kuanza kwa mradi tarehe 17/12/2020

4. Mradi wa ujenzi wa barabara sehemu ya Njia panda Nduta Kibondo Mjini (25.9km). Hadi sasa 57.3% zimejengwa. - Kuanza kwa mradi tarehe 03/7/2020

5. Mradi wa ujezi wa barabara ya Kibondo – Mabamba mpakani mwa Burundi (47.93) kwa kiwango cha lami. - Maendeleo ya mradi yapo katika design. - Mkataba umesainiwa tarehe 8/01/2023

Barabara Kibondo hadi Nyakanazi yote sasa ni lami
20230422_155530.jpg
IMG-20230422-WA0091.jpg
IMG-20230422-WA0092.jpg
IMG-20230422-WA0085.jpg
IMG-20230422-WA0084.jpg
IMG-20230420-WA0002(2).jpg
IMG-20230420-WA0063(1).jpg
IMG-20230420-WA0060(1).jpg
IMG-20230420-WA0054.jpg
IMG-20230420-WA0062(1).jpg
IMG-20230420-WA0061.jpg
IMG-20230420-WA0057(1).jpg
IMG-20230420-WA0058(2).jpg
IMG-20230420-WA0055(1).jpg
IMG-20230420-WA0069(1).jpg
IMG-20230422-WA0021.jpg
IMG-20230422-WA0065(1).jpg
IMG-20230422-WA0057.jpg
IMG-20230422-WA0056.jpg
IMG-20230422-WA0028.jpg
IMG-20230422-WA0053(1).jpg
IMG-20230422-WA0052(1).jpg
IMG-20230422-WA0054(1).jpg
IMG-20230422-WA0045(1).jpg
IMG-20230422-WA0043.jpg
IMG-20230422-WA0042(1).jpg
IMG-20230422-WA0041(1).jpg
IMG-20230422-WA0063.jpg
IMG-20230422-WA0066.jpg
 
Naona kama wewe ni mdau. Mngefungua ID ya ofisi kabisa, ili pia iwe rahisi kupata ufafanuzi wa mambo mengine.
 
Isiwe lami ya kubumba tuu ambayo italeta gharama kuumbwa baadae kuzifanyia matengenezo ya mara kwa mara na kuleta usumbufu kwa watumiaji
 
Ndani ya Miaka Miwili ya rais Samia
Bwashee mbona naona kuna miradi mingine (mingi) ilianza wakati wa mwamba Mwakeye Mzilankende (rip) 2020, lakini wewe umeamua kutoa sifa zote kwa miaka miwili ya rais Samia peke yake?
Sina tatizo na rais Samia kusifiwa kwa kazi anazofanya, lakini mtu unapoamua kusema uongo kwa lengo la kumsifia rais, hapo ndipo sikubaliani.
 
Bwashee mbona naona kuna miradi mingine (mingi) ilianza wakati wa mwamba Mwakeye Mzilankende (rip) 2020, lakini wewe umeamua kutoa sifa zote kwa miaka miwili ya rais Samia peke yake?
Sina tatizo na rais Samia kusifiwa kwa kazi anazofanya, lakini mtu unapoamua kusema uongo kwa lengo la kumsifia rais, hapo ndipo sikubaliani.
Sukuma gang bwana 😂😂, miradi ikisuasua mnasema sababu JPM kafariki. Miradi ikikamilishwa mnataka sifa ziende kwa JPM. Yaani mradi ulioanza 2020 Leo hii 2023 unataka aseme JPM ndio kajenga? Kwamba akiwa kaburini ameagiza wahandisi waende site? 😂😂.

Poleni sana
 
Bwashee mbona naona kuna miradi mingine (mingi) ilianza wakati wa mwamba Mwakeye Mzilankende (rip) 2020, lakini wewe umeamua kutoa sifa zote kwa miaka miwili ya rais Samia peke yake?
Sina tatizo na rais Samia kusifiwa kwa kazi anazofanya, lakini mtu unapoamua kusema uongo kwa lengo la kumsifia rais, hapo ndipo sikubaliani.
Kwahiyo Mkuu unataka Kila Kitu Aandikwe Magufuli? Hizi ni hela zimetoka kuendelez miradi ndani ya miaka miwili huko Kigoma. Magufuli alikuwa kashakufa. Sasa nimtaje wapi? Nielekeze sehemu ya kutaja nimfix hapo aonekane alikuwepo hela zilipokuwa zinatoka.. Sina chuki na mzilankende. Ndani ya Miaka miwili ya Samia, au hizo Bilioni 567 zilizotolewa, Wapi Magufuli alitakiwa kuandikwa ili ionekane anahusika? Nirekebishe
 
Kwahiyo Mkuu unataka Kila Kitu Aandikwe Magufuli? Hizi ni hela zimetoka kuendelez miradi ndani ya miaka miwili huko Kigoma. Magufuli alikuwa kashakufa. Sasa nimtaje wapi? Nielekeze sehemu ya kutaja nimfix hapo aonekane alikuwepo hela zilipokuwa zinatoka.. Sina chuki na mzilankende. Ndani ya Miaka miwili ya Samia, au hizo Bilioni 567 zilizotolewa, Wapi Magufuli alitakiwa kuandikwa ili ionekane anahusika? Nirekebishe
Tatizo siyo kumtaja au kumfix Magufuli, Magu hahitaji kutajwa ili aonekane, alishajipambanua zamani.
Tatizo ni uandishi wa kichawachawa. Kujaribu kuaminisha watu kuwa mafanikio yote yamepatikana ndani ya miaka miwili wakati miradi ilianza mapema kabla.
Huhitaji kurekebisha popote, just be objective. Nyie kama vijana tunaowategemea kuleta mabadiliko kwenye taifa letu, mnapaswa kufanya mambo nje ya box ili kujipambanua kuwa we can rely on you.
 
Sukuma gang bwana 😂😂, miradi ikisuasua mnasema sababu JPM kafariki. Miradi ikikamilishwa mnataka sifa ziende kwa JPM. Yaani mradi ulioanza 2020 Leo hii 2023 unataka aseme JPM ndio kajenga? Kwamba akiwa kaburini ameagiza wahandisi waende site? 😂😂.

Poleni sana
Wewe huna nyimbo zaidi ya kupalilia ubaguzi wa kikabila, sihitaji kukujibu.
 
Isiwe lami ya kubumba tuu ambayo italeta gharama kuumbwa baadae kuzifanyia matengenezo ya mara kwa mara na kuleta usumbufu kwa watumiaji
Ila watanzania mnapenda sana kulalamika na kulaumu tuuu. Mngekuwa enzi za huko nyuma, nadhani kizazi chenu ingekuwa kishafutwa duniani. Hamna jema kwenu.
 
Sukuma gang bwana 😂😂, miradi ikisuasua mnasema sababu JPM kafariki. Miradi ikikamilishwa mnataka sifa ziende kwa JPM. Yaani mradi ulioanza 2020 Leo hii 2023 unataka aseme JPM ndio kajenga? Kwamba akiwa kaburini ameagiza wahandisi waende site? 😂😂.

Poleni sana
Hawa watu wa hovyo sana. Ile miradi ya Jakaya sifa anapewa JPM, ukiuliza wanakwambia alikuwa Waziri wa Ujenzi. Ukiwauliza hii miradi ya JPM akiwa Rais kwanini Basi sifa hampeleki kwa Waziri wake wa Ujenzi, wanabaki kufura tu. Sukumagang ni moja ya kirusi Kibaya sana Tanzania kwa Sasa.
 
Hawa watu wa hovyo sana. Ile miradi ya Jakaya sifa anapewa JPM, ukiuliza wanakwambia alikuwa Waziri wa Ujenzi. Ukiwauliza hii miradi ya JPM akiwa Rais kwanini Basi sifa hampeleki kwa Waziri wake wa Ujenzi, wanabaki kufura tu. Sukumagang ni moja ya kirusi Kibaya sana Tanzania kwa Sasa.
Nonsense
 
Mm nimefurahi sana mkuu passioner kwa uzi huu wapo watu humu ndani wanajenga picha kwamba hakuna kabisa huyu mama wa watu anafanya lakini ukifika field unaona miradi inaendelea na mingine imekamilika kama.madarasa mabweni nk!
Mnyonge mnyongeni mama anafanya kazi ila kwq style tofauti kimyakimya
 
Ndani ya Miaka Miwili ya rais Samia, Tanroads imepewa Bilioni 567 za Kujenga Kilometa 420 kwa Mkoa wa Kigoma tu. Hadi sasa km 100 zimejengwa.

Hii hapa ni miradi ya barabara ambayo inaendelea hadi sasa hivi Mkoani Kigoma yote.

1. Mradi wa ujenzi wa Barabara ya kazilambwa (Tabora) Chagu (Kigoma) 36km kwa kiwango cha lami. Hadi sasa 82% imejengwa. - Kuanza kwa mradi ni tarehe 03/08/2020

2. Mradi wa ujenzi wa Barabara sehemeu ya Malagarasi – ilunde uvinza 51.1Km kiwango cha lami. Hadi sasa 31% imejengwa. - Kuanza kwa mradi tarehe 07/10/2021

3. Mradi wa ujenzi wa Barabara ya Manyovu Kasulu – Kibondo – Kabingo kwa kiwango cha lami 260.6Km. Imegawanyika katika LOTS 4.

LOT: I. – Kasulu – Manyovu naviunganishi vyake 68.25Km kwa kiwango cha lami (Super pave). Hadi sasa 47.12% imejengwa.
- Kuanza kwa mradi tarehe 14/09/2020.

LOT: II. – Kanyani – Mvugwe (70.5Km). Hadi sasa 54.00% imejengwa. - Kuanza kwa mradi tarehe 23/10/2022

LOT: III. –Mvugwe – Njiapanda (59.35Km). Hadi sasa 66.3% imejengwa. - Kuanza kwa mradi tarehe 26/10/2020

LOT: IV. –Nduta - Kabingo (62.5Km). Hadi sasa 78.5% zimejengwa. - Kuanza kwa mradi tarehe 17/12/2020

4. Mradi wa ujenzi wa barabara sehemu ya Njia panda Nduta Kibondo Mjini (25.9km). Hadi sasa 57.3% zimejengwa. - Kuanza kwa mradi tarehe 03/7/2020

5. Mradi wa ujezi wa barabara ya Kibondo – Mabamba mpakani mwa Burundi (47.93) kwa kiwango cha lami. - Maendeleo ya mradi yapo katika design. - Mkataba umesainiwa tarehe 8/01/2023

Barabara Kibondo hadi Nyakanazi yote sasa ni lami
View attachment 2596358View attachment 2596359View attachment 2596360View attachment 2596361View attachment 2596362View attachment 2596363View attachment 2596364View attachment 2596365View attachment 2596366View attachment 2596367View attachment 2596368View attachment 2596369View attachment 2596370View attachment 2596371View attachment 2596372View attachment 2596373View attachment 2596374View attachment 2596375View attachment 2596376View attachment 2596377View attachment 2596378View attachment 2596379View attachment 2596380View attachment 2596381View attachment 2596382View attachment 2596383View attachment 2596384View attachment 2596385View attachment 2596386
mkuu acha kudanganya umma barabara hizo zote wakandaras wamelala haijulikani mradi huo wa barabara kutoka nyakanazi kigoma utakamilika lini!
 
Ila watanzania mnapenda sana kulalamika na kulaumu tuuu. Mngekuwa enzi za huko nyuma, nadhani kizazi chenu ingekuwa kishafutwa duniani. Hamna jema kwenu.
Itakuwa Kiswahili hukielewi au unasoma kwa tafsiri unayoipenda ......hakuna sehemu niliyolalamika au kuonesha kulalamika ndo maana nilianza na neno (isiwe) ikiwa inasimama kuwa onyo na onyo sio ulalamishi
 
Back
Top Bottom