Tanroads Pwani, huyu mhandisi hapaswi kuwa kazini. Mapinga haharibu barabara

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Oct 20, 2014
15,333
24,227
20231105_175911.jpg
20231105_175905.jpg
20231105_175845.jpg


Si kawaida kuwasagia kunguni wahandisi wanzangu, lakini hii tunayoiona kwenye picha sijui niite uzembe, uhujumu aukukosa uelewa kabisa juu ya masuala ya barabara.

Lakini kwa vyovyote kichofanyika pale Mapinga kuelekea kilima cha Kerege , ni uharibifu ambao unaiondoa barabara ya Dar-Bagamoyo katika matumizi mazuri yanayotarajiwa.

Tunajua hapo nia ilikuwa kuweka vituta aina ya ndita.
Cha kusikitisha huyo mhandisi hajui aina ya lami iliyopo pale.
Lami iliyopo ni ile inaitwa Surface Dressing na inaweza kuwa layer moja au mbili.
Lakini kwa vyovyote lami hii ni nyembamba sana hata iliwa layer mbili, ukubwa wa 20-25mm(inchi moja).
Sasa kilichofanyika pale ni kuikata layer hiyo ili waweke lami sina nyingine(asphalt concrete). Lami hizo zimeshindwa kuumana na zimebanduka.
Kilichotokea na hasa baada ya mvua ni lami ya vituta kubanduka na layer za tabaka la chini ya barabara kuanza kulowa.
Kma kuna kansa , basi kwa barabara hii ni kansa, layer za chini zikiingia maji basi matengenezo ya barabara ni kila miezi sita.
Kansa hiyo.
Barabara imekatwa zaidi ya sehemu tano hapo Mapinga.

Sasa kwa Tanroads sijui weledi wa mainjinia wenu ukoje.
Injinia asiyeelewa mambo hayo kitaalam atafute sehemu nyingine kuajiriwa.

Hii barabara sasa hivi ndio mbadala wa Morogoro road, kwa uhujumu/uharibifu huu lazim vichwa vikatwe.
 
Picha ya eneo moja haitoshi kutoa hitimisho la kumfukuza mtu kazi.
Pengine walipaswa kuweka lami ya kushikanisha tabaka la chini ya hivyo vituta.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
View attachment 2804999View attachment 2805001View attachment 2805004

Si kawaida kuwasagia kunguni wahandisi wanzangu, lakini hii tunayoiona kwenye picha sijui niite uzembe, uhujumu aukukosa uelewa kabisa juu ya masuala ya barabara.

Lakini kwa vyovyote kichofanyika pale Mapinga kuelekea kilima cha Kerege , ni uharibifu ambao unaiondoa barabara ya Dar-Bagamoyo katika matumizi mazuri yanayotarajiwa.

Tunajua hapo nia ilikuwa kuweka vituta aina ya ndita.
Cha kusikitisha huyo mhandisi hajui aina ya lami iliyopo pale.
Lami iliyopo ni ile inaitwa Surface Dressing na inaweza kuwa layer moja au mbili.
Lakini kwa vyovyote lami hii ni nyembamba sana hata iliwa layer mbili, ukubwa wa 20-25mm(inchi moja).
Sasa kilichofanyika pale ni kuikata layer hiyo ili waweke lami sina nyingine(asphalt cincrete). Lami hizo zimeshindwa kuumana na zimebanduka.
Kilichotokea na hasa baada ya mvua ni lami ya vituta kubanduka na layer za tabaka la chini ya barabara kuanza kulowa.
Kma kuna kansa , basi kwa barabara hii ni kansa, layer za chini zikiingia maji basi matengenezo ya barabara ni kila miezi sita.
Kansa hiyo.
Sasa kwa Tanroads sijui weledi wa mainjinia wenu ukoje.
Injinia asiyeelewa mambo hayo kitaalam atafute sehemu nyingine kuajiriwa.

Hii barabara sasa hivi ndio mbadala wa Morogoro road, kwa uhujumu/uharibifu huu lazim vichwa vikatwe.
Mbona mimi naona barabara ipo shega tu. Yani watanzania hatuna shukrani na hatupendi vya kwetu. Laiti ungeona barabara za central African republic na Haiti usingeleta huu uzi.
 
Picha ya eneo moja haitoshi kutoa hitimisho la kumfukuza mtu kazi.
Pengine walipaswa kuweka lami ya kushikanisha tabaka la chini ya hivyo vituta.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kimsingi huyo Injinia hajui anafanya nini na kama hajui alichofanya ni uharibifu mkubwa sana wa kurudia lami eneo lote hilo.
Gharama yake inaweza fika milioni 400, sasa wataka watu wakenue tu!
 
Back
Top Bottom