Jacobus
JF-Expert Member
- Mar 29, 2011
- 4,708
- 1,733
- Thread starter
- #121
Sasa hata wiki haijaisha Vodacom wametoa tangazo lao. Linakupa ujumbe wa moja kwa moja kinachokusudiwa na linakufanya usisimke kwa lafudhi iliyotumika.1. Yule jamaa anamiliki gari hawezi kukosa king'amuzi kiasi cha mkewe kwenda kwa jirani kuangalia ‘continental'
2. Yule jamaa anaonekana kabisa mazingira anayoishi siyo ya uswazi kiasi eti watu wakaangalie ‘continental' kwa majirani zao, nyumba waliyokodi kua-act-ia inaonesha mazingira ya kuwa na maisha ya hali fulani ambayo ni shwari, hakuna uhalisia wa mtu wa hadhi hiyo mkewe kwenda kwa jirani kuangalia ‘continental'
2. Kwa hoja hizo walipaswa kuja na angle nyingine badala ya hiyo ya eti mke wa mtu ametoka nyumbani kwenda kuangalia continental kisa nyumbani hakuna continental.
3. Yule jirani mwenye continental haeleweki kama anacheza comedi au kitu gani, maana ni kama chizi Fulani hivi. (macho kama amekula msuba) tangazo halina maudhui, na ndo shida ya matangazo mengi ya bongo, watu wanachanganya matangazo na vichekesho visivyochekesha refer: matangazo ya Sharo billionea na matangazo ya mzee majuto, mfano lile la magodoro eti konda wa daladala anaota anapiga debe kumbe anampiga mkewe.
Kwa ufupi ni hayo tu, wapingaji wenzangu ongezeeni points.